Skip to main content

Knowledge vs Ego....


Kwa maCeleb Ego hujionyesha wazi kwenye mahojiano ya moja kwa moja. Baadhi wanadhani kuwa ni wao tu ndio wanazo hizo Ego, nitakupa mfano na pengine kukusaidia(kama hujui) kuitambua kutoka kwa Mwenza wako.

Kwa mimi na wewe Ego zetu hujitokeza zaidi pale tunapogombana. Ndoani/Mahusiano huwa tunagombana sana eti? Wakati mwingine ugomvi unakuwa hauna hata maana.


Ujue kuna ile kugombana kwasababu mmoja wenu kafanya kosa kubwa kama vile umegundua kuwa amekuwa akipeleka Pesa mahali ambapo hupajui! Kwa mfano. Sio kwanini hakupokea simu?!!


Na ikiwa mnawatoto basi mnaweza kugombana kwasababu mmoja wenu anahisi kuwa anaingiliwa kwenye kona yake ya malezi(wanaume) au mwingine(sisi wakimama) kuhisi kuwa watoto wanaonewa au mwenzio hatoi muda kuwaelewa watoto na badala yake anatanguliza kufoka (hasira) kwa watoto.


Katika hali halisi kama mmoja wenu anawakilisha linalomkwaza kwa namna ya kawaida(kukereka bila hasira/kufoka) na mwingine kusikiliza hakutokuwa na ugomvi. Inaitwa MAWASILIANO/KUWASILIANA.


Lakini kwa sababu ya Ego kubwa (kujiamini kupita kiasi/kiburi) au ndogo(kutojiamini/kujishtukia)ya wenzetu wa Jinsia ya Kiume kunasababisha issue ndogo kuwa kubwa.

Kwanini inakuwa kubwa? Kwasababu wanawake tunapenda kuongea na kuelezea kila kitu(mie), wakati wenzetu hawapendi kusikiliza na matokeo yake utaambiwa "yameisha, sitaki kusikia/ongelea hii issue tena" wakati hatujamaliza. Au anakuvuta na kukubusu au kufanya Mapenzi matamu ya ki-Ego hehehehe  ili tu usiendelee kumwaga manoleji.


Sasa kwasababu hujamaliza ni wazi kuwa issue itakuwa inaning'inia na itakukera kwa muda wa siku 3 kama sio Wiki nzima....kwanini amekukatisha?  Kwanini hataki kuimaliza issue na mfikie  mafaka? Well sababu ya Ego yake.


Kwa Weusi Ego huenda juu kupita maana ya juu kwasababu wanaume wa Kiafrika hawapendi kufunzwa au kuelekezwa na Wanawakee......ikiwa mwanamke anaelekeza basi utaambiwa huna heshima au unajifanya unajua wakati hujui kitu(kwasababu tu wewe ni mkimama).


Kisayansi, Wanawake tunakua kiakili haraka kuliko wenzetu na wepesi kujifunza na wazuri kutunza info (za maana na makorokoco)kuliko wanaume. Pia tunafunzwa au tunapata uzoefu wa kimaisha kama sehemu ya kufunzwa, tofauti na wanaume ambao huachwa wajifunze wenyewe. Hivyo ukweli ni kuwa sisi tuna knowledge kuu zaidi ya wanaume(inategemea na umri/elimu though).


Sasa unafanya nini ikitokea Ego ya mwenza wako ipo juu zaidi ya Masikio yake? Well akianza kuja juu wewe Msikilize halafu dharau. Siku akitulia ibua issue kwa upole na muimalize.


Ukijibu ni wazi mtakuwa mnajibizana na hakutokuwa na mtu anaemsikiliza mwenzie na matokeo yake mnaishia kuwa na mahasira ambayo hawasaidii.


Sasa Imagine mmoja wenu anarudisha namba(anakufa) baada ya ugomvi wa kijinga unaohusisha ego zaidi ya Uelevu? Anakufa bila muafaka......Ze hatia sasa!
Ahsante kwa kuichagua Blog hii.
Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao