Skip to main content

Namba ya Simu imekuwa too personal....

Heyaaa!

Unawajua wale watu wanagawa namba yako ya Simu kwa watu wengine bila idhini yako.

Tangu enzi mie nachukulia namba yangu ya simu ambayo haihusiani na "Kazi" ni personal na hakuna mtu anapaswa kuwa nayo isipokuwa wale ambao nadhani ni muhimu maishani mwangu kama sio leo basi huko baadae.

Sasa kutokana na Maendeleo ya Kitekinolojia Simu si ndio zimezidi kuwa PERSONAL kuliko namba? Halafu unashangaa kwanini watu wanaweka Passwords au PIN ku access simu zao.

Nilipopata simu yangu Mpya (kumbuka nimekuwa nyuma na  Teknolojia ya  Simu kwa Miaka 3.5)....so niliponunua ze latest simu si ndio ikanishtua.

Ile mambo ya urahisi wa kupokea na kutuma Emails mdio ikanitisha kabsaaa. Nime add Email address nikaletewa the whole thing.....kumbuka sijagusa emails via desktop kwa miaka sasa nilipoona mafolda yaliyokontaini barua za wapita njia na some picha zao dated back in 1999 to 2005 si nikapata Mini heart attack! Nikabonyeza futa daima milele.

Zaidi ya hizo kuna zile unasubiri mtu akuchokoze halafu jmkumbushie kwa ushahidi wa Email iihihihihihi cant wait. Hizi jimeziacha kwenye sever ya Yahoo.

Hakuna mtu anataka mapasti yake yaonwe na watu Kazini au mahali popote utakapoisahau Simu yako. Pia sio vema watu wajue kama jana wewe na mumeo mligombana via whassap.

So yeah hata mimi Mpinga PIN na Password ku access simu nimebadili Msimamo.......ila siziamini Pin na Password hivyo naingia simuni mwangu kwa alama za Vidole.

Babai

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao