Skip to main content

Mwenza Mshindani/Mpinzani...utamjuaje?



Kuna baadhi ya watu wameumbwa/zaliwa kuwa Washindani na hivyo kwao ni kawaida(pia ni vizuri), mara nyingi huliweka hili wazi mwanzoni kabisa mwa Uhusiano. Wakati mwingine wewe mwenyewe unaweza tu kugundua kuwa Mpenzi wako ni Mshindani kwenye shughuli zake za Kibiashara/Kazi, Masomo, Utunzaji wa Pesa, namna anakutunza n.k. Lakini hutofikiria hata siku moja kuwa mkifunga Ndoa hatokubali wewe "umshinde" kwenye jambo lolote.



Ukiachilia mbali mtu kuzaliwa hivyo(mshindani) pia Ushindani unaweza kusababishwa na Mazingira, Uzoefu au Malezi. Kwa wale ambao wamezaliwa wachache au wengi (Mtoto wa  Pili, Mtoto wa 3 au 5 kati ya watoto 8-10) au yule wa Pili kutoka Mwisho kati ya watoto zaidi ya 5(hii ni Uzoefu wangu binafsi mie sio Mtaalam).



Pengine unaweza usigundue mpaka mtakapokuwa na Watoto, ambao huibia mambo mengi sana kati ya Wewe na Mwenza wako. Kumbuka Watoto huwarudisha nyote wawili kule mlikotokea(utotoni) na hivyo  kutaka kulea wanao kama ulivyolelewa wewe au tofauti na ulivyolelewa ili kuepuka Uzoefu Hasi ulionao Ukubwani....na hapa ndipo "Ushindani"  huibuka. 

 
Sasa utajuaje kama Mume/Mkeowako anakuchukulia wewe  kama Mpinzani/Mshindani wake badala ya Mwenza wake?

1-Ukimnunuliza Zawadi nzuri na Ghali, basi yeye atakununulia Ghali zaidi(Wanawake huwa tunafanya makusudi ili kupata the most expensive....au ni Mimi tu?)


2-Anakukosoa kwanza kabla/balada ya kuuliza kwanini umeamua kufanya jambo fulani. Bila shaka kama Wenza mnashirikiana kwenye kila jammbo lakini kumbuka kuna Mambo mengine hutokea ghafla na hivyo kuhitaji maamuzi ya haraka na hapo kwa hapo, huwezi kumngojea Mwenza aje/apokee/rudishe Simu.


3-Anatumia Maneno ya Umoja zaidi "Mimi", "Niki", "Mwanangu"  n.k....nitakupa Mifano:-
Anapowaonya Watoto..."Mimi Mzazi wako sipendi tabia mbaya badala ya Sisi Wazazi wako hatupendi tabia Mbaya".


"Hii Summer nikienda Likizo na sio Tukienda likizo. Nikimalizia ile Nyumba badala ya Tukimalizia ile Nyumba".

Mkizozana/pishana kuhusu kuadabisha Watoto hasa kama yeye ni Mfokeaji (kwamna anafoka tu hata kwa kosa la Mtoto ambalo linahitaji muongozo wake kama Mzazi)...."huyu ni Mwanangu nitamlea nitakavyo".


4-Ukikosa Nafasi fulani ya Juu Kikazi au Kielimu....haonyeshi kujali sana(anakuwa kama vile kafurahia bila kuonyesha, lakini kwa sababu ni Mwenza wako hakika utajua tu kuwa hajaumia kama ulivyoumia wewe.


5-Akigundua unafanya Jambo fulani vizuri basi hatokusaidia kamwe! ukiomba msaada atakuambia "sipendi kuingilia mambo yako" hihihihi ukweli ni kuwa hataki kufeli halafu wewe ufaulu.


6-Ukija na Wazo zuri la Kimaendeleo ama anakukatisha tamaa  na baadae yeye Kulifanya au anakwambia umwachie yeye afanye Uchunguzi  kwanza....hutopata majibu ya Uchunguzi kuhusu wazo lako bali atakupa Wazo lingine linalofanana na lako.


7-Kwenye Kufanya Mapenzi....unajijua upo Vizuri, lakini hata siku moja hatokusifia. Ila ukimsifia yeye anafurahia huyo halafu hakuambii kuwa kakufanyia hivyo kwa ajili yako....anasema "najua". Nikupe Mfano? napenda Mifano....:-

Sio kila siku unamfanya/mnafanyana vizuri, ila kuna zile siku  unajisikia  upo "Juu" na unataka kuwa "extra" unamuamulia na unauhakika kabisa kafurahia kutokana na Matokeo during na after Tendo....lakini hatokusifia ng'ooo! Ila yeye akikuamulia siku hiyo unampa sifa zake, anakujibu "i know am good" hehehehe. How rude!!



Tangu nimemalizia na mambo ya Kufanya Mapenzi basi unaonaje Post ijayo tuangalie namna ya kubana/Kaza Misuli ya  Uke mara baada ya Kufanya Mapenzi Usiku tayari kwa ajili ya cha Asubuhi/Alfajiri. Sie tulio kwenye Ndoa ambao huwa hatuogi baada ya Tendo(kutunza Utamu eee)....si unajua Manii ikikaa Ukeni, Uke unakuwa "over relaxed" au tuseme "over expand(tanuka/panuka)? au hujui?...Usikose basi(Wanawake tu).

Ahsante kwa kuichagua Blog hii, nathamini na kuheshimu muda wako Hapa!

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao