Skip to main content

Imani ya Dini ni Msingi mzuri kulea watoto....

 

Pamoja na kusema hivyo haina maana kuwa Dini ndio kimbilio kwasababu ukizidisha huko Dinini pia unaweza kuongeza viungo kwenye matatizo yako ya akili au kuongezea mengine. Unapokuwa unafuata Imani ya Dini (Traditional Churches na Uislamu, hao matawi ya ukristo wa kisasa aka MATAPELI mie siwatambui) inakusaidia kuishi kwa heshima na kufuata princimples zake, unajua nini chakufanya(unamkimbilia Mungu) unapopata matatizo  mfano kupoteza kazi, migogoro kwenye urafiki, wazazi, ndoa, ndugu au hata pale unapoyumba kiimani.

 

Sio tu kwamba unakuwa na kimbilio (Mungu) bali pia unakuwa na Community kutokana na Asilia yako(Kabila) ambayo kwa kiasi kikubwa mnakuwa mnajadili masuala mbali mbali ya kimaisha na mnakuwa na activities hata kama ni mara moja kwa Mwaka, mnakuwa karibu kwavile mnamisingi inayofanana, mnaiheshimu na hivyo inakuwa rahisi kuepuka “Drama” ambazo ni chachu ya matatizo ya Akili.

 

 Kutokana na muibuko wa social media, kumekuwa na watu wakipeana mioyo au kufundishana namna ya kujitenga na kuwa wabinafsi which ni nzuri sana kama umezunguukwa na watu wakorofi ambao kutwa wanakusababishia matatizo na kukuondolea amani, ila kama huna Imani ya Dini na Ukabila (kwa kiasi Fulani) ni wazi kuwa huna “community” na matokeo yake unaweza kuwa mpweke kupita kiasi na matokeo yake kupata matatizo ya Akili. Online community itakufanya ujisikie vema na ukajiona mtu fulani muhimu lakini its is not real, uki-log out utabaki peke yako na upweke wako. Labda kama una Mke/Mume mwema na watoto.

 

Kama unaishi nyumbani(Tanzania) huenda usihisi upweke na hata kuhitaji sense of community kwasababu tayari upo karibu na ndugu na jamaa, kama sio wa Damu kuna wale wa Kikabila ambao mna-share values zilezile kwasababu.

 

Miezi kadhaa nilikuwa kwenye Semina kuhusu Matitizo ya Akili, waandaaji wakawa wanauliza ni vitu gani vinasababisha matatizo ya Akili? Watu mbali mbali wakawa wanajibu,kuwa ni Mazingira, Urithi, Unyanyaswaji kiakili, kihisia na kimwili katka umri mdogo, Matukio Hasi ya kimaisha (Vifo na Uzazi) kupoteza kazi/Ndoa na Umasikini.

 

Waliposema umasikini, nikashtuka na kama kawaida yangu nikabisha kuwa Umasikini  peke yake hausababishi matatizo ya Akili isipokuwa ukosefu wa Imani ya Dini na Community, nikaambiwa nielezee how? Nikawaambia nilipozaliwa (Tanzania) na kupata elimu yangu ya awali, kuna masikini mkuu  na wengi hawasumbuliwi na matitizo ya Akili kama watu wa nchi hii ambao katika hali halisi sio masikini in comparison. Watu wa Nchi za Magharibi wameacha kumuamini Mungu(hawana principles wala values) na wanalea Watoto wao kiholela bila Misingi, Mipaka wala Values za kufuata/simamia.

 

                                                        Nyumba za Masikini  wa Ulaya ya nilipo.


Ukiangalia Tiba ya Matatizo mbalimbali ya akili moja wapo ni kujiunga na Vikundi vya watu ambao wanamatatizo kama  yako, hii haina tofauti na nilichosema hapo juu kuhusu umuhimu wa kuwa na “sense of community” iwe Dini au Kabila au vyote(ila usipitilize).

 

 Siku hizi watoto wanakua tu kama Miti Michakani huku wakiamini kuwa wao kama wao wanauwezo wa kufanya chochote watakacho na hata kuvuka mipaka bila kujua wameivuka na hawajui wapi pa kukimbilia Zaidi ya Wanadamu wenzao(Madaktari na wataalamu wengine wa matatizo ya Akili) ili kupata msaada wa kiimani. Mtoto wa miaka 8 anakua akitegemea madawa kurekebisha ubongo wake(dawa za anxiety au za kuzuia mimba zote zina athiri Ubongo), huyu mwanadamu akifika miaka 20 atakuwa hajijui kwasababu kwa miaka 12 artificial brain chemicals zimekuwa zikirekebisha natural brain chemicals alizozaliwa nazo. Siku akichoka kutumia dawa ili awe kama rafiki zake ambao hawatumii midawa daily…anakuwa mwehu na kusababisha madhara kwa wengine!

 

 

Natambua kuwa watu nchi za Afrika wana matatizo ya akili lakini sio kwa kiasi kukubwa sana kama huku nilipo hasa kwa watoto, Watoto wengine wanahitaji Upendo, wanahitaji wazazi wao karibu na attention na sio Anti-depressant au anti-Anxiety. Lakini kwasababu siku hizi wazazi  wote mpo busy Kazini na wengine mkaamua kuwa single parent by choice, muda wako kama mzazi kutoa attention/kulea na kupenda kwa vitendo mtoto/Kijana/Binti unakuwa haupatikani kirahisi. Hii ina madhara makubwa sana kwa Mtoto ambae anakua na baadae kuwa mtumzima mwenye matatizo ya Aikili.

 

Siungi mkono watu waendelee kuishi kimasikini, nilichojaribu kusema ni kuwa Umasikini pekee sio sababu ya kuwa na matatizo ya Akili, ukizingatia Masikini wa Nchi hii ni Mwananchi wa kipato cha kati Tanzania…Hata hivyo, nikutakie siku njema.

 Bai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao