Skip to main content

Sababu nyingine kwanini tunawachukia Mawifi....

....(Dada wa Wenza wetu) wa sasa au waliopita(Ex), hasa kama mlizaa kabla hamjakutana au  kabla ya kuachana. Kama uliikosa ile ya mwanzo isome hapa. Hello, ipo jambo?

Madada huwa na viherehere bin vimbelembele vya kutaka kujua kila kitu, hasa Uhusiano ukiwa bado Mpya tangu kuanza/kuisha. wanaweza kujifanya wapo karibu na wewe na wanakupa support, wanakujua na kukupoenda blablabla.


Mawifi hao hao bado ni Shangazi wa Watoto wenu na ni Kaka wa Ex/Current Mumeo,  kwa maana hiyo bado watakuwa karibu na yeyote atakae kuwa na Kaka yao. Hivyo basi kuambiwa/shuhudia mambo mengi/kupewa ripoti kuhusu Mjaza nafasi(mke/Mpenzi mpya) na watoto wake na wakati huohuo wapo karibu na wewe Ex na Watoto wako.


Sasa kama wewe ni Ex au Current one mwenye utimamu hakika utaanza kujiweka  mbali na Mawifi kwa sababu chache zifuatazo:-

-Hawachelewi kukulaumu kuwa umembadilisha Kaka yao.

-Watakuwa wanazungumza na Kaka yao kuhusu Wifi yao wa Sasa na watoto wake na kamwe hawatokuambia(kama wewe ni Ex).

-Watakuwa wanajua kila kitu kuhusu Ex wa Mumeo na watoto wao bila wewe kujua...hasa kama sio muumini wa Blended family(ikiwa wewe ni Current).

-Wanapenda kujimilikisha Watoto wako na kukutenga wewe Mama yao(kama wewe ni Ex).

-Wanaibua Drama bila sababu ya Msingi(wote).

Nini cha kufanya ili kuepuka hayo na mengine uyajuayo:

Pamoja na kuwa Kijamii  Familia Mbili huwa Moja, kwamba mnapofunga Ndoa (au kuwa kwenye Uhusiano wa  muda mrefu) haina maana kuwa hao ni kweli Ndugu zako. Hata siku Moja usijifanye wewe ni Ndugu moja na Ndugu wa Mumeo(kabla hajawa Ex), hata kama wanakupenda kama Peremende.

-Hakikisha Familia yako hajiweki karibu nao
-Waheshimu kama wanavyo kushehimu au kama Dada wa Mumeo, kumbuka Upendo haulazimishwi kama hamja-click  usijipendekeze.

-Kama ni watu wa Drama, wachukulie kama walivyo(a.k.a dharau) na punguza mawasiliano. Kumbuka Wifi hawezi kuwa rafiki hivyo usijiachie sana hata wakiomba radhi.

-Weka mipaka linapokuja suala la Malezi ya watoto wako, ikitokea wameenda  kutembea kwao, wasipofuata matakwa yako, wapige Stop kuchukua wanao(wapwa zao).

-Usiogope kusema Hapana/Sitaki.

Una swali? au Nyongeza?....shoot/share nami dinahicious@gmail.com
Nitaweka hapa kwa faida ya wengine. Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Bai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao