Imepotelea wapi? Au ndio kwenda na Wakati?
Juzi kati nimekutana na Picha ya Maiti ya Mpendwa wangu....pamoja na familia kufanya kazi ya ziada kuzuia upigaji Picha wa shughuli nzima ya Mazishi achilia mbali Mwili wa Marehemu wa mpendwa wetu zaidi ya alieajiriwa kwa ajili ya kazi hiyo....bado kuna jitu likapiga picha na ku-share online.
Kwasababu hana Uhai tena haina maana kapoteza Haki zake kama Mwanadamu mpaka atakapozikwa(Fukiwa).
Maiti ingeweza ingejisitiri na kupozi ili apendeza au kutokea vizuri zaidi....pia angechagua ni Picha gani itumike kutangaza Tukio lilipolekea Mauti kumfika.
Unapata faida gani ku-publish au ku-share picha ya Maiti?.....kwanini unataka tumkumbuke Marehemu kama Maiti na sio alivyokuwa Hai na mwenye furaha?!!
Unaweza kusema naegemea kwa Waingislishi kwa vile naishi huku na wao hawana utaratibu wa kuonyesha Maiti au kuiaga zaidi ya Jeneza na Picha ya Marehemu alipokuwa hai....nia ni kubaki na kumbukumbu ya yeye na sio Maiti yake.
Maiti inaagwa/angaliwa na wanafamilia au ndugu na jamaa wa karibu (kama watapenda, sio lazima). Lakini hukuti picha za Maiti ya Mpendwa husika kila kona ya Blogs na Magazeti.
Pia wenzetu Waislamu huwa hawatazami/aga Maiti sasa kwanini tusiheshimu Imani yao na kutopiga Picha Maiti zao na kuzisambaza Mitandaoni?.
Kwanza kitu gani kinakufanya uende kwenye Msiba wa watu na Lisimu lako, au Litablet au Likamera?....upo msibani kufariji na kuwapa ushirikiano Wafiwa lakini badala yake...wewe upo busy kuchukua picha na kushare na kuchat online.
Unaenda kwenye tukio(eneo alipofikwa na Mauti), badala ya kutoa ushirikiano upo busy kuchukua picha ya Maiti hatua kwa hatua kisha mbio mwenye liblog/lisite lako.
Hata kama ni Mwandishi wa Habari, hupaswi kutumia Picha za Maiti ya Mtu kwenye Gazeti, TV wala Site....kuwa na Utu hulipii Kodi!
Nasikitishwa sana na hii tabia ya Wabongo ya ku-publish Maiti za watu online na kwenye Magazeti.
Babai...
Mapendo tele kwako...
Juzi kati nimekutana na Picha ya Maiti ya Mpendwa wangu....pamoja na familia kufanya kazi ya ziada kuzuia upigaji Picha wa shughuli nzima ya Mazishi achilia mbali Mwili wa Marehemu wa mpendwa wetu zaidi ya alieajiriwa kwa ajili ya kazi hiyo....bado kuna jitu likapiga picha na ku-share online.
Kwasababu hana Uhai tena haina maana kapoteza Haki zake kama Mwanadamu mpaka atakapozikwa(Fukiwa).
Maiti ingeweza ingejisitiri na kupozi ili apendeza au kutokea vizuri zaidi....pia angechagua ni Picha gani itumike kutangaza Tukio lilipolekea Mauti kumfika.
Unapata faida gani ku-publish au ku-share picha ya Maiti?.....kwanini unataka tumkumbuke Marehemu kama Maiti na sio alivyokuwa Hai na mwenye furaha?!!
Unaweza kusema naegemea kwa Waingislishi kwa vile naishi huku na wao hawana utaratibu wa kuonyesha Maiti au kuiaga zaidi ya Jeneza na Picha ya Marehemu alipokuwa hai....nia ni kubaki na kumbukumbu ya yeye na sio Maiti yake.
Maiti inaagwa/angaliwa na wanafamilia au ndugu na jamaa wa karibu (kama watapenda, sio lazima). Lakini hukuti picha za Maiti ya Mpendwa husika kila kona ya Blogs na Magazeti.
Pia wenzetu Waislamu huwa hawatazami/aga Maiti sasa kwanini tusiheshimu Imani yao na kutopiga Picha Maiti zao na kuzisambaza Mitandaoni?.
Kwanza kitu gani kinakufanya uende kwenye Msiba wa watu na Lisimu lako, au Litablet au Likamera?....upo msibani kufariji na kuwapa ushirikiano Wafiwa lakini badala yake...wewe upo busy kuchukua picha na kushare na kuchat online.
Unaenda kwenye tukio(eneo alipofikwa na Mauti), badala ya kutoa ushirikiano upo busy kuchukua picha ya Maiti hatua kwa hatua kisha mbio mwenye liblog/lisite lako.
Hata kama ni Mwandishi wa Habari, hupaswi kutumia Picha za Maiti ya Mtu kwenye Gazeti, TV wala Site....kuwa na Utu hulipii Kodi!
Nasikitishwa sana na hii tabia ya Wabongo ya ku-publish Maiti za watu online na kwenye Magazeti.
Babai...
Mapendo tele kwako...
Comments