Skip to main content

Je Unaogopa Kujaji watu(wenzio)?


Habari yako?


Nilikuwa Likizo ya Kiangazi.....katika hali halisi  nilipaswa kukujulisha lakini nikahisi kama vile nitakuwa najionyesha au napitiliza ku-share so nikapiga kimya. Anyway habari kwa ufup,  kama bado unajali ni kwamba Madoa ya Tetekuwanga(Chickenpox) yamepungua Weusi.




Ujisedhani hali ya Hewa ya UK inafanya Ngozi kutakata haraka ndugu, nilipewa Mkorogo(andikiwa dawa ya kuondoa Weusi) nitumie kwa Muda wa Wiki 8. Baada ya kugusa Wiki ya Pili nikaona Vijitundu vya ngozi(pores) vinapanuka! Aiiii nikautupilia mbali Mkorogo.



Duania ya leo inamengi na kila kukicha tunaongezewa sheria za namna ya Kuishi vizuri au kuishi na watu kwenye jamii. Tunaambiwa tusiwajaji wenzetu kitu ambacho sio rahisi kwa sababu kujaji ni asili ya  mwanadamu, pia bila kujaji hakika utakuwa unafanya maamuzi mambovu na hivyo kuishi ukilalama "kwanini mimi".




Nimekwishawahi kukuambia hapa(kwenye blog hii) kuwa mie huwa najaji watu/mtu kama wewe ila tofauti yangu mimi na wewe(hello hihihihi) ni kuwa, huwa najitahidi kuelewa na kukubali kwanini wapo walivyo au kwanini wanafanya wafanyavyo nikishindwa naishia na "but why?". Sina tabia ya kumchukia mtu au kumcheka ama kumdharau kwasababu nimepitisha "jajimenti" kutokana na muonekano wake au matendo yake mabaya ya awali ama Ugonjwa/matatizo yake kiafya.







Nina uhakika kabisa sio Mimi tu ambae najaji watu ama vitu na pengine vitendo vya mtu kabla sijamjua/fahamu......naamini wewe pia unajaji kabla hujafanya uamuzi wa Kurafikiana  na mtu au kununua Kiwanja au nyumba na pengine Bidhaa fulani kwa ajaili ya matumizi binafsi au ya familia.





Sasa unaposhupaa kuwaambia wenzio kuwa "msinijaji mpaka mnijue kwanza" unakosea.....kwasababu hakuna mtu ana muda wa kusubiri akujue kwanza halafu apitishe "jajimenti".....mfano mdogo ni pale Mabinti wanapogombania kuwa ma-Miss, pamoja na vigezo vinavyowekwa bado unakuwa "judged" na Jamii  kabla hawajapata nafasi ya kukujua(via magazeti ya Udaku).





Nukta ni kwamba usiogope kujaji kwasababu ni "human nature" wakati mwingine huwezi kujizuia kwasababu kuna poster zinasema "dont judge me before you know me" sijui "nenda kafanye kazi badala ya kunijaji".....wakati unajaji unakuwa njiani kwenda Job. 



Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao