Skip to main content

Review Undugu wako...

Familia/koo nyingi huwa kuna mtu ambae karibu wote wanaMshuku....wanamuona hatari....kutokana na mambo yake Kiuchumi kuwa safi na kila anachosema basi ni "sheria" au hupewa "umuhimu" au "umakini" hata kama alichosema ni upuuzi!






Yaani watu kwenye Familia\Ukoo husika hawaishi kwenda kwa huyo mtu, watoto wake, Mke/Mume wake wote wanapewa attention tofauti na akina nyie Hohehahe.






Mtu huyu na Familia yake hufurahia yote hayo na huwa on the look out kuona nani anakuja speed ili kuwa kama yeye au kumpita Kiuchumi....basi akigundua atafanya kila alijualo kuzuia Ndugu (tumbo moja) au Jamaa(ndugu wa mbali wale wa kuunganisha mjomba, binamu etc) asifanikiwe.






Umewahi kumpa Ndugu yako wa hivyo idea ya Biashara au Mradi halafu akakukatisha tamaa kisha yeye anaifanya hiyo Biashara au ule mradi ambao alikuambia kuwa huwezi kufanikiwa ukiufanya, kwamba utapoteza pesa tu??.....hihihiihi sasa amka na review Undugu wenu!






Mtu huyu huwa hasaidii wenzake ambao ni masikini kuweza kujikomboa, siku zote atakupa senti ili uendelee kumuona Muhimu maishani mwako na hivyo kurudi kwake kuomba tena na tena.






Yaani anafurahia kukusaidia kidogo mara kwa mara....badala ya kukusaidia mara moja lakini msaada huo uwe ni wa muda mrefu.






Mf: kukupa Mtaji ili ukajiajiri kuliko kukulipia Ada ya shule na senti za Matumizi ya watoto, zikiisha urudie tena...hiyo ni furaha yake kwani unatendelea kumuona au kumchukulia kama Mkombozi wako hehehehehe!






Wahenga walisema "ukitaka msaidia mtu, usimpe Samaki....mpe Nyavu na umfunze kuvua ili awe anavua mwenyewe"!





Actually sio Wahenga waliosema(sijui aliesema), nilisoma huo Msemo Twita enzi zile....


Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao