Skip to main content

Karibu, jisikie upo Nyumbani....

Utawekewa "Maeneji" mabaya nyumbani kwako na maukarimu yako yaliyopitiliza yasioyojua mipaka, shauri yako!


Unawajua wale wageni wanakuja kwako alafu wanaaza Ziara rasmi ya Chumba hadi Chumba, Droo hadi Droo, wanajipulizia Manukato yako na kujaribishia Viatu na Nguo zako.....WANANIUDHI sana.


Wazungu wao huona sifa au sijui ni Kacha yao! Hata sielewi, kama ni mara ya kwanza kufika kwake atakupa Ziara ya nyumba yote mpaka Stoo kwa hiari yao....(Tuwaache).

Ujue hapa Duniani bana kila mtu anamikosi yake, shida, raha na tabu zake. Hujui kapita wapi kutegemeana na "Imani" yake ili kujaribu kuiondoa Mikosi (kila mtu na siri yake bana). Siku unamkabidhi Nyumba yako unaanza kuona mambo hayawi mambo.

....usikute "eneji" yangu nzuri kwangu mimi na familia yangu, sasa ukinikabidhi nyumba yako nijisikie ka' kwangu alafu "eneji" yako mbaya ikai-triger "eneji" yangu nzuri na kuzalisha "sumu" yakawa mambo sio mambo usilalamike....Mfano tu usinijaji bana eeh!

Mie bana kwangu ni kwangu, ukija wewe ni Mgeni tu....nitapika, nitaandaa kila kitu hata kama nimetoka Kujifungua jana! Nitaitafuta tu hiyo nguvu....sikupi nafasi hata!....kwa Dinah hakuna "jisikie upo nyumbani BS" kuna "karibu sana" tu.

Ukitaka kitu niulize/niombe nitakuelekeza ukachukue au nitaenda kukuletea. Kitandani kwangu huweki matako yako(hukai) utaanzia wapi kwanza, Chumbani tu hauingii(ni marufuku)!

Hata nikienda kutembelea watu huwa "sijiachii" nyumbani kwa watu na kutembelea chumba hadi chumba(Uzungu wenu huko huko), hata kama nimekaribishwa kwa "jisikie upo nyumbani".


Stori time: Mie nilisoma Kutwa sio! Sijawahi ku-share chumba wala kitanda na mtu baki (zaidi ya wadogo zangu). Nilipokuja huku nikawa na-share nyumba sio Chumba wala kitanda, so wanafunzi wenzangu wa karibu (nyie mnaita marafiki) wakija kunitembelea walikuwa wakiishia Sebuleni.

Summer moja hivi Rafiki yangu akawa amepata replacement mahali karibu na kwangu, akaomba kuja kulala kwangu ili kesho yake awahi Kazini siku ya kwanza.

Nikamwambia hakunaga noma, wee njoo tu, nikamuandalia alale Sebuleni...heee! Mwanamke wa Kighana nusura alie kisa eti nimegoma asiingie Chumbani kwangu ku-"have a look".

Ikabidi nimfunde.....Kitanda ulaliacho na Mumeo hakipaswi kuonwa au kukaliwa na mtu ambae hamjachangia Damu (isipokuwa Mumeo).....ndio akanielewa.

Last Xmas alitualika kwake...mara nikahitaji kumbadili "Mini me" Nepi! Akanipeleka Chumbani kwake....kabla sijaingia nkamuuliza, "Sandy-O is this your bedroom?" Akasema "Yes-O, make yourself comfortable, feel at home-O". Nkagoma kuingia!(silly woman).

Ukarimu ni muhimu sana Maishani lakini kama ilivyo kwenye kila kitu, tambua mipaka au jiwekee "Mipaka" ya Ukarimu wako.


Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao