Skip to main content

Faida za Kumnunia Mwenza wako....

...Habariyo?


Wanawake tunajulikana kuwa tunapenda  sana kununa-nuna si eti? Lakini hata Wanaume pia hununa, ila wao huwa hawaiti "kununa" bali "nataka kuwa peke yangu ili nifikirie" au pengine anaweza kukuambia hajisikiii vizuri au anamawazo.


Sote tumetofautiana, jambo dogo kwako linaweza kuwa kubwa sana kwangu, hali kadhalika kauli yako ambayo wewe unadhani ni ya kawaida inaweza kuwa Tusi kuu kwa mwenzio na hata kuhatarisha Ndoa/Uhusiano wenu. Inategemea na Malezi/Makuzi, Mazingira, Uzoefu n.k.



Wakati mwingine Kununa is all you need! Biga Mnuno kwa Siku 5(ukizidisha Mkeo/Mumeo ataku-cheat hihihihihi siku ya 6 kidate na ya Saba one night stand....Hisabati Muhimu).....the rule(Bibi yangu alisema), nuna  Maximum Siku Tano tu ukizidisha huna Mume/Mke!



Kununa huko hupunguza ukaribu kati yenu kama Mke na Mume, unapokea majibu kwa mkato, ukiingia tu ndani, mmoja anahisi usingizi  ghafla hihihihihi....pia hukupa hisia ya "nampenda" lakini sipendezwi nae...ananiuDhiiii( ndio love___ but don't like___?)....Kizungu sijui, Kiswahili sijui....nipo nipo tu sijui kama naenda au narudi....anyway!



Kununa kwako huwa hakuna faida(Machoni mwao) lakini huwa kuna sababu ya Msingi tu kwanini hasa Mkeo/Mumeo kakununia. Unajua unapokuwa kwenye "Ngazi" ya Urafiki na mapenzi ni rahisi kupata nafasi ya "kufikiria" Tusi au kosa/kwazo alilokufanyia Rafikio wa Kiume/Kike....so hata ukinuna utakuwa kwenu na yeye Kwao.



Lakini unapokuwa kwenye Ndoa na Mnaishi kwenye "Kanyumba"....Nafasi hiyo hupotea, huwezi kuikimbia Nyumba yako kila mara ambapo Mumeo/Mkeo wako anakuudhi! Mbaya zaidi ikiwa wewe kama Mie hapa, unaishi Ughaibuni....hakuna "kwenu" kule alipo Mama yako ambako ungeweza kwenda na kupumzika kidogo ili kufikiria mpaka Hasira ziishe(Uache kununa) hivyo unaishia kupishana na Mwenza wako bila Jambo wa Habari.



Kwa kawaida, Mnapopishana Maneno na kupelekea Mabishano  na labda mmoja wenu hatoi nafasi ya mwingine kujieleza, ili kukunyamazisha....anatupia "tusi" na Maneno mabaya ambayo pengine yataumiza Hisia zako.....Maumivu hayo hukufanya uamini kuwa Mumeo/Mkeo atagundua kuwa amekukwaza/kosea na hivyo atakuomba Msamaha.




Siku inakaribia kuisha na hakuna Msamaha wala Dalili yake.....kinachofuta hapo ni "Kula Bati"....yaani unamnunia....akiwahi kulala wewe una-stay late watching Tv, aki-stay late wewe unaenda kusoma Kitabu. Hakuna kula pamoja wala kupika(kwa Mwanamke kupika ni sehemu ya kupendezwa na mwenza, kama hakupendezi kwa maudhi yake kwanini Umpikie eti?) kwa Wanaume huja na chakula chao au hula Nje(kwanini ale chakula chako wakati hujamuomba msamaha).



Sasa kuna watu wameumbwa kusoma wenza wao na kugundua kuwa wamekosea mahali, wengine huuliza "nimekukosea nini Mpenzi, mbona unaonekana haupo sawa" na wengine huwa hawana habari mpaka uwaambie makosa yako(kama vile wewe ni Mzazi kwao). Wengi hasa Wanaume hawajui au niseme Wazito kuomba Msamaha? au Wanaomba Msamaha kwa vitendo?


Haombi msamaha mpaka umwambie amekukosea wapi, which inaondoa uzito wa Msamaha wake.....kwasababu Msamaha mzuri ni ule unaotoka kumoyo bila kulazimishwa au kuambiwa sio ndio?!!



Nukta ya Post hii ni hivii.....unapomnunia mwenzio kwasababu amekuudhi sio Utoto na wala sio Ujinga. Ni sehemu muhimu kwako ili kuweza kutuliza Akili na Hisia zako zilizoumia  na kufikiria Kosa(kauli yake chafu iliyo kukwanza) na hivyo kuwakilisha issue Mezani tena katika hali ya Upole lakini Firm.


Fundisha Mwanao umuhimu wa Kuomba radhi/Msamaha, na ikiwa wewe Mzazi umemkosea mwanao usisite kumuomba msamaha, kwani "tufanyayo kwa Vitendo ndio hufanywa/igwa  na Watoto wetu"-Christian Bwaya.


Shukurani kwa Muda wako hapa ambao nauthamini pia Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Baibai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao