Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2014

Ijumaa moja Baada ya Mauaji ya MwembeChai!

Maisha haya! Nimekumbuka 1996/97 Mauaji ya Mwembe Chai (siku mbuki vema na sitaki ku-google vilevile)! Siku chache baada ya Mauaji yale bado kulikuwa na Maandamano ya Siri ya "Waislamu wenye Hasira".....Kile kifo cha yule Kijana pale Mwembe chai akianguka LIVE baada ya kupigwa Risasi na Polisi (FFU sijui) akiwa amevaa shati la Bluu Mpauko(light Blue) kamwe haitonitoka Kichwani! Ni kifo cha kwanza nilishuhudia live(on Tv)!! Sasa bila kujua si tukaenda Kariakoo siku ya Ijumaa! Ile tumemaliza manunuzi si tukakutana na Waandamanaji na FFU...wakayaachia Mabomu ya "Machozi"....oh boy! Nilihisi Vita kuu ya Mwisho wa Dunia ambayo sina Uzoefu nayo ndio imefika!!! Kimbia, huku na kule mara Tukakutana na jamaa (sijui Katibu au Mlinzi, ila alikuwa Mhindi) Wa SSC pale Msimbazi, akatufungulia Mlango kwenye Jengo la Simba....akawa anaita akina Mama na Watoto waende kupata Huduma ya kwanza....hihihihi kunawishwa Maji Usoni(wasn't a laughing matter then)! Anyway! Baada ya hapo k

Kujikanganya nako!

Kuna siku nilisikilizishwa Nyimbo za Bi Rozi Mhando akizungumzia "Kunyang'anywa" Mali zao na Wageni..."Wao kuwa Wageni Nchini mwao". Aliendelea na kuimba kuhusu kuchukua na Kunyang'anya vilivyo vyao kwa Jina la Yesu!.....Nkajiuliza Kunyang'anya(kutumia nguvu) si ni Dhambi?!! Halafu nikakumbuka Ubunge ni Career Path kwa watu Mashuhuri ila issue nzima inayonifanya niandike hapa ni ile ya kuji-contradict!! Isitoshe kuwa Mlokole kwa Miaka zaidi ya 20 lazma utarudi nyuma (utachoka) kumsubiri Yetu (hihihihi my ribs... Wapendwa na Watumishi habari gani?) na hivyo kuhama Kanisa, Kuanzisha Kanisa Lako au kujiingiza kwenye mambo mengine ambayo ni tofauti na Misimamo yako. Si walokole tu wanaoji-contradict kwa kukataa "Mikorosho" lakini wakati huohuo Kumuita Yesu ni Mume wa Wajane (Wajane sio Wanawake tu kama ulikuwa hujui, kuna Wajane wanaume) kwa mfano tu!! Kujikanganya ni kitu cha kawaida ailimradi

Kizazi cha Santuri, Kaseti CD Vs MP3...

Nimekatiza mahali mtaa wa ki-Posh nikakutana na "Bei Nanini CafE" haraka haraka akilini ikaja "Price and what's not"....not exactly what they meant ni mimi tu na Utamu wa Kiswahili.....liwache hili! Unakumbuka enzi zako ulipokuwa unakuwa miaka ya 92+ hapo ndio Tv zinaanza kuchanganya(sio Vituo) bali watu kumiliki Tv(wageni wa Jioni wakapungua nyumbani kwetu). Kila ulichokuwa ukifanya Mzazi wako anakukatalia akisema "enzi zetu tulikuwa hivi na vile....sio nyie watoto wa siku hizi"! Halafu unatamani kumuambia "sasa Mama enzi zako si zimeisha, hizi zetu" lakini huwezi, unaishia kununa. Nakumbuka Baba(Marehemu) alikuwa anasema "hivi huko Madukani hakuna nguo za wakubwa, zote ni za watoto tu?" Akimaanisha zinabana au fupi!....tukamwambia "Baba hii ndio mitindo ya kileo".....alisema "vaeni mtakavyo lakini mkija Ofinisi kwangu sitaki kuona chupi ndefu" (Suruali za Kubana).

Kizazi cha Miaka ya 90!

Na haraka zao!! Yaani wapo mbio-mbio tu japo mbio zao zinatofautiana.....kuna wale wa starehe(Now) na wa maisha yajayo(Future)!! Mdogo wangu wa Mwisho anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni. Nilipopata habari za yeye Kuposwa nilipata hasira za ajabu! Nikabaki nalalamika "yaani mdogo wangu mdogo hivi anaolewa"...."Vipi huyo mwanaume akienda kumtesa"? "Kwanini asisubiri kidogo jamani akue (huku nalia) bado mdogoooooooo" she's 23yrs! Mama akaniuliza(Simuni), ningekupa taarifa kuwa anamimba au kazaa ugelia kiasi gani?!! Kabla sijajibu!! Asali wa Moyo nae akauliza swali hilo hilo(live).....nikasema but she's my little sister....can she just wait another 2yrs?!!! Anyway, ilinichukua mwezi Mzima kukubali kuwa my baby little sister-o anaenda kuolewa!! Sasa leo naongea nae, ananiambia "nipo site dada" Nkauliza Site ya maandalizi ya Ndoa? Akanijibu "Hapana Da Dinah, tunajenga"!!

Nimeachwa na Teknolojia...

Ah! Nimebanwa kweli siku mbili hizi....ila nafurahi kuwa nimepata muda wa kuongea na wewe kabla sijaenda kulala.....mmh! Tangu nimekuwa Mama wala hakuna kulala ni kujilaza tu. Kuna tuwimbo tuwili twa Ali Kiba tunanikuna kweli yaani "Mwana Daslama" na "Kimaso" ingekuwa zile Kanda za enzi ninge-rewind kwa Penseli mpaka Kanda ikatike....ujue kuna Wasanii wa Bongo Flava halafu kuna Ali Kiba(I just love that Kid). Achana na hili. Jana nikaenda Dukani kuangalia Simu....Teknolojia imenishinda au niseme tu imenipita! Simu yangu ya mwisho ilikuwa (usicheke) Blackberry Bold 9900, ikatumbukia chooni (umama siku za mwanzo uliniCost!!!). Siku naenda mtembeza mwanangu City center kwa mara ya kwanza si nilipanda Treni heheheheheeeeeeee mwanamke nashuka na "Pram" lenye Mwanangu obviously!!....nikaacha Hand bag kwenye Treni(walinirudishia though)! Turudi kwenye Teknolojia ya Simu, wala siamini kama nimekaa Miaka 3 bila

Mtu chake...

Kwa kawaida mimi sina tabia ya kuangalia watu ninapokuwa natembea na hata kama nimekaa mahali nitakuangalia kama nimependa ulichovaa....na kuangalia kwenyewe ni kwa Sekunde chache tu. Kuna watu wanajua kukodolea macho wenzao bila kupepesa! Yaani anakukazia macho mpaka unaona aibu kwa ajili yake! Ukitaka ugomvi na watoto wa London wale wa Uswahilini bana wakazie Macho hivyo....anakufuata na kukuuliza "what you looking at?" huku kashikilia Kisu! Kisu bit pale juu nimeongezea tu chumvi, ila kuna vipigo na vifo kadhaa vilitokea kutokana na mtu kumkodolea macho mwenzie. Stori time: Sasa jana tupo mtaani tunatembea na watoto....nyie mnatoka Weekend sie twatoka J'tatu....kisa na sababu? Ili tusiwe sawa, hakuna lingine wacha kutuJAJI eeh! Nasikia Asali wa Moyo analalamika "mijaume ya kiafrika sijui ikoje (yeye mwenye Muafrika) inamkodolea macho mke wa mtu wakati inaona kabisa yupo na Mtu wake" Hee! Nka

The why's!

Nilijua siku nikizaa mmoja kati ya wanangu (au wote) watakuwa waongeaji sana kama errr Mimi?!! Well, najua kuwa napenda kuongea (labda kwa vile sinywi pombe au sina nguvu ya kupigana) lakini sio muongeaji kihiiivyo. Nakumbuka Marehemu Baba alikuwa anawaambia watu "aah kuwa makini, binti yangu huyu anamaneno sana". Kiukweli kabisa na admit mimi ni Mbishi sana....nope! wala sina asili na watu wa Kibondo, Kigoma! Labda kwa vile sina Nguvu za kupigana lakini wakati huohuo sipendi kuonewa, sipendi kudanganywa na siamni katika "kubali yaishe" BS na wala sio "ndio bwana"....sasa nikiwa na uhakika na ninachokisema nitakubishia mpaka kesho muda kama huu. Turudi kwenye uongeaji ambapo ndipo Babuu(my 1st born) anapokuja sasa....Laaaa! Mwanangu anaongea jamaniiiii....akianza stori zake....halafu ana "why's" za kutosha. Maana nilikuwa nahofia Hisabati akianza shule, sasa nina shughuli ya kujibu wh

Mama wa Nyumbani...

Kwa mwaka mmoja na nusu (au tuseme miwili maana nilianza likizo ya Uzazi nikiwa na Mimba ya Miezi 5) nimekuwa Mama wa Nyumbani. Mie kuwa Mama wa nyumbani ilikuwa choice kutokana na moja ya Misimamo yangu ya kimaisha ambayo wengi hushindwa kunielewa....kwamba miaka 3 ya mwanzo ya wanangu ni lazima niifaidi (as in kuona wanavyobadilika kila siku, kuwafunza manners n.k kabla hawajaanza shule rasmi). Pia ile hali ya mimi kutoamini mtu mwingine kuangalia wanangu, nahisi kuwa hawatawapa huduma, upendo na attention inavyotakiwa, na wao hawataniambia kwani bado wadogo. Hiyo ilikuja baada ya kujifungua mtoto wa Pili, yule wa kwanza bado nilikuwa na ile "lazima nirudi kazini, am financially independent working Mum" hivyo Babuu akawa Day care akiwa bado mchanga. Back to Mama wa kunyumba! Heeeeeeee! Nawaheshimu wote, kazi yenu ni ngumu, Kuzaa is nothing compared to Mama wa Nyumbani na anashatili malipo ya juu ambayo ni zaidi ya £60,000 kwa mwaka....well sio wote bali wale ambao hawana

Maghorofa-2

Siku nimekatiza mahali nkasikia sauti ya Kike kwa Lafudhi ya Kipemba "Bwana Dullah wee panda basi mwenzio nipo hoi".....nkajisemea eh watu na shughuli zao asubuhi-asubuhi. Wacha mawazo machafu! Bwana Dulla alikuwa Chini ya Ghorofa akitaka Bibie amfuate kwani aogopa panda Lift-ini peke yake! Sasa Glasgow-Scotigo kama nilivyogusia jana ni Jiji (lililozubaa) lakini linamajengo Marefu mengi kuliko Majiji mengine ndani ya UK. Pamoja na sifa hiyo wataalam wanadai hayakujengwa vema na mbaya zaidi yana reputation mbaya ya "Komando Yoso" Vijana wakorofi na familia mbazo ni masikini(wanaotegemea Benefit). Wananchi wakaanza kuzikimbia nyumba za Maghorofani na kukimbia maeneo ambayo kuna majengo hayo Marefu kwa kuhofia "status" zao na kuibiwa au kuuwawa. Baada ya Muda Serikali(almashauri ya Jiji husika) wakaamua kuyabomoa yale ambayo waliona ni ghali sana kuyatengeneza na Mengine kuyagawa(kuyauza) kwa Mashirika

Majengo marefu(Maghorofa)!

Kuna yale yaliyojengwa kati ya Miaka ya 40s na 70s ( I guess) Ilala, na yale pale kati ya Mnazi Mmoja na Stesheni, Posta, Kariakoo, Tandika, Keko, Upanga, Ostabei. Halafu kuna yale ya Miaka ya 80-90 maeneo ya Tabata, Mbezi Beach.....tulia, nazungumzia Maghorofa ya NHC na ya Kampuni kubwa kama vile TTCL, PPF na kadhalika sio yake binafsi. Ninayoyataka hapa ni yale ya 40s-70s, ambayo hayakujengwa katika mfumo mzuri wa Maji safi na Maji taka, Nyaya za umeme zimekaa kihatari-hatari na Juu ya Ghorofa ya Mwisho kuna uwazi kwa ajili ya eer "kupunga hewa" " kufurahia the view"?!!! in which kwa nchi yenye watu wenye ma-stress na ma-depression kama UK ingekuwa rahisi kujipoteza (kujirusha ili kufa).....mbona tungewa-sue NHC mpaka wangekoma. Pamoja na hasi hizo bado majengo yale yana sifa ya kujengwa kwa kutumia Malighafi Imara ukilinganisha na Maghorofa yanayojengwa Karne hii. Magorofa hayo yakikarabatiwa mmmh itakuwa gharama kuu na pengine kulipuliwa na yaanza kuanguka labd

Reality Tv Shows....

Haiyaaaaa (Waswahili wa huku ndio wanasalimiana hivyo)....Wakishua wanasema how do yo do.....asa nani anamuda wa "hau-du-yu-du Maisha haya?!! Unakumbuka enzi Reality shoo zinaanza kulikuwa na slogan ya "Movies are boring, Reality is exciting"....well not exactly ila ili-sound hivyo bana eh! Basi bana si Ndio akina Kadarshian* wakaanza na mimi nikiwa mmoja wa watazamaji wa mwanzo kabisa nikiamini kuwa nilichokuwa nakiona ni uhalisia wa Maisha yao....kwa miaka miwili.....mai miaka Miwili naangalia scripted "reality" Tv shoo (nalia hapa kwa aibu). Basi bwana, nikaacha kuangalia na kuchukia Reality Tv shoo zote ikiwemo Big Brother! Sasa nilipomimbika 2012 nilianza Likizo ya Uzazi nikiwa na Mimba ya Miezi 5.....unataka kujua kwanini? Hehehehehe aiii nilikuwa "rough" sana na kazi yangu inahitaji u-smart bana, nkaona mmh ntakosa Maternity Leave hapa, mwanamke wacha nikimbie mapemaa(natania). 2012 ndio nikaanza tena

Kupenda kusifiwa....

Ah! Kama wewe ni mzuri wa jambo fulani hakika utakuwa unajijua hivyo sio mbaya kujisifia mwenyewe.....au subiri Mpaka urudishe namba (ufariki) ndio watu wakusifie kwa Mema na hata kwa yale mabaya yako. Mmh! Lamini ukifariki unakuwa umemaliza ya Duniani, sasa sifa za Walimwengu uliowaacha zitakusaidia nini? Kungekuwa na uhakika wa Sifa hizo kukupunguzia Madhambi uliyofanya au Ukali wa Moto siku ya Kihama, ingekuwa Poa! Sasa, kuna Watu wameumbwa kuzitafuta Sifa kwa nguvu.....yaani mtu anatengwa, anafanyiwa maovu na mabaya yote lakini yeye yumo tu kujionyesha Mwema kwa hao Walimwengu.....wacha kujipendekeza, fanya yako....hutakiwi na huna umuhimu kwao! Unawajua wale Jamaa wanafanyiwa mabaya, wanaharibiwa familia zao au Mradi ambao ulikuwa Tegemeo kiuchumi....Jamaa waharibifu wakirudi na kuomba Msamaha wanasamehewa na Ujamaa unarudi upya. Mie siwezi bana, ukinitenda ama nalipiza Kisasi kwa Jamii yako Nzima au nakufuta akilini (nachukulia kuwa

Kuwekana...

Heloooooooo there! Mie huwa sishangai mtu akimchomekeza Jamaa yake (binamu, mtoto wa ba' mdogo).....nilishakuambia Ndugu ni wale mnaochangia Damu kwa Baba na Mama vinginevyo nyie ni jamaa tu! Hii haina "Dinah kakaa sana Ulaya kabadilika"....tangu Mdogo mie huwa siwachukulii Jamaa kuwa Ndugu! Ndugu zangu ni wale tuliotoka Tumbo Moja au Baba na Mama Mmoja.....kama hutaki kukubali bana shauri yako! Mambo ya kulazimisha Undugu bana ni kumaskishana (kutiana umasikini) na kuongezeana ma-stress tu.....hii ndio huwakosesha watu "bahati" ya kufanikiwa. Bana mie ningekuwa sijui nani ni nani Serikalini halafu kuna nafasi za kazi zinapatikana unadhani nitakuajiri wewe wakati nina Mpwa wangu (Jamaa) anaelimu na ujuzi ka' wako nyumbani? Aiii nitampa nafasi yeye kwanza, akiikataa ndio wewe wa Nje utafikiriwa. Najua sheria za kazi na kadhalika BUT Mpwa wangu sio Ndugu yangu, hatu-shei damu wala Ubini sasa undugu unatoka w