Za watoto wakati wa kuoga au kubadilisha.
Siku koja Mwanangu wa kwanza alipokuwa na miaka 3.....well bado ananiaka hiyo, aliuliza "mummy why baby doesnt have ______ like me?"......nkamwambia kwasababu ni binti, mabinti hawana_____(au unataka niseme kwa kiingereza...).
Kuanzia siku hiyo siwaogeshi pamoja wala kuwabadilisha nguo wakiwa chumba kimoja.
Je unadhani muda gani muafaka kutenganisha watoto Kijinsia linapokuja suala la kuokoa kuwabadilusha pamoja?.
Maswali anayouliza babuu kuhusu mwili wake ni magumu sana.....lakini yupo kwenye umri wa kujifunza so hatuna budi kujibu kiuwazi na sio kumkalipia au kumarufuku asiulize maswali kuhusu mwili wake.
Siku kauliza kwanini akikojoa Uume unakua....."mummy when i take pee my _____ grows.....but why?"
Siku nyingine (nilicheka mpaka nikaanguka chini) katoka mbio chooni eti " i went for a poo but then pee want to come so i stopped"......baba mtu akamwambia sometimes it happens so he shouldnt stop.....kwani alirudi chooni!
Akijaiona hii post hukoo baadae anaeza kunisuu kwa kumuaibisha.
Babai.
Comments
heri ya mwaka mpy a( ilochelewa)... maana sijapita avenue hii siku nyingi.
Nimecheka na hii post maana mwanangu mie wa kike. Saasa mwaka fulani alipotembelewa na binamu zake toka hukohuko uliko, akamuona binamu yake ( a year older than her by then , kumbe hadi sasa gap ni hiyo hiyo, issshhh but walikuwa wadogo kiasi by then), ana pee kwa kubenjulia kiuno kwa mbele as he was and still is a boy...
Naye si akaanza kung'ang'ania kubenjua ka..... kwa mbele anasema I want to weeeeeee just like S ... does...
na for like two months ilikuwa ni taabu kumwambia akae kwenye toilet seat for a peee.
Aliendelea ku maintain kuwa atasit wakati wa 'big F' tuuu which was her conventional name for a poo.
Wana wana mambo na ndo sehemu ya burudani ya uumbaji wa Mungu.
siku njema kwako na endelea kusukuma mpira mama ( kick the ball)