Skip to main content

Kukabiliana na Mwenza/Mpenzi "mpya" baada ya Miaka kadhaa...


....kwa maana ya yeye kubadilika/shwa na "Rafiki" zake kama niliyogusia Post iliyopita, ikiwa hukuisoma basi bonyeza hapa. Upo salama lakini?....twenzetu!


Kwanza kabisa usimwambie kuwa umebadilika, lakini akikujia na mambo mapya ambayo awali hakuwa akipenda/fuatlia then hoji kulikoni? mf: tangu lini Mpenzi unatazama Eastenders? Hee siku hizi unafuatilia hiki/kile? hii itamfanya atambue kuwa unaona mabadiliko.



Pili, Jiweke mbali, yaani mbaaaaaali na hao/huyo "Rafiki" unaedhani ana/amembadilisha Mwenza/Mpenzi wako. Usimuulizie, akianza kukupa stori bila kutaja jina la Mhusika, wewe sema tu "tunamzungumzia John"(taja jina la huyo rafikie mpya)? Halafu onyesha kuwa huna "interest" ya kujua zaidi.(hii itafikisha ujumbe na hivyo kuacha stori za huyo mtu/watu).



Tatu, Ataanza kutaka kukutanisha wewe na huyo "Rafiki" kwa kisingizio chochote tu, kuanzia "ametualika kama familia" au "anataka kuja kututembelea ili awaone watoto/apajue Nyumbani". Weka Mguu chini na mtolee Nje kwa upendo na upole kwa kumwambia kuwa Mpenzi/Mume wangu....vyovyote unavyomuita. Ashura ni Rafiki yako, mmekutana Kazini na nafurahi umejenga urafiki na mtu Mahali pa  Kazi. Ila ni vema kama ukitenganisha Maisha yako ya Kazini na ya Nyumbani.



Hapa lazma atabisha kwasababu atakuwa tayari kaongea na kumhakikishia "Rafiki" yake kuwa atakwenda  na Familia/Mke/Mume wake, sasa ili asimuangushe ni wazi atakubishia na hata kuonyesha Ukali na kukufanya ujisikie kuwa hupendi watu, atasema hakuelewi, atasema umebadilika na mengineyo basi tu kukuuudhi ili umkubali. Usi-panick. Tabasamu na Mwambie haupo Comfy  kukutana na Mtu wa Kazini kwake amjue yeye Mumeo/Mkeo/Mpenzi wako huko na sasa amjue Nyumbani pia.



Ongeza kwa kusisitiza (ukiwa firm bila kufoka) kwamba  huyo ni Rafiki yake yeye na sio Rafiki wa Familia yenu hivyo basi ni muhimu ya Kazini yabaki huko na ya Nyumbani yabaki Hapa(nyumbani). Kama ni muhimu sana na hutaki kumuangusha rafiki yako, basi nenda mwenyewe. Mimi na Watoto(kama mnao) hatuhusiki na urafiki wako wa Kikazi.



Nne, Mwambie mwenza wako kuwa ni vizuri kutengeneza Marafiki lakini ni vema zaidi ikiwa mtatengeneza marafiki kama Pea nje ya Kazi, kwamba muwe na Marafiki wapya ambao hamkukutana Kazini. kwasababu kuwa na Rafiki anaekujua Kikazi, Kisosho na Kifamilia/Nyumbani ni Hatari na ni Mwanzo wa kutengeneza Adui.



Kumbuka, wapo watu wanatafuta Marafiki ili kujenga Uadui  mahali pa Kazi. Utendaji ni Ushindani. Kupata kazi na Kubaki kwenye kazi na hatimaye Kupanda Cheo kunahitaji Ushindani. Ushindani huo unaweza ukawa Mzuri kabisa na ulio-base kwenye utendaji na Bidii yako, lakini pia wapo ambao hupenda njia za Mkato.




Sasa unapoanza Kazi mpya, unakuwa "vulnerable" na hivyo  "maadui" huchukua nafasi hiyo ili waje kukumaliza kirahisi huko baadae. Sikutumi kuwa usijenge marafiki kwa kuhofia wao kuwa Maadui baadae, isipokuwa nasema kuwa ni muhimu Rafiki wa kzini wabaki huko na Nyumbani wawe wengine. Ikitokea Kazini kumebuma, angalau Nyumbani kutakuwa Salama....kwamba  hamtowavuruga Watoto na hakutakuwa na "Mama mbona hatuendi tena kwa akina Peter"?  "Mama naomba kumpigia Simu  Antie Rose". Vilevile Adui hatokuwa na lolote alijualo kuhusu Nyumbani kwako na kulitumia ili kukumaliza zaidi.


Nadhamini Muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao