Skip to main content

Misinformation za Online nazo.

Hellooooo!


Urahisi wa kuweka chochote online kwa nia ya ku-share au "kuelimisha" wengine ni mzuri sana!




Sote tunajua kuwa kwenye kila kitu kuna Faida na Hasara zake, kama Mwanadamu unatakiwa kupima na kufanya uamuzi kwa kuzingatia faida zaidi (utafaidika?).





Sio sote tuna-share yote(kila kitu) online....kwenye Blog ya D'hicious nimeshare mengi tu ila sio yote nijuayo (mengine naweka kwa ajili yangu mimi binafsi) na Binti yangu na Mwanae huko mbeleni Ntakapo kuwa Proper Bibi.






Hali kadhalika kwenye Blog nyingine Mf za Urembo, Fashion hufanya hivyo pia....tena hawa huwa hawabani some info, wanakudanganya kabsaaaaaa(wanapindisha ukweli) ili uogope au ukosee na hivyo usitokee as Mrembo kama wao wanavyoonekana au Nywele zako zisikue kama zao.






Safari yangu ya Nywele (nilishawahi kukuambia about) imenifanya nijaribu Mengi, kukosea Mengi na Kujifunza Mengi halafu nikarudi kwenye "rutini" yangu ya enzi ambayo kabla ya YouTube na Blogs za Nywele na Afya ya nywele zangu imekuwa njema.....(The new thing kuongeza Oils kwenye Conditioner).





Narudia tena, usichukue kila unachosoma online kama kilivyo, pima Faida na Hasara....kama ni Tiba(Madawa) au Afya ni vema kuangalia chanzo chenye uhakika Mf: site za Hospitali au Shirika la Afya, kwa huku nilipo NHS.com ina info nzuri sana kuhusu Magonjwa yote, yep Mpaka Ebola....sio Blogs ya mtu anaejiita Doctor(could be anybody).


Story time:Nilipoanza Kazi miaka ka' 20? Iliyopita....sikumbuki(tafanya hisabati baadae)....anyway! Niligundua kuwa ile Makala nzuri sana ya Urembo iliyokuwa inaendelea kwenye Gazeti Fulani na "mmiliki" alikuwa Mwanamke(kwa mujibu wa Picha na Jina).....kumbe MUANDISHI wake alikuwa Baba mtu mzima na hakuwa Mtanashati, alikuwa a bit rough(hajipendi)!






Sasa linapokuja suala la Afya yako au matumizi ya Madawa hakuna "Trial and Error" kama kwenye Urembo(utanawa) au Nywele(utazikata)



Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao