Skip to main content

Eating Clean: Kifungua Kinywa kwa busy mums

Kama wewe ni busy Mum wa watoto wawili chini ya Miaka Mitano bila Msaidizi kama mimi,  hakika utakuwa unatafuta Kifungua kinywa kitakachokaa tumboni muda mrefu. 



Chakula kitakachokuchukua kuanzia saa Moja asubuhi mpaka saa Kumi na Moja Jioni(au muda wako unaokula Chakula cha jioni/usiku). Hapo katikati unaweza kutafuna chochote na kunywa maji (ya kutosha) ili kujiongezea nguvu na kukata Kiu ila hutopata hisia ya kutaka kula chakila kizito.



Baada ya kujifungua mtoto wa pili nilikuwa nakula Lunch asubuhi na nilifanikiwa kupunguza Mwili wa "Mimba".....then nikagundua Mayai na Kale(mboga jamii ya Kabeji).



Nadhani ni kama Spinach(sio Mchicha kama Wanavyoita wa UK na US), unazijua zile Spinachi tulikuwa tunapanda kwenye Bustani za Shuleni(kama ulisoma Shule za Msondo aka non Academy? Radha yake na Muonekano wake ni tofauti lakini nahisi kuwa ni Jamii hiyo.



Kwa kawaida nakula Mayai 3(kiafya unajitaji 2 kwa siku)....huwa nachanganya na Kale  kisha naweka kwenye Microwave kwa dk 3. Halafu nanyunyizia chumvi na pilipili Manga. Nakula na tunda Moja.



Huwa nabadilisha matunda kati ya Apple na Ndizi Mbivu au Embe Mbivu. Siku nyingine nabadilisha "upishi"......badala ya kuMicrowave huwa nakaanga kwa kiasi kiduvhu cha Olive oil na kisha naongeza Jibini kwa juu(kabla Yai halijapoa).....kama picha inavyoonyesha.



Mwili wako unahitaji Protein kama mwanamke kwa ajili yakujenga Misuli(kama unazoezika) na Kale ina Vitamins na Mineral muhimu na inasaidia Nywele na kucha zako kuwa na afya njema na kukua haraka kuliko kawaida yake.


Mabadiliko ya mwanamke baada ya kuzaa ni mengi higyo ni vema kuwa muangalifu na unachokiweka au kukiondoa mwilini. Mlo huu haukinai (mwaka wa pili na nusu nakula hivyo kila Asubuhi) na haunenepeshi so long unakula mlo huu mara moja Kwa siku. Na usile mlo mwingine uliopikwa kwa kutumia Mayai.

Naheshumu na kuthamini muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao