Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2015

Kula Fresh Vs Natural?

Hi.....kwa mara nyingine! Back in 2006 kulikuwa na mabishano kuhusu matumizi ya vitu ambavyo sio asili kwa matumizi ya Mwanadamu. Wengi wetu (tukisaidiwa na chunguzi mbalimbali) tuliamini kuwa matumizi ya vyakula vya Kopo, Madawa ya kutibu, aina za Sabuni, matumizi ya Microwaves n.k huenda ndio sababu ya magonjwa  Mengi yasiyotibika na kuu ni Saratani. Miaka ikapita na tukakugundua kuwa kutokana na Maendeleo ya Teknolojia kwenye kila kitu hakuna u-natural......kwamba hakuna mtu anakula kiasilia kwasababu mazao yote yanakuzwa na Mbolea ambayo ni "man made". Ukiachilia mbali Mbolea ni Maji tutumiayo kumwagilia mimea na madawa ya kuua wadudu wanaoshambulia Mazao.....Umepata idea ya wapi naelekea ambako sitaki kufika(sitaki post ndefu). Bado mabishano yapo au niseme yameamia kwenye utunzaji wa ngozi na Nywele. Watu wanajisifu kuwa wao ni Natural na hawataki Chemical(relaxer) kwenye miili yao lakini bado wanakunywa maji (bombani au chupani yote yanakemikali). Wanatumia Sabun

Sijafa-sijaumbika....

Si nikaumwa Tetekuwanga!!! Isije siku tunakutana ukaanza kunifokea/Suta kwanini nilisema nina ngozi nzuri wakati nimejawa na madoa ka Chui(as if unajali). So wacha nijihami mapemaa. Sikutegemea kuwa siku moja ningeugua Ugonjwa huu so nilipoanza kuumwa nkasema Mimba nini? Unajua....unapofanya Mapenzi nyama kwa nyama na Mumeo kitu cha kwanza kuangalia ni Mimba kila unapojisikia vibaya ili nisijetumia Madawa nakuua au kulemaza Kiumbe(sio kwamba naitaka hiyo Mimba). Ndio hivyo sasa nimeugua gonjwa la Kiwahili(sio kweli).....akati nakua kuna watu (Majirani zetu) walikuwa wanatukuza magonjwa ya Kudumu kama vile Moyo,Kisukari nakadhalika. Utasikia "sie hatuumwi magonjwa ya Kiswahili kama Tetekuwanga, Typhod, Kifua kikuu na mengine yote ya kuambukiza. Tunaumwa Magonjwa ya maana kama vile Kisukari, Saratani, BP" hihihihihi.....sijui ulikuwa utoto wao au ujinga wao? Sitoki nje bila kujipaka tope(foundation) kuficha Madoa Meusi usoni....naaa hakuna kujiamini hapa.....natisha hahah

Chanya....Wanaume na tofauti zao (SY2)!

Hai? Baada ya sehemu ya kwanza iliyofunikwa na Hasi (bado ninazo kibawo though)nimeona sio mbaya tukiangalia zile tofauti ambazo ni Chanya. Bila kupoteza muda twendeeee! Wanakufia kimahama mpaka hawajielewi lakini sio ki-Romeo....hawa jamaa hawajui kuweka wazi hisia zao wazi kwa kukuambia wanakupenda na kukunidi na kukumisi kila siku, na Kamwe hutowasikia wakisema "bila wewe maisha yangu ni bure". Utakuwa umeambiwa/umesoma mahali kuwa Mwanaume asipokuambia hivyo ujue hakupendi.....sio kweli! Pili, wanafurahi kuonekana kama Familia, yaani siku hizi zile "date night" sijui "outings" hazipo.....kila mkitoka basi na wanenu pembeni. Ukimkumbushia "sisi"anakuambia "watoto bado wadogo kwanini tuwe wa binafsi na kujitoa wenyewe?"(family man?). Tatu, Tangu mmefunga Ndoa hakaribishi rafiki zake ambao ni Single na ukaribu wake kwao unapungua. Sio kwamba anaogopa watakuiba bali anajihisi kuwa kwenye era nyingine ya Maisha yake. Nne, Mara ya m

Baba/Mama yao Mzungu.....?

Watu(Wazungu) wanapouliza kama Mumeo/Mkeo ni Mzungu kwasababu watoto ni weusi na sio WEUSIiiiiii tii, unafurahi? Unakwazika?  au unapata (mie)nafasi ya kutoa Elimu kuwa Weusi wetu Waafrika unatofautiana na kwanini? Nilikwisha wahi gusia kuwa kuna baadhi ya watu Shuleni kwa Babuu wanadhani Baba yake ni Mzungu......nikiwa na Kibibi ambae hana rangi ng'avu sana kama Kaka yake bado watu wanadhani Baba yake ni Mzungu. Halikadhalika watoto wakiwa na Asali wa Moyo (baba yao)bado wanauliza "is their mother white"? Inafikia mahali unachoka kutoa Elimu ya tofauti ya Weusi......jamaa wanadhani Waafrika wote tuna rangi moja kwamba wote ni Chocolate au Dark Chocolate. Ikitokea unakarangi ka Caramel au umepauka zaidi basi wewe ni mixed race(toa macho kwa mshangao)! Sasa hili ni Jepesi kwa Mimi mkimama wa Kitanzania(sikwaziki kirahisi).....ilimtokea Mkimama mmoja wa USA ayeeee alikasirika mpaka akaamua kwenda public(youtube).....Weusi wa USA wapo verevere demaged na Ubaguzi. Pamoj

Kiswahili kwenye Matangazo UKtv

Sema, mambo! Kiswahili kimekuwa Common sasa kama Kiinglish, yaani inakuwa taabu kuwateta watu(not that i teta watu....). Natumia Kiswahili zaidi kuficha ukali wa maneno pale wanangu wanapoleta ujinga. Mfano tupo mtaani na watoto halafu wakawa hawasikii....unawaambia "do you want to chapwa au am going to chapa you"......wanajibu "no dont chapa us" na kuacha ujinga hehehehe. Sasa ukisema neno kuchapa kwa Lugha yao bana utaitwa abuser na unaeza nyang'anywa watoto. To the nukta: Kuna Matangazo mawili ya Kiswahili moja la Holiday (lastminutes.com) na lingine la Bank linalomhusisha Mmasai(Co-operative Bank).....nenda kaguge. Siangalii Tv kihiiiivyo ila wanangu wamenishtua niliposikia wanaimba sijui 'ninini matako'.....nkauliza "where did you learn that word?"......nikaambiwa "its only an advert mum, dont be silly". Nka-rewind si nkakutana na Tangazo la holiday jamaa anaimba kwa Kiswahili pamoja na maneno mengine akatamka "matako&

Wanaume na tofauti zao....

Kuna wale wanaodhani kuwa na wewe ni "Feva" hivyo ushukuru Mungu. Aina hii huwa wanategemea uwafanyie kila kitu kuanzia kuwapikia mpaka kutafuta mbinu za kuendeleza "moto" kwenye ndoa yenu. Unafanya yote hayo na pengine zaidi.....yeye ana-chill tu. Yaani hata ukiumwa hakutengenezei Uji. Inafikia mahali unajiuliza "nafanya yote haya kwa ajili yake, yeye ananifanyia nini? Pili, Wanajifanya wanaujua Usawa kuliko Feminist (well wanaume pia wanaweza kuwa mafeministi as in wanasaidia kupigania Usawa kwa wote). Lakini sasa kwanini ni wewe tu ndio umnunulie Zawadi ghali na wewe kupata Kadi tu kutoka kwake kwenye ile siku yenu Maalum? Tatu, Wazee wa Mipango aka wazito.....huyu bwana ana plans lundo halafu nzuri zinazotekerezeka lakini utekerezaji Sufuri. Sasa si unipe mgao mie nikutekerezee? Mpaka nikuombe....Aiii! Nne, Wadaku.....kila stori ya Mjini anayo yeye....kila mwanajamii wa jamii yake ama anamjua au rafiki yake ni rafiki yake. Anashadadia(bado mnatumia hil

UK ya leo sio ile ya 1998-2006

Habari? Unajua enzi hizo kuishi Ulaya(ya UK) ilikuwa raha sana na tulikuwa na mahela ya kumwaga.....hata mie nilikuwa tajiri Mwanafunzi. Unakumbuka enzi zile tulipokuwa summer holiday(kipindi kama hiki) unagoma kurudi kwenu na badala yake unabaki Ulaya kupiga Kazi siku 7 za Wiki ili "kufuga" pesa? Wakati wa term mtu kutoka Bongo anakuomba senti.....unamwambia nipe wiki nitakurekebishia......unaenda chukua kazi kwa Wakala na unamaliza tatizo la mtu just like upepo. Fast foward mpaka 2008.....wa Ulaya Mashariki wakaanza kumiminika nankujaza kazi zote za Mawakala tena kwa malipo chee(wanachukua mpaka £3 kwa saa)......sasa mimi Muafrika na yule Mbritish (kiwango cha malipo ni tofauti na wa Ulaya Mashariki)! nikufanyie kazi lwa £3 sijipendi?? Siku hizi ni kama Bongo tu.....kama hujapata bonus kazini kwako basi utabaki na Mshahara ule ule......siku hizi hata zile overtime hazipatikani. Mkurugenzi anachukua extra hours hihihihihi. Sasa mtu akikuomba msaada na  ukamwambia....e

Chunga Ulimi usimuudhi Mpenzi....

Hello! Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Mambo tunayoambiwa tuyafanye kwenye Ndoa ili tuishi kwa Amani ni mengi mno na yanachukua "utambulisho" wetu......halafu vipi kuhusu Ndoa yenye furaha? Mambo kama "usilopokea....soma nyakati kwanza ili usimuudhi mwenza wako", hii inakufanya uwe mtu mwingine na sio wewe.....katika hali halisi ni task itakayokukosesha furaha kwasababu utakuwa unaishi kama mtu mwingine na sio wewe. Unasoma nyakati only kama issue unayotaka kuiwakilisha kwa mwenzio ni ya kubomoa au kujenga Ndoa yenu. Lakini mambo ya kawaida kama vile kutaniana na kuzungumzia watoto hayahitaji "kusoma nyakati". Kingine ni kusema unavyojisikia baada ya kuvumilia vya kutosha.....ujue wakati wote sisi ni wepesi kuona makosa  madogo madogo ya Wenza wetu kuliko kuona yetu(sio rahisi kuona makosa yako). Na ikitokea Mwenza sio mwepesi kukuambia pale unapokosea basi wewe unadhani kuwa ni kawaida tu na unasonga na maisha. Siku yakimfika shingoni anakuambia ras