Skip to main content

Ngono ya Usiku mmoja M'ke vs M'me....



...nani Malaya? Hello there.


Kwenye harakati za Mpito za Ujana ni wazi unajifunza kwa kufanya mambo mengi kwa kupatia au kukosea. Sio mara zote unakosea ili kujifunza(usifanye makosa makusudi kwa kisingizo cha kujifunza), wakati mwingine unakosea kwa Uzembe(kutokujali).





Kama ilivyo kwenye kila kipindi cha  " Mpito" mambo huwa magumu.....wakati mwingine mtu unajikuta unakata tamaa na kuamua kuwa LIWALO NA LIWE na hapo ndio maamuzi ya kizembe yanapojitokeza. Inaweza kuwa Pombe au Utumiaji wa madawa na Ngono Holela au vyote.




Inawezekana kabisa kufanya hayo ni katika hali ya kutafuta "amani" au kuondoa "msongamano wa mawazo" na pengine ku-fit in na jamii inayokuzunguuka wakati huo wa Ujana wako. Kwaharaka haraka unaweza kudhani umepata "tiba" lakini katika hali halisi unajiongezea shida/majukumu kabla ya Muda wako.




Sasa, kutokana na hali ilivyo siku hizi (Mambo ya Haki sawa sijui Usawa) inafanya mambo mengi ambayo awali yalifanywa na baadhi ya Wanaume tu sasa hufanyika kwa urahisi  kwa upande wetu wakimama ( hello Feminist).....ni vema kwenye masuala ya Kikazi, Kipato, Kielimu na Heshima. Linapokuja suala la Ngono ya USIKU MMOJA ondoa imani/msemo kuwa "kama Mwanaume anaweza hata Mwanamke anaweza".






Pamoja na Ulevu wangu  wote(mdogo) kwenye suala la Usawa, ikiwa wewe ni mwanamke huwezi kujifananisha na Mwanaume linapokuja suala la Umalaya. Huna haja ya ku-justfy Umalaya wako kwa kusema " mie mwanamke Malaya, lakini Mwanaume Player".....kama umeamua kuwa Malaya fanya hivyo kwasababu zako nyingine na sio "Usawa"!!





Unataka nikuambie kwanini? well....kwa kifupi ni kuwa Wanaume na Wanawake tumetofautiana Kimaumbile(kama ulikuwa hujui), Mwanaume hazai, wewe unazaa, mwanaume akifanya ngono na wewe akioga unakuwa umetoka mwilini mwake(kwenye ngozi ya uume wake), lakini wewe utaendelea kuwa na mwanaume huyo kwa namna mbili tofauti Moja zaidi ya Siku tatu (kama hukutumia Condom) na Pili, ni kwa kati ya mwezi mpaka miezi 3(kwa Uke wako kujirudi), ikiwa Umbile lake lilikuwa kubwa.





Nikuambie pia Kiimoshino na Kisaikolojia?....aii nafasi imejaa, hebu Kaguge.


Nisikuchoshe

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao