Ni vema kuwa Mshindani mahali pa Kazi, Shuleni au Kimichezo, kwamba ni vema kuhakikisha unakuwa juu/mbele kuliko uwezo wako.
Unaweza kuwa umezaliwa hivyo(mshindani) au umejifunza kutokana na "kusukumwa" na Wazazi wako.
Nimewahi kuzungumzia hili lakini niliegemea zaidi ushindani kati yako na watu wengine uwaonao kwenye Sosho media au Mtaani(au was it in my head?).
Pamoja na kuwa ushindani unakusaidia kufanya vema kwenye maisha yako Kikazi, Kielimu au Kimichezo bado hali ya Ushindani au kutaka kushindana pasipo husika kunaweza kukuharibia.
Ukiiendekeza hali hiyo na kuiweka kwenye kila kitu ufanyacho inaweza kuumiza watu wako muhimu kama vile mke/mume, watoto na ndugu.
Kabla ya kufanya mapenzi hii inakuna kichwani "juzi na jana nilianzisha mie au nilikuwa juu.....leo zamu yake. Bila kusema unamsukuma au kumvuta mwenzio awe juu yako"? Huo ni ushindani na can put mkeo/mumeo off.
Katika hali halisi....anaelianzisha ndio atakae so huyo huyo ndio awe mtendaji mkuu, kwamba amfanye mwenzie atake au awe tayati kuneng'enuka.
Pengine sio mshindani kwenye kufanya mapenzi lakini ni mshindani kwenye masuala mengine......unarudi home na kuanza kugombania TV kwa mfano...."umeshinda nyumbani siku nzima sasa ni zamu yangu".
Wengine mnapitiliza mnashindana na watoto wenu....."mmeangalia vipindi vyenu siku nzima sasa ni zamu yangu " hihihihihi well this was me nikaamua kubadilika na kuangalia Tv watoto wakilala( kama sijachoka that is).
Binafsi sio Mshindani yaani sina habari na nani kafanya nini-wapi-kwanini lakini napenda kuganya Vema na kufanikiwa hivyo naelekeza nguvu zangu kwenye Bidii zaidi ya "lazima niwe kama fulani au zaidi yake"!
Ni vema kuacha ushindani wako mahali pa Kazi au Elimu-ni na sio kuwa mshindani kwenye kila kitu na hivyo kuharibu au kuondoa maana ya Familia/Ndoa yenye furaha.
Nakupenda kwa kuitembelea Blog hii leo.
Babai.
Comments