Skip to main content

Pale unapokuwa Mke mwema....


....halafu unaonekana sio mwanamke "kamili", kwanini? kwasababu hulalamini-lalamiki pale mumeo anapoacha bafu chafu baada ya kuoga au pengine anachelewa kuamka na kuacha kitanda kipo shagala bagala....(hizi sio kazi za mwanamke ni usafi), huombi-ombi pesa ya manunuzi, Vipodozi wala Salon.





Inawezekana upo hivyo kutokana na Malezi/mafunzo uliyopitia au huenda umejifunza kupitia Blogs, maana Siku hizi kuna kila aina ya maelezo yanayotuelekeza namna ya kuwa  Wake(na waume) wema, mengine ni mazuri na mengine yanapotosha.....Akili kumkichwa unapoamua kuchukua na  kujaribu ulichokisoma!





Ulalamishi na kutaka jambo/kitu kifanyike pale tunapotaka  ndio  inatufanya wanawake kuwa wanawake (ni sehemu ya uanamke), sasa hayo yakikosekana inakuwa kama vile Mumeo ameoa  mwanaume mwenzie ahahahaha. I mean sawa kujitegemea kiuchumi na kuepuka ulalamishi.....lakini pia tukumbuke kuwa baadhi ya Wanaume hupenda Changamoto Ndoani (sio za kugombana na muumizana mioyo/hisia)!





Natambua kuwa unajua kuwa Changamoto kwenye Ndoa zipo za aina  nyingi na zinatofautiana, nitakupa mifano(kama kawaida) kuna zile zinamsaidia kufanya maamuzi ya Busara kwa ajili ya Familia  yenu, zipo zinazomsaidia/msukuma kuwa Msafi/kuwa na Manners, pia kuna ambazo zinamfanya ajisikie MwanaMume(ridhisha ego yake), kuna za Asili(Magonjwa) na kuna zile za kuangamizi Ndoa yenu.




Sijui utakubaliana au kutokubaliana na lipi hapa! ila kama umesoma mpaka mstari huu na umepata hisia ya kutaka kujibu/comment kwa Hasi au Chaya basi tambua kuwa umekuwa inspayadi.


babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao