Kwanini Mataifa hayo yanaendelea kuwa Tegemezi wa Nchi za Ulaya Magharibi na Marekani?(Wacha sababu za Kisiasa na Historia hapa sio mahali pake)....
Leo hapa (kwako itakuwa Jana) Mimi na Asali wa Moyo tulikuwa tunajadili kuhusu Ubinafsi wa sisi wanadamu, tukafikia mahali tukakubaliana (kwa kawaida huwa hatukubaliani)!
Wazungu ni Washenzi kote-kote na wengi wao hawaamini Mungu as in kusali kucha kutwa na kwenda kutoa Sadaka kanisani kila J'2 lakini linapokuja suala la kusaidia Binadamu wengine wenye Matatizo huwa mstari wa Mbele!
Huenda hilo ndilo linalowafanya waendelee kufanikiwa, kwamba hawakai(kupoteza muda) kusali na kutegemea Mungu awashushie Mahela ili wawasaidie wengine au kukesha na kuomba ili Mungu awape Makazi wakimbizi mahali palipo na Vita.
Wanafanya yote hayo kwa Vitendo.... kuna Maduka kibao ya Misaada ambapo watu hujitolea vitu ambavyo hawavihitaji tena(Mitumba) na kuuzwa ili kusaidia Masikini wa Nchi zinazoendelea, Waathirika wa Vita n.k.
Pamoja na kuwa watumishi wa juu sehemu hizo za "misaada" hupata faida bado sehemu kubwa ya mapato ya "Misaada" inakwenda kwenye "kusudio".
Pia kuna wale ambao hujitolea kwenda "umasikinini" (Nchi zinazoendelea) au Vitani kusaidia Wakimbizi.
Ndani ya Nchi husika iliyoendelea kuna "Vikundi" kibao vya kupigania Haki za watu ambao hata hawawahusu, mf; Kusaidia watu wasio na Makazi, Kusaida wanawake wenye matatizo, Kusaidia "fund" kwa ajili ya wagonjwa wa Saratani na Uchunguzi ili kupata Dawa n.k.....ndio wanapata Mishahara mizuri lakini kazi zao zinatekerezwa na Matokeo yanaonekana.
Wote hao hawakeshi na kuomba kwa Mungu, bali wanathubutu na kufanya sehemu yao kwa Akili na Nguvu zao walizopewa na Mungu(niaminivyo mimi).....Mungu anawarudishia Baraka Zaidi ndio maana wapo hapo walipo(in my head).
Angalia Ebola(kwa mfano) inavyotupelekesha Afrika, halafu tunakesha na kukemea "pepo la Ebola toka kwa Jina la Yesu" aliekuambia Ebola ni Pepo nani?.....na bado unasubiri Mzungu akuletee Dawa....Madaktari wa Afrika na Serikali zao walikuwa "Wavivu" kufanya research tangu Ebola ilipo ibuka Demokrasia ya Congo kwa mara ya kwanza?......Aiiii nimeingia kwenye Siasa sasa, wacha nifunge Simu.
Furahia Mwanzo wa Mwisho wa Wiki yako...
Babai.
Mapendo tele kwako...
Comments