Skip to main content

Na-admire sana watu wa Medical...

Nakupenda kwa kuichagua Blog hii...

Unajua wale wadada wakubwa inatokea unawapenda, unatamani kuwa kama wao (Kielimu) utakapokuwa Mkubwa?!!






Mie nilikuwa nawapenda sana Wadada Wanasheria, Waandishi wa Habari na Young Docs (au tuliwaita Medical assistants sababu walikuwa hawajafuzu).....sasa kuna mmoja alikuwa jirani yetu enzi hizo bado kabinti, alikuwa anasoma Russia.






Kwasababu alikuwa Mkubwa sana kwangu hatukuwa na utaratibu wa kuongea lakini tulikuwa karibu sana na alionyesha kunipenda kweli-kweli!






Kila J'Mosi alikuwa ananiita "Dinah Mdogo wangu unakazi?(Za shule)... ukimaliza naomba uje unikwangue Mba"!! Usicheke tafadhali (hihihihihihihahahahahaha)...Basi mwenyewe nafurahi naenda kumkwangua "dada MA" Mba....honestly!!!






Namkwangua, nikimaliza nampaka mafuta halafu namsuka....heee! Najua kusuka blaa tangu nina miaka 7 shukurani kwa Bibi na MSesere(Doll) wangu....nika-master Kusuka Mitindo nilipofika miaka 15 hivi....by 18 nilikuwa nasuka watu kwa Hela including Dada mMedical Assistant baibeee (Nimeanza kujitegemea kiuchumi kitambo ujue!).






Sifa kuu ni kuwa nikimsuka mtu simvuti/umizi ngozi na nywele zake hazikatiki akifumua....SISUKI watu usijedhani najitangazia Biashara bure!!






Baada ya Muda Dada akawa sijui "MD" sijui nini nini na akaolewa, akahama na kuhama....bado na admire sana Medical People, Naomba sana wanangu waje kuchagua kusoma Medicine.






Napenda Proper Degrees, sio zile useless zile sijui ninininiLogy zile....ah nimepoteza Track ya nilichokuwa nazungumzia.....Hebu nikumbushe!


Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao