Skip to main content

Kwa Mliojipiga/Lipua/Fuata Sheria Ughaibuni....


....yote Maisha na kila mtu anayatafuta kwa namna yake sio(usidhani nakukebehi, naelewa sana). Sasa kama ilivyokawaida ya Mie, ninapohisi kuwa nimejifunza huwa sio mchoyo ku-share. Hujambo lakini?




Unafurahia simu yakoo Mpya(smartphone) ambayo ipo loaded na ma-Apps mwengine wala hujui kazi yake(unadhani yanafanya Simu yako kufanya kazi vema) kumbe katika hali halisi sivyo. Baadhi ya Apps(zile zinazowekwa kila unapo Update Software) huwa zinawekwa na Mitandao husika ili kufuatilia Nyendo zako.




Tangu zamani wamekuwa wakifuatilia ili kuboresha Huduma za Mawasiliano, lakini kutokana na uwingi wa Uovu hasa kutoka kwa wenzetu wale Wauaji kwa jina la Dini yao takatifu, hali imekuwa mbaya linapokuja suala la "privacy".



Sio Kampuni za Simu tu ndio zinatabia(banwa Kishria) bali pia Facebook, Google na Whassap wanatabia ya kutunza yote unayo-post kwa ajili ya "kuboresha" Huduma zao (wanamaanisha kutunza Data uwekazo kama Ushahidi pale  mambo yamebuna na Serikali/Polisi wanazitaka).




Umewahi kuiona Application kwenye simu yako inaitwa Computrace Agent? well pengine wala huna habari kwasababu sio mtu unaependa kujifunza nini kinafanya nini na kwanini? sasa CA inaku-monitor wewe na yote usemayo ufanyayo unapokuwa kwako au mahali popote uendako(so long unabeba simu yako).




Hii Computace Agent App haitoki hata ufanye nini? na wala usijipe Moyo kwa kusema "natumia simu hii lakini namba ya whassap sio namba ya Mtandao wa Simu hii"......muhimu ni Device sio namba ya Simu.




Haya endelea kujiachia na ndugu zako wa Kibongo waliopo Bongo huku mnabadilishana mapicha ya kihistoria(utotoni), au...au...ulienda kumtembelea Rafiki yako Bongo baada ya yeye kukualika huko (kumbe ulienda kwenu) wakati Serikali inakutambua wewe kama Msomali, Mrwanda, Mzanzibari, Mkongo, Mrundi, Mmisri au kutoka kokote kwenye Machafuko Kisiasa na huna Ndugu aliyebaki(wote waliuwawa hihihihihi).....akili kichwani mwako.




Mie binafsi nafurahia Teknolojia hii kwasababu napenda  na kujali Usalama wangu na Familia yangu (si wajua mambo ya kutekwa, kupotea, kuibiwa n.k), hii App na nyingine kama hii ni muhimu sna Maishani, Ila kwako wewe inaeza kukuletea mwisho wa kuishi Ughaibuni.


oh hey....nakupenda kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao