Skip to main content

Dawa za Kuzuia Mimba.....Ukweli uliofichwa!


Haiyaaa! Kitambo eti?

Leo tuzungumzie Dawa za Kuzuia Mimba, pengine unajua Mengi kuhusu hili zaidi yangu kwa sababu mie sijawahi kuyatumiaga haya Makorokocho bana. Sababu kuu haikuwa kwamba niliogopa Saratani (zote zinaongeza Uwezekano wa kupata Cancer), au Kunenepa(inategemea na Mlo wako) au kukonda bali sikutaka kuwa "mchafu"......Napenda Ngono sana tu ila sina Mpango wa Kuolewa na Wewe wala kuzaa na Wewe sasa kwanini unikojolee(achie uchafu wako, wakati wangu unauosha in sekunde).





Mara nyingi huwa nakuwa Mkali ikiwa Binti(well mdogo wangu) ananijia na kuniomba ushauri wa kutumia Dawa za kuzuia Mimba wakati hana mpango wa kuolewa na huyo Bf wake.....nkauliza utakojolewa na wangapi in your life wajameni??!! Pia huwa naudhika ninaposikia Wanaume wanasema kuwa ni kazi ngumu sana kumalizia Nje na Condom inapunguza "utamu" na hivyo kuwasukuma/Lazimisha Wanawake kwenda na kutumia Vidonge/Sindano au kufanyiwa "upasuaji mdogo" ili kuwekewa ile "Y" aka Coil.




Madhara(side effects) za Dawa hizi(ondoa Condoms kwenye Pic hapo juu) zipo nyingi na zinazojulika ni zile ambazo ni za Kitibabu. Zile za kihisia huwa zinafichwa.....well wanasema unaweza kuwa Depressed  in which inaweza kufanya Uhusiano/Ndoa kuwa na matatizo sasa hilo sio ninalotaka kukuambia hapa.





Wanaume hawa hawa wanaowalazimisha Wanawake kwenda kuongeza Mahomono wasiyoyahitaji, huwa wanashangaa kwanini  Wake/Wapenzi wao hawawapendi/tamani tena, unakuta Mkimama anavutiwa na aina nyingine kabisa ya Wanaume na sio alie nae tena(anakuwa sio type yake)......mara zote utasikia "tangu Mke wangu kazaa, amebadilika sana, hanipendi tena".....well si ulikataa kutumia Condom na kumlazimisha atumie Dawa za Kuzuia Mimba.




Sasa kwa huku Ughaibuni kila Dawa unayopewa inaelezea faida na hasara zake(sio kupewa kama zawadi na Mhudumu wa Dula la Dawa Baridi), lakini badiliko ya Mwanamke kutompenda Mwenza wake anymore huwa hawaiweki wazi(nadhani kwa sababu za kibiashra), lakini inasemekana kuwa, Mmwanamke anaeanza kutumia Dawa za Kuzuia Mimba baada ya kukutana na Mwenza wake(mwanaume) hubadilika na kutokumpenda tena mwanaume huyo.





Na wale ambao wanapenda Wanaume wakati tayari wanatumia Dawa za Kuzuia Mimba hubadilika na kuwachukia/kutowapenda waume zao pale wanapoacha kutumia Dawa hizo......ndio maana wakimama wakishika Mimba huwa na Mahasira  kwa waume wao eeeh? Homono...homono....HOMONOO!




Stori Time: Kuna mjamaa na Mkewe, wamependana kwa Miaka kibao na kujaaliwa watoto kadhaa. Life happened(matatizo) wakatengana sio kwa hiyari bali kwa sababu za "kisheria", jamaa Kaswekwa kwa Miaka 2 na hawakupewa ile "haki" ya kupata Ngono mara moja kwa Mwezi so Mkimama(mkewe) akaona aiii ya nini kuendelea kutumia Midawa ya kuzuia Mimba wakati Mtiaji Mimba yupo Jela, Mkimama aka-withdraw.




Mara akaacha kwenda kumtembelea Mumewe Jela, akienda ni kwasababu watoto wamelazimisha. Mkimama akaanza Kupendezwa na "type" nyingine ya Wanaume.....unaijua ile hisia ya "nimevaba na nimepoteza Muda wangu  na nimekuwa used na limtu ambalo hata sio type yangu" ile....yeah? kama vile unakutana na Ex  halafu huamini kama ulilala nae na kujiuliza hivi nilikuwa nimelewa au? yaani huyu ndip angekuwa mke/mume/  Mama/Baba wa wangu YAACK!! au ni mimi tu?! hihihihihihi.





Basi Baada ya Miaka yake Mitatu (Miezi 18) jamaa huyu hapa, Mkewa walaaa hana habari. Mumewe anaanza kushangaa kulikoni Mke wake anatereza nje nini? hakukuwa na Ushahidi wala nini. Mke msafi, alikuwa nasubiri Mumewe atoke ndio aombe Talaka maana tangu kaacha kutumia Dawa za Kuzia Mimba amejikuta hampendi wala kumtamani Mumewe tena.




Jamaa akaanza kulia, hajui ataishi vipi bila Mkewe.....watoto wanabembeleza Mama aendelee kubaki na Baba yao, lakini Mama anasema hawezi kwa sababu Baba yao sio Mtu ambae anampenda au angempenda kama asingekuwa "chini" ya Madawa ya Kuzia Mimba.....amevaba!!


Hii haina Mikutano ya Familia, wala Saikolojisti wala Kansela wa Mmahusiano na Ndoa Kanisani kwenu.....Kuvaba hakuna Dawa wala Therapy na Yesu hausiki. Ziiiii Endi.


Naheshimu na kuthamini Muda wako, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao