Skip to main content

Posts

Showing posts with the label AliKiba

Amina wa Ali Kiba adai Talaka Mahakamani na Kiba(2)....

Soma Mosi na Pili hapa .... Tatu, Mtoto anamuhitaji Mama yake full time kwa Miaka 5 ya mwanzo ya Maisha yake baada ya hapo PT sio mbaya. Malezi ni Kazi  kama kazi nyingine na inachosha Akili na Mwili, tofauti ni kwamba hakuna Likizo na huwezi kuacha/badilisha na pia kwa  Tz Mke (Mama wa Mtoto) huwa halipwi na hiyo inafanya kuwa "Kazi" hiyo kuonekana kuwa ni rahisi. Mkeo anapoamua au mnapokubaliana kuwa yeye abaki Nyumbani kulea watoto ni jambo zuri na la kuheshimika kwa Ulimwengu wa sasa. Mkeo akigoma kufanya Kazi ya Kulea na kuamua kwenda kufanya kazi/biashara nje ya nyumbani ni wazi kuwa mtahitaji "Mlezi" wa watoto wenu wa hapo nyumbani na yule wa "shule", na atalipwa kwa "rate" nzuri tu kulingana na Kipato/aina ya Maisha mnayoendesha. Wengi kwenye Mitandao wamelichukulia suala la Amina na Kiba kwa kuangalia Kona ya maisha waliyonayo wao kwa sasa, na sio Maisha ya Star Mkubwa mwenye Thamani ya Dollar  Millioni 5(11,570,000,000). Pi

Talaka ya Amina kwa Ali Kiba...

Mimi na wewe hatujui kwa Undani ni kitu gani hasa kilichopelekea wawili hao kufunga Ndoa 2018. Lakini kutokana na Maelezo ya Amina kwenye Hati ya Madai tunajua kuwa Kiba alikuwa Mtesi/Mnyanyasaji kwa Mkewe (Kiakili, Kimwili, na Kisaikolojia)baada ya Miezi 6 ya Ndoa. Kwa maelezo hayo inaonyesha kuwa Amina hakuwa "kipenzi" cha Familia ya Mumewe na hivyo kuhisi kuwa mahali walipo watu hao sio Salama kwake na kwa Watoto na hivyo kurudi kwao Mombasa*. Pia Amina ameongeza kuwa Mumewe(Kiba)ni Muasherati na hakuiheshimu yeye(Amina) wala Ndoa yao(alimdhalili adharani). Amina amedai kiasi cha Laki mbili kwa mwezi(Ksh) kwa ajili ya Matunzo yake na watoto. Madai ambayo yamesababisha Watanzania wa Twita kuhoji... Tu(na)jigunza nini kwenye tukio hilo. Moja, Kwa Msanii mkubwa kama Ali Kiba ambae ana Thamani ya Dollar Millioni 5(568,500,000Ksh) Laki mbili kwa mwezi kwa mahitaji ya Mtoto sio pesa nyingi, pengine haitoshi tukiongeza Ulinzi, Usafiri na Bima ya Afya.  Unalipa Matunzo

Rudisha Heshima ya Ndoa: Mfanye Mkeo ajihisi Malkia...

...Mengi ni yaleyale yanajirudia.....kukumbushana sio mbaya, kwavile tunatofautiana ni wazi kuwa Mkeo atakuwa  na vijimambo vyake ambavyo anapenda kufanyiwa ili kujihisi kuwa yeye ni "Malkia". Umalkia ninao uzungumzia hapa sio ule wa kuishi kwenye Jumba kubwa zuri lililojaa watumishi au kumfanya Mumeo kuwa Mtumwa kwako....la asha! Habari gani? Kwa kawaida Wanawake(wake) huwa na tabia ya kujitahidi kuwa Wake wema, tunafanya mengi sana kwenye Ndoa(au Uhusiano) na Familia(kama mmebarikiwa Watoto) wakati mwingine kama sio mara zote huwa tunasahau kuwa nasi pia tunahitaji kujisikia kama ambavyo tunawafanya Waume zetu kujihisi Wafalme. Soma Jinsi ya kumfanya Mumeo ajihisi Mfalme  kama uliikosa. Kama kawaida kwenye haya mambo hakuna Kanuni hivyo jaribu haya kama hujawahi na hakikisha unamsoma Mkeo vizuri ili kujua ni kitu gani hasa anahitaji kutoka kwako kama Mumewe. -Pamoja na kuwa anapesa zake, mgawie kiasi cha Pesa  zako bila sababu.....weka mahali ambapo ataziona kwa

Mwenza Mshindani/Mpinzani...utamjuaje?

Kuna baadhi ya watu wameumbwa/zaliwa kuwa Washindani na hivyo kwao ni kawaida(pia ni vizuri), mara nyingi huliweka hili wazi mwanzoni kabisa mwa Uhusiano. Wakati mwingine wewe mwenyewe unaweza tu kugundua kuwa Mpenzi wako ni Mshindani kwenye shughuli zake za Kibiashara/Kazi, Masomo, Utunzaji wa Pesa, namna anakutunza n.k. Lakini hutofikiria hata siku moja kuwa mkifunga Ndoa hatokubali wewe "umshinde" kwenye jambo lolote. Ukiachilia mbali mtu kuzaliwa hivyo(mshindani) pia Ushindani unaweza kusababishwa na Mazingira, Uzoefu au Malezi. Kwa wale ambao wamezaliwa wachache au wengi (Mtoto wa  Pili, Mtoto wa 3 au 5 kati ya watoto 8-10) au yule wa Pili kutoka Mwisho kati ya watoto zaidi ya 5(hii ni Uzoefu wangu binafsi mie sio Mtaalam). Pengine unaweza usigundue mpaka mtakapokuwa na Watoto, ambao huibia mambo mengi sana kati ya Wewe na Mwenza wako. Kumbuka Watoto huwarudisha nyote wawili kule mlikotokea(utotoni) na hivyo  kutaka kulea wanao kama ulivyolelewa wewe

Nakupa mapenzi alionipa Mama....

Unless hujui Elimu ya Viumbe Hai hasa kuhusu Mwanadamu utabisha na pengine kuwa offended. Unaeza kudhani kuwa Ali Kiba amemkosea adabu Mama yake na pengine ulajiiliza utampaje mpenzi wako Mapenzi aliyokupa mama obviously hayato tosh......halafu ukawaza ni mapenzi gani hasa mwenzetu alipewa eeeh! Well uhusiano wa kwanza wa mtouo yeyote ni ule wa yeye na Wazazi wake.....mtoto hajui kupenda mtu yeyote zaidi ya wazazi wake hivyo lolote analopata kuyoka kwa wazazi hao ni mapenzi. Linapokuja penzi la mama kwa mtoto wale wa Kiume au Baba kwa Binti yake kidogo kuna mkanganyiko na wengi hushindwa kuelewa lakini kama nilivyosema ikiwa kama unalijua vema Somo la Viumbe Hai baada ya High school(ambayo mie sikuipata hii ni another sitori ya siku ingine) utaelewa. Vitendo vya kimapenzi au upendo ambavyo Mama alitupatia baada ya Kuzaliwa na kipindi tunakua ndivyo ambavyo tunavifanya au tunapenda kufanyiwa na Wapenzi wetu tukiwa watu wazima kwa......mf kunyonyana Chuchu, kukumbatiana, kupeana mab