Skip to main content

Jinsi ya kutojali.....au niseme jinsi ya kuto-give a damn?


....pengine how not to give a F*ck imekaa vizuri!! najua maana moja tu ya hilo neno F, nakumbuka Mwaka wa Kwanza Chuoni(when I was in London)....Jamaa mmoja alinambia "go f**k yourself" nkamwambia really?can you show me how?.....Darasa likawaka moto kwa kicheko. sasa sijui walikuwa wananicheka mimi(sijui Kiingereza) au jamaa. Achana na hili!



Kujali kuhusu kila kitu au mambo ambayo watu wanajaribu kukufanyia na kwanini wanafanya hivyo husababisha maumivu ya Hisia.....unajua ile hisia unayoipata(ulipokuwa mdogo) pale unapomsalimia mtu Mzima halafu haitikii? Unaanza kujiuliza huku "umia" Baba/Mama nanilihu kwanini haitikii "shikamoo yangu"(labda alikuwa anakutaka) but kwa umri wako mdogo unahisi kama vile umenyang'anywa kitu cha thamani kinachoitwa "Heshima kwa wakubwa" ambacho Baba na Mama yako walikufunza.



Mie binafsi nilikuwa nalalamika daily Watu Wazima wakinichunia, siku Marehemu Baba akanambia "kama hawaitikii Salamu yako basi usiwasalimie, achana nao" nkahisi huyu Mzee vipi? Unatufunza  daily tuwe na adabu na kusalimia wakubwa wetu, leo unaniambia nisiwasalimie.....tena? 


Tangu siku hiyo nikawa "Mwanzilishi" wa kuuchuna, nikiamini kuwa huwzi kunichunia mimi wakati mie ndio CEO hihihihihi silly eeh! Ukinichunia kwasababu ya issue zako za Kimaisha na mie nakuchunia milele. Hii imenisaida sana kwenye kutojali kuhusu watu wengine watanifikiriaje.




Ni rahisi sana kumwambia mtu asijali watu wanasema nini juu yake na kwamba yeye aendelee na Maisha yake, hasa kama mhusika ni Mdogo(20s). Unaweza kudhani kuwa Era  hii ya Sosho Midia ni rahisi kwasababu kuna Memes, Ushauri wa Jinsi(hows)  na Quotes kila kona. Uwingi wa hizo "makitu" ni  kithibitisho cha ongezeko la Ugumu wa "kutokujali" watu wengine wanasema/fikiria nini kuhusu wewe au chochote ufanyacho.



Kila mtu Duniani anamaoni yake kuhusu kila mtu na kila kitu....Wakosoaji, wafuatiliaji na kila aina ya watu wapo huru na karibu zaidi na wewe(japo hawakujui) kuliko ilivyokuwa Miaka ya nyuma(wakati mimi nakua miaka ya 90).



Pamoja na kuwa sehemu ya kukosolewa huko kunaweza  kukusaidia kufanya mabadiliko na kuwa mtu bora/mwema zaidi bado kama binadamu una hisia na unaweza kuumia  kwa kiasi fulani na ukashindwa kufanya kile ufanyacho au kuboresha kile kilichokosolewa9inategemea na Uimara wako sio).



Kama kawaida, mimi nimeishi maisha  tofauti sana na "dada yako" mkubwa  na kwa muda mrefu  kukupita wewe hihihihihi hivyo nitakupa Hows zangu za  kutokujali Walimwengu wanasema nini, Kwanini na wapi? Chagua unalodhani unaweza kulifuata na kisha changanya na ya kwako na ya watu wengine ili kufanikiwa kwenye hili. Ila  ukifanya haya (bila mpangilio huu)yote  na kuchanganya na uyajuayo utanufaika zaidi. Twende sasa:-



1-Uvumilivu- Unapitia hayo yote kama sehemu ya Ukuaji, unajifunza along the way na  the moment unaingia 28 utaona mabadiliko Makuu ya jisni unavyopokea na kuchukulia vitu/mambo. Haya unayopitia sasa utakutana nayo tena baada ya Kuolewa/Oa, yatahusisha watu ambao ni Muhimu kwa Mkeo au Mumeo....usipojifunza kuchukulia watu kama walivyo au kutojali sasa, ni wazi utaiona Ndoa ni Chungu na kuhisi umeolewa/Oa Ukoo Mzima.



2-Focus-Weka Focus yako kwenye mambo muhimu zaidi kwako kuliko mtu/watu wengine ambao sio muhimu. Unacotengeneza sasa ndio kitakachokusimamisha huko mbele kimaisha, iwe ni Elimu, Biashara, Mafunzo n.k. Pia Focus yako kwenye ufanyalo itasaidia usiwe na Muda wa "kujali" yasioyo na Muhimu.



3-Toa time out-Kwa Ndugu/Jamaa/Marafiki ambao ni wabaya/wasio na umuhimu kila baada ya muda(mie nilikuwa nafanya kila mwaka).....usisubiri mpaka wakukosee. Angalia tu ni nani anaumuhimu kwa sasa na ubaki nae karibu, wale ambao hawana umuhimu wachunie kwa muda. Hii huokoa muda na kupunguza Lawama.


Wazuri sio wale anaokuja kwako/kwenu kila siku au kukupigia simu kila siku na kuchat/catch up(kila siku?). Wazuri ni wale wanaoheshimu Muda  na  Nafasi yako....lakini ukipatwa na Shida watakuwa  karibu na kusaidia kwa namna yeyote awezayo.




4-Jione/Tambua kisha Jisifie- Ukingojea kusifiwa, utangoja sana na ukitegemea  Likes, RTweets tambua tu kuwa wasifiaji wa Online sio wakweli hihihihi (most of them). Sasa ni lazima utakuwa na moja (au yote)kati ya haya  mf. Elimika(kishule au kidunia), mrembo/mtanashati, Imara, unamahali pa kulala(hata kama ni kwa mama/baba), unajilipia/changia bills, unafanya mambo na kufanikiwa bila mchango wao. Lolote zuri au unalojivunia wewe kama wewe.....Jipe sifa!




5-Jitolee Muda-Kusaidia wengine. Kumsaidia Mtu sio lazima umpatie pesa. Muda wako ni Mali tosha, na huitaji kujitolea Siku nzima.....somea watoto kitabu mara moja kwa mwezi/wiki, saidia wengine kujifunza somo ambalo ni gumu kwao lakini kwako ni jepesi. Fanya jambo kwa ajili ya mtu mwingine ambae hakuhusu(toa msada/saidia).



6-Jisomee...iweni Koran(Koroani), Biblia, Makala, Vitabu, itakusaidia kujifunza zaidi na kupata Amani.


-7-Usiogope kujitoa "mhanga".....Kama kuna issue inajadiliwa popote ulipo (kwa mfano)na unahisi kuwa unataka kuongezea, Uliza au kupinga with facts/points au kuunga mkono. Ingia kati na chukua sehemu yako na simamia usemacho lakini pia kubali kujifunza/elewa points kutoka kwa washiriki wengine.



-8-Usiogope kukosea..... lakini usikosee makusudi(makosa yatakusaidia kujifunza zaidi)


9-Jipe time off Sosho Midia, au kama unaweza chagua  Platform Moja na usiwe kwenye kila Sosho midia "outlet". Kumbuka Dunia imekuwa Kijiji(Ahsante Teknolojia na urahisi wa kuifikia Internet), kwenye kila Sosho Midia utakutana na watu walewale na tofauti itakuwa majina labda, lakini mitazamo yao inaweza isibadilike. Sasa kama hawakupendezwa na wewe Insta hawawezi kupendezwa na wewe Snapchat etc.




-10-Kuwa Mbinafsi....ulikuja Duniani(ulizaliwa) peke yako na utaondoka(kufa) peke yako! So yeahaa don't give a fuck of what-who-where or why. Post hii nimelenga wadogo zangu, lakini kama wee umekua mwili tu na akili bado imebaki in your early 20s.....hongera kwa  kuibamba Post hii.


Ahsante kwa kuichagua Blog  hii na tafadhali share, tambua kuwa nathamini muda wako hapa.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao