Skip to main content

Rudisha Heshima ya Ndoa: Mfanye Mkeo ajihisi Malkia...


...Mengi ni yaleyale yanajirudia.....kukumbushana sio mbaya, kwavile tunatofautiana ni wazi kuwa Mkeo atakuwa  na vijimambo vyake ambavyo anapenda kufanyiwa ili kujihisi kuwa yeye ni "Malkia". Umalkia ninao uzungumzia hapa sio ule wa kuishi kwenye Jumba kubwa zuri lililojaa watumishi au kumfanya Mumeo kuwa Mtumwa kwako....la asha! Habari gani?


Kwa kawaida Wanawake(wake) huwa na tabia ya kujitahidi kuwa Wake wema, tunafanya mengi sana kwenye Ndoa(au Uhusiano) na Familia(kama mmebarikiwa Watoto) wakati mwingine kama sio mara zote huwa tunasahau kuwa nasi pia tunahitaji kujisikia kama ambavyo tunawafanya Waume zetu kujihisi Wafalme.


Soma Jinsi ya kumfanya Mumeo ajihisi Mfalme kama uliikosa.


Kama kawaida kwenye haya mambo hakuna Kanuni hivyo jaribu haya kama hujawahi na hakikisha unamsoma Mkeo vizuri ili kujua ni kitu gani hasa anahitaji kutoka kwako kama Mumewe.

-Pamoja na kuwa anapesa zake, mgawie kiasi cha Pesa  zako bila sababu.....weka mahali ambapo ataziona kwa urahisi lakini atakuwa "suprised" na andika "hizi zako, tumia utakavyo", kwa Mfano. Badili ujumbe kila mara unapofanya hivyo.


-Onyesha/toa Shukurani kwa  kazi yake ngumu ya kutoa Malezi mazuri anayowapa watoto, hasa pale unapoona Watoto wanajiamini lakini wana Nidhamu(kuna tofauti kati ya kujiamini na kuwa mtovu wa Nidhamu), kama ni Mama wa Nyumbani. Kumbuka Malezi ni jukumu lenu w ote kama Wazazi lakini kwa Kawaida Mama huchangia zaidi ya Baba, hasa kama Mama huyo ni wa nyumbani.

-Onyesha(onesha) unajali anapokaribia na anapokuwa Hedhini, jifunze namna ya kumpa support, kipindi hiki huwa kigumu kwa baadhi ya Wanawake kama ambavyo ma-teenager huwa japokuwa ni kwa muda mfupi.

-Sifia Mapishi yake na sema Ahsante kila anapokuandalia chakula.

-Usishindane au kulinganisha  "attention" anayotoa Mama kwa  Mtoto/Watoto wenu, wewe ni mtu Mzima unaweza kujihudumia. Watoto bado wanajifunza na wanahitaji "attention" zaidi yako. Mkeo sio Mama yako bali  Mpenzi wako ambae pia ni Mama wa Watoto wenu. Usisahau.

-Mpeleke Manunuzi(Madukani) kila baada ya Muda fulani....sio kwenda kununua Chakula bali mahitaji yake binafsi kama vile Vipodozi, Manukato. Pads n.k,

-Anapokuambia  jambo "serious" hata kama sio hivyo kwako. Msikilize mpaka Mwisho ndio uulize swali, usiulize maswali katikati kabla hajamaliza anachokuambia. au Jitahidi kumsimamisha kwanza alafu ndio uulize....usiulize kwa kuingilia. hii itakusaidi kumuelewa zaidi.

-Jifunze Mzunguuko wake wa Ngono ambao unaenda sambamba na wa Hedhi...zile siku ambazo anakaribia ndio muda Mzuri  wa wewe "kulianzisha" na pengine kutotumia Kinga, baada ya Hedhi Mkeo atakuwa anatamani kupita kisi na ndio muda anafurahia/taka zaidi...kipindi hiki Mwili wake ubakuwa tayati kumimbwa hivyo tumieni Kinga kama hamtaki Mtoto....baada ya Siku  ya 14-16 (inategemea na urefu wa Mzunguuko)tangu Hedhi kuanza Mkeo hupoteza hali ya kutaka Tendo, sio kwamba hatamani bali anahitaji "msaada" ili kutaka Tendo hivyo ongeza ujuzi kwenye kumuandaa ili kumsaidia kufurahia Tendo atakapokuwa tayari.

-Onyesha au sema adharani kuwa yeye ndio Boss....mf; Dukani, mmenda kununua Kapeti au Gari, pamoja na kuwa Muuzaji anasisitiza ununue na unajua umelipenda lakini Mkeo anaonyesha kusita, mwambie Muuzaji "huyu ndio Boss wangu, Uamuzi wake ni wa Mwisho".

au Mmekutana na "Rafiki" yako ambae hamjakutana kwa  muda mrefu, rafiki anakuomba mkutane Pub, wewe hukupanga kwenda huko siku hiyo, unamrushia Mpira Mkeo..."Mpenzi ulisema baada ya hapa unataka kwenda wapi?".....mkeo atasema atakako hata kama hakuwa na mpango huo, atajua kuwa hutaki kwenda Pub na huyo Mtu.

-Muachie afanye maamuzi kwenye mabadiliko ya Nyumba(ndani), Mambo ya kununua Pazia, Sahani, Sufuria na Mashuka haikuhusu.

-Punguza ukaribu au poteza marafiki wote wa Kike, hata kama ni Dada zako(just saying, females are snakes, I don't even trust myself kama Wifi/Rafiki kwa Wanaume hihihihi).

-Msabahi na Muage kwa Busu na/au Kumbato.....usisahau kumpigia  Simu kumjulia hali unapokuwa mbali na Nyumbani.

-Mueleze(wasiliana) kwa uwazi kuhusu Hofu zako, Shida zako....misukosuko ya Kikazi/Biashara. Hakuna mambo ya "kiume nakabiliana nayo mwenyewe"huyo ni Mkeo ni ubavu wako, mshiriki wako, Mshauri na mtu pekee anaekujua kiundani kuliko hata Wazazi wako...anaweza kukusikiliza na pengine kukusaidia kuondokana na baadhi ya "mambo ya Kiume".

-Usimkosoe/Fokea kabla hujaua sababu ya yeye kufanya alichokifanya au kilichopelekea Mtoto kuumia ambapo wewe unadhani ni Kosa, jifunze kuwasiliana bila kumfanya Mkeo ajisikie vibaya.


Nisikuchoshe si eti?

Una swali? shoot at me on dinahicious@gmail.com. Kumbuka nitakujibu  hapa kwa faida ya wengine wenye swali kama lako na sio kwa Email. Shukurani kwa kuichagua Blog hii, tambua kuwa nathamini na kujali Muda wako hapa.


Bai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao