Skip to main content

Wanawake na Usenge!

Kwanini sisi wakimama ni wepesi sana kukubali hawa jamaa?.....Hi are you well?


Usinielewe vibaya! Siwachukii wanaojibadilisha kutoka Jinsia moja kwenda nyingine(I feel sorry kwa mume/mke na watoto though). Pia sina habari na Wanaume wanaopenda kujiremba au kuvaa nguo za kike.



Hakika sijali nini mwanaume na mwanaume mwenzie au mwanamke na mwanamke mwezie wanafanya chumbani kwao(keep it there).




Lakini sitoacha kujiuliza au kuuliza ni nini hasa kinafanya wanawake kuwa wepesi kuwakubali hawa jamaa kwenye Jamii? Kwanini sisi ni wa kwanza kuwachukulia poa na hata kurafikiana nao?



Ni ile "huruma nature" tulioumbwa nayo au ni kwasababu Wanaume wengi ni Waoga wakidhani hali hiyo(Usenge) inaambukiza so wanakuwa wagumu au wenye Chiki/hasira wakihofia "kubadilishwa"?


Pengine wanaogopa kuwadondokea Wasenge wa Kiume hihihihihi kama unaeza mtamani wa jinsia yako akiwa Mtupu na ukawimika wewe ni Msenge tu hata kama umeoa na unawatoto.....usiogope toka Kabatini.



Back to the post: Binafsi (dada mkubwa) mwenye Wadogo wa Kiume. Hakika nilikuwa napata hasira nikifikiria vipi madogo wakiwa  Wasenge? Nitawachukia? Nitawaua?


Natambua hii ni hofu ya wazazi wengi(hasa wa kiume) na can break your heart lakini kutokana na Mazigira yalivyo sasa na urahisi wa kufikia au kipatabinfomations ni vema tubadilishe namna tunakuza wenetu.


Kamwe sitokufundisha  namna ya kumlea mwanao au kukuambia lea mwanao kama nileavyo wanangu......mwenyewe najifunza daily hapa.


Nina Kijana na Binti.....je huwa namfikiria Mwanangu wa kiume kwenda kwingine na hivyo kujitahidi kumlea kama MWANAMUME? Hapana!


Nawalea wanangu kama wanangu....kila moja anajijua kuwa yeye ni a Girl na mwingine ni a boy so i go with flow.


Babuu akilia-lia au kunung'unika simuambii "boys dont cry.....au dont cry like a girl" namwambia a 4yr old...grown nursery boy dont cry like a stay home baby. Hapendi kuitwa baby na hapendi kukaa nyumbani so that works.



Unapoanza kum-feed mtoto kuwa Wavulana ni  Wakakamavu, Jasiri, hawalii au kuwa emotional ni wazi kuwa unamwambia mwanao wa kiume "usiwe kama msichana" au Wasichana ni Wadhaifu.



Watu wenye tabia hii ni wanaume ambao hawathamini mwanamke na nadhani wanahofu kuu kuwa watoto wao watakuwa Wasenge.....wakidhani Usenge ni kuwa mwanamke.



Usenge sio Uanamke.....kupenda kuvaa mavazi ya kike au kujiremba sio Uanamke....kuwa na Matiti sio Uanamke.....kuwa mbeya sio Uanamke.



Mimi kama mwanamke najiamini na kukuambia kuwa Uanamke ni zaidi ya kuwa emotinal.....unamke ni zaidi ya kulia-lia na mengine ambayo Wanaume mnaita "tabia za kike"



Nimechanganya topics didn't I? 2-in 1 Blog post si ndio. Asante kwa kuichagua blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao