Well kwani tulisaini mkataba wa mimi kuwepo hapa kila siku? Hihihihi usiache kusoma bana, hebu baki hapa upate stori ya Wig.
Ujue kuna siku akili inachoka alafu kunakuwa kama "empty" hivi kichwani kwa ndani, yaani hata yasiyo na maana nayo huondoka basi inakuwa ngumu kidogo kuandika ili ueleweke.
Ikifikia mahali unaandika (huku unasoma bila shaka) lakini unahisi hakileti maana....basi tambua kuwa unahitaji Mapumziko kiakili! Anyway....
Wanangu na Baba yao wamelala....Joto limewachosha, maana leo ka' tupo Kisarawe.....achana na hilo.
Nimekaa hapa nikakumbuka Wig langu la kujinyonga wenyewe mnaita Curl sijui Karikiti. Kwa kawaida mie sio mvaaji wa hayo mavitu, ila baada ya "issue" ya nywele nkasema ngoja nami niwekeze kwenye "Afro Wig".
Siku (2.5yrs ago) nkalivaa, baada ya kutoka Kazini nkaenda Chekechea kumchukua Babuu ....hee! Mtoto wacha alie alafu anaangalia juu (lilipo Wig) hehehehe....nikazuga bana mbele ya Wazungu as walijua nimebadilisha Mtindo wa nywele....kumbe sio Zangu!
Kufika garini, nikalitoa Wig langu, nikafunga Kilemba, aiii mwanangu akafurahi.....ili kuhakikisha kama kweli anaogopa Wig, siku nyingine nikalivaa nikiwa nyumbani.
Ayeee! Mtoto alilia mpaka nikaogopa. Basi bwana ikawa mimi na Wig basi, nkalihifadhi Boskini!
Jana nika-google "Afro Curl Wig", zikaja picha na YTvideos, mwanamke nkaanza na Video.....huwezi kuamini!!!
Kumbe nilikuwa nakosea kuvaa Wig langu, sio kwamba lilikuwa linatisha bali nilikuwa nalivuta zaidi mbele kupita "hair line" so likawa linaonekana sio "natural" hivyo nikawa natisha! Haa watu kazini hata wasiniambie....the washenzi hihihihi.
Maskini mwanangu nilikuwa namtisha, yaani mtu ambae alipaswa kumlinda dhidi ya vitisho na hatari ndio____mbaya sana.
Anyway, siku hizi nalivaa Wigi langu inavyotakiwa pale ninapohisi sitaki kusumbua nywele zangu za asilia....well relaxed-asilia (haileti maana lakini umenielewa).
Kuna tofauti kati ya Ushamba na Ujinga, mimi kwenye Wig nilikuwa mjinga, sasa nimejua (najicheka hapa hatari).
Nikutakie mwanzo mwema wa mwisho wa Wiki.
Babai.
Mapendo tele kwako...
Comments