Nimekumbuka 1996/97 Mauaji ya Mwembe Chai (siku mbuki vema na sitaki ku-google vilevile)!
Siku chache baada ya Mauaji yale bado kulikuwa na Maandamano ya Siri ya "Waislamu wenye Hasira".....Kile kifo cha yule Kijana pale Mwembe chai akianguka LIVE baada ya kupigwa Risasi na Polisi (FFU sijui) akiwa amevaa shati la Bluu Mpauko(light Blue) kamwe haitonitoka Kichwani! Ni kifo cha kwanza nilishuhudia live(on Tv)!!
Sasa bila kujua si tukaenda Kariakoo siku ya Ijumaa! Ile tumemaliza manunuzi si tukakutana na Waandamanaji na FFU...wakayaachia Mabomu ya "Machozi"....oh boy! Nilihisi Vita kuu ya Mwisho wa Dunia ambayo sina Uzoefu nayo ndio imefika!!!
Kimbia, huku na kule mara Tukakutana na jamaa (sijui Katibu au Mlinzi, ila alikuwa Mhindi) Wa SSC pale Msimbazi, akatufungulia Mlango kwenye Jengo la Simba....akawa anaita akina Mama na Watoto waende kupata Huduma ya kwanza....hihihihi kunawishwa Maji Usoni(wasn't a laughing matter then)!
Anyway! Baada ya hapo kukatulia, tukatolewa nje ya Jengo la SSC kwenda kupata Usafiri....kwenye Daladala! Tulikuwa tumepanda na baadhi ya Waandamanaji!
Akamuuliza Mzee mmoja na Kanzu yake...."Baba na wewe ulienda K'koo kuandamana".....Mzee akajibu "ndio mwanangu, tunapigania haki yetu"....Mdogo wangu akaulia "una watoto"...yule mzee akasema Sita na wote wapo Sekondari.
Mdogo wangu si akaanza Risala sasa? "Wee Mzee mzima badala ya kuhangaikia maisha ya wanao na kuboresha maisha yako, unaenda kupoteza muda kuandamana. Sasa kwa bahati mbaya umepigwa Risasi umekufa au Bomu umekatika Miguu nani atatimiza mahitaji ya wanao?"
Akaendelea "Wazee wengine hamfikirii, mnakuwa wabinafsi sana na Dini zenu, Pigania haki ya kupata vifaa Mashuleni, sio Dini"
Mie hapo nywiii(kimya) bado natetemeka huku nafikiria Mabomu ya Machozi yataniathiri vipi huko mbele, sikuwa na sauti wala nguvu....ujue mie ni Muoga mnoooooo linapokuja suala ya kuingiza mahewa, madawa, sumu mwilini mwangu!!
Ah! Mauaji yanayosababishwa na Dini hunisikitisha sana.
Mungu amrehemu yule Kaka alieuwawa pale Mwembe chai.
Heri ya Mwanzo wa Mwisho wa Wiki.
Bai.
Mapendo tele kwako...
Comments