...just incase? Mie binafsi siwapendi Rafiki zake wote...well sio wote, wapo ninaowapenda ila Asali wa Moyo hayupo karibu nao so nimebaki na nisio wapenda which means siwapendi WOTE!! anyway...
Siku nkaenda shiriki Semina ya Wanandoa Wachanga(mie mepita Miaka Saba so nilienda kama Mzoefu). Dunia ya leo watu wanadanganyana sana aisee. Mke wa Pastor aliedumu kwenye Ndoa kwa Miaka 28, akawa anashauri Wanawake walio Ndoani ambao hawana "uzoefu".
Mengi yalisemwa ila lililonigusa ni hili la LAZIMA na MUHIMU sana kuwa karibu na Rafiki wa Mumeo, just incase siku moja mkikorofishana na wewe ukashindwa kuongea moja kwa moja na Mumeo. Kwamba unaenda kwa Rafiki yake/zake na kuwaomba wamfikishie ujumbe....au "Ongea na mwenzio, maana mimi hanielewi" Kweli Mama Pasta? kweli kabisaa??
Huyu ni Mume wangu(najisema kimyomoyo Seminani), tulipokula Kiapo ilikuwa kati yake Yeye, Mimi na Mungu na tuna-share kila kitu(isipokuwa Miswaki na DNA?) ikiwa kuna issue kati yetu Mama Pasta tunaiweka Issue Mezani, tunazungumza na kufikia muafaka wenyewe na Mungu wetu. Ndoa ni ya Watatu Mama Pasta, Mungu, Mume na Mke, ikitushinda tunaipeleka kwa alietufungisha ndoa, akishindwa(which is rare) basi tunarudi Nyumbani kwa Wazazi.....huko nako ikitokea Sufuri basi tutajaribu Kansela ambae ni Mtaalam na hatujui sote(hatopendelea)....duh! mpaka tufike huko Ndoa itakuwa imekwisha uwawa...mie Mwenyewe Mshauri hihihihihihi!
Hakuna Uhusiano usio yumba, sema miyumbisho inatofautiana. Jambo kubwa kwenye Ndoa yetu huenda ni dogo sana kwenye Ndoa ya Watu wengine. Mfano mie sipendi kutukanwa au kudharauliwa, sasa siku Asali wa Moyo akinitukana au kuonyesha dharau huo utakuwa Mwanzo wa Mwisho wa Ndoa yetu! hii haina Kansela wala Mfungisha ndoa....Kuvumilia? vumilia wewe....mie sijui kuvumilia matusi wala dharau.
Ninachojaribu kusema hapa ni kuwa, huitaji na sio lazima kurafikiana na Rafiki wa Mumeo/Mkeo ili tu iwe rahisi ikitokea mmepishana/kosana/gombana na mwenzio. Kama ilivyo kwenye Mapenzi, Urafiki/Ukaribu na Mtu haulazimishwi....ni ku-click au unclick!
Kwa wewe ambae hukufundwa na Bibi/Shangazi yako labda (Kama Somo la Sayansikimu, sio muhimu ila inasaidia sana Maishani) na unategemea/amini zaidi Wake wa Mapasta/Wachungaji wakushauri kutokana na "umri mkubwa" wa Ndoa zao. Tambua kuwa Umri wa Ndoa sio kielelezo cha Ndoa Imara yenye Furaha, Upendo na Amani. Wengi hubaki kwenye Ndoa kwa sababu nyingine nyingi tu ambazo hazihusiani na Maana wala Lengo la Ndoa.
Pia kumbuka kuwa Uzoefu wa Mtu sio mara zote muhimu bali Elimu. Kufundwa ilikuwa ni Elimu ya Kijadi ya Awali ya kumuandaa Binti Kimaisha(sio kingono pekee kana wengi wanavyofanya siku hizi) atakapokwenda kuwa Mke na Mama.
Sijui nyie, lakini jinsi mnavyokuwa pamoja kwenye Ndoa ndivyo ambavyo mnajifunza zaidi kuhusu mambo mengi kimaisha kama Pea, vilevile inafikiwa mahali mnajikuta hamuendani tena na "marafiki" zenu wa zamani ambao kila mtu "alikuja nao". Mara nyingi mnaachana na baadhi as you grow older na kutengeneza Marafiki Wapya kama Mke na Mume by the time umefikia utu Uzima mnajikuta na Marafiki wa kweli wa chache na wengi wao ni wale mliotengeneza Pamoja kama Wanandoa.
Sikutumi uwafukuze rafiki wa Mumeo ambao labda (kama mie) huwapendi, bali husihisi presha ya kujenga urafiki nao, ila ni muhimu Mumeo aelewe kuwa Humpendi fulani na fulani ili ikiwezekana apunguze kuwaleta kwenu.....you know some watu wana bad energy, ukiwaona tu energy yako na yake zina-crush(weka Smile Emoji)!!
"Waheshimu Ndugu na Rafiki wa Mumeo, lakini usirafikiane nao"-Marehemu Bibi yangu Binti Z.K.
Waulize Google for me, kwanini hatuna Emojis kwenye Blog via PC ambayo ni Google Product?
Babai.
Siku nkaenda shiriki Semina ya Wanandoa Wachanga(mie mepita Miaka Saba so nilienda kama Mzoefu). Dunia ya leo watu wanadanganyana sana aisee. Mke wa Pastor aliedumu kwenye Ndoa kwa Miaka 28, akawa anashauri Wanawake walio Ndoani ambao hawana "uzoefu".
Mengi yalisemwa ila lililonigusa ni hili la LAZIMA na MUHIMU sana kuwa karibu na Rafiki wa Mumeo, just incase siku moja mkikorofishana na wewe ukashindwa kuongea moja kwa moja na Mumeo. Kwamba unaenda kwa Rafiki yake/zake na kuwaomba wamfikishie ujumbe....au "Ongea na mwenzio, maana mimi hanielewi" Kweli Mama Pasta? kweli kabisaa??
Huyu ni Mume wangu(najisema kimyomoyo Seminani), tulipokula Kiapo ilikuwa kati yake Yeye, Mimi na Mungu na tuna-share kila kitu(isipokuwa Miswaki na DNA?) ikiwa kuna issue kati yetu Mama Pasta tunaiweka Issue Mezani, tunazungumza na kufikia muafaka wenyewe na Mungu wetu. Ndoa ni ya Watatu Mama Pasta, Mungu, Mume na Mke, ikitushinda tunaipeleka kwa alietufungisha ndoa, akishindwa(which is rare) basi tunarudi Nyumbani kwa Wazazi.....huko nako ikitokea Sufuri basi tutajaribu Kansela ambae ni Mtaalam na hatujui sote(hatopendelea)....duh! mpaka tufike huko Ndoa itakuwa imekwisha uwawa...mie Mwenyewe Mshauri hihihihihihi!
Hakuna Uhusiano usio yumba, sema miyumbisho inatofautiana. Jambo kubwa kwenye Ndoa yetu huenda ni dogo sana kwenye Ndoa ya Watu wengine. Mfano mie sipendi kutukanwa au kudharauliwa, sasa siku Asali wa Moyo akinitukana au kuonyesha dharau huo utakuwa Mwanzo wa Mwisho wa Ndoa yetu! hii haina Kansela wala Mfungisha ndoa....Kuvumilia? vumilia wewe....mie sijui kuvumilia matusi wala dharau.
Ninachojaribu kusema hapa ni kuwa, huitaji na sio lazima kurafikiana na Rafiki wa Mumeo/Mkeo ili tu iwe rahisi ikitokea mmepishana/kosana/gombana na mwenzio. Kama ilivyo kwenye Mapenzi, Urafiki/Ukaribu na Mtu haulazimishwi....ni ku-click au unclick!
Kwa wewe ambae hukufundwa na Bibi/Shangazi yako labda (Kama Somo la Sayansikimu, sio muhimu ila inasaidia sana Maishani) na unategemea/amini zaidi Wake wa Mapasta/Wachungaji wakushauri kutokana na "umri mkubwa" wa Ndoa zao. Tambua kuwa Umri wa Ndoa sio kielelezo cha Ndoa Imara yenye Furaha, Upendo na Amani. Wengi hubaki kwenye Ndoa kwa sababu nyingine nyingi tu ambazo hazihusiani na Maana wala Lengo la Ndoa.
Pia kumbuka kuwa Uzoefu wa Mtu sio mara zote muhimu bali Elimu. Kufundwa ilikuwa ni Elimu ya Kijadi ya Awali ya kumuandaa Binti Kimaisha(sio kingono pekee kana wengi wanavyofanya siku hizi) atakapokwenda kuwa Mke na Mama.
Sijui nyie, lakini jinsi mnavyokuwa pamoja kwenye Ndoa ndivyo ambavyo mnajifunza zaidi kuhusu mambo mengi kimaisha kama Pea, vilevile inafikiwa mahali mnajikuta hamuendani tena na "marafiki" zenu wa zamani ambao kila mtu "alikuja nao". Mara nyingi mnaachana na baadhi as you grow older na kutengeneza Marafiki Wapya kama Mke na Mume by the time umefikia utu Uzima mnajikuta na Marafiki wa kweli wa chache na wengi wao ni wale mliotengeneza Pamoja kama Wanandoa.
Sikutumi uwafukuze rafiki wa Mumeo ambao labda (kama mie) huwapendi, bali husihisi presha ya kujenga urafiki nao, ila ni muhimu Mumeo aelewe kuwa Humpendi fulani na fulani ili ikiwezekana apunguze kuwaleta kwenu.....you know some watu wana bad energy, ukiwaona tu energy yako na yake zina-crush(weka Smile Emoji)!!
"Waheshimu Ndugu na Rafiki wa Mumeo, lakini usirafikiane nao"-Marehemu Bibi yangu Binti Z.K.
Waulize Google for me, kwanini hatuna Emojis kwenye Blog via PC ambayo ni Google Product?
Babai.
Comments