Skip to main content

"Dayaspora" na Kuzikwa "Nyumbani"...

Mtu aliehamia Nchi nyingine kwa Kupenda(uamuzi wake binafsi) nae ni "Diaspora" au ni  "Migrant" au yote mawili kwa pamoja? kwasababu tunatumia neno "dayaspora" wacha niende nalo ili kurahisi mambo.


Wewe umeishi zaidi ya miaka 10 nje ya Tanzania, umejenga Marafiki(ndugu) wapya, umeanzisha Familia(ambayo haina uzoefu na Nyumbani kwa Wazazi/Mzazi mmoja) na kuwekeza kwenye "Property(ies)" na Biashara nyingine. 


Lakini ukifariki "watu" wanalazimisha uzikwe kwenu(sio kwako kwenye Familia uliyotengeneza ambako ndiko ulikofia) na Marafiki wa Ukubwani.



Sio tu ni ubinafsi wa Jamii hiyo "nyumbani" bali pia ni kujipa Majukumu na Gharama ambazo sio zao(hata kama wanachangisha) bila kusahau kuwanyima Watoto na Mkeo/Mmeo Haki ya kutembelea Kaburi lako wanapohitaji kufanya hivyo.


Familia yako kutumia Milioni kadhaa kuja "Nyumbani" kila mara wanapotaka kuongea na Mzazi/Mwenza wao ulielala Kaburini ni ghali. Ukiachilia hilo mbali hao wanaolazimisha "ukazikwe kwao"...wakisha zika hawatembelei tena Kaburi lako kwasababu wameisha zoea kutokukuona mara kwa mara kwa sababu ulikuwa anaishi mbali. 



Binafsi sikuwahi kuona umuhimu wa wapi Mfu anatakiwa kuzikwa, mpaka Kaka yangu alipofariki na Ndugu kutaka azikiwe Nyumbani(Baada ya yeye kuishi nje ya Tz kwa miaka 22 ).  Hoja yangu ya "Ni vema azikiwe alikoishi maisha yake ya Ujana karibu na Mkewe na watoto wake" ilipita japo kwa mbinde.



Weka pembeni  suala la kusafirisha Maiti kutoka nchi yeyote ile ni ghali(japo unasafirishwa kama Mzigo), kuna suala la Waombolezaji Kula/Kulala mpaka Mwili wako utakapo wasili na pia kule kwako (ulikofia) kuna Maturubai na waombolezaji pia.


Vilevile kuna Gharama za kutunza Mwili, kuuandaa/tengeneza na nauli za Mke/Mume aliebaki na Watoto.



Ni wawache sana wanaweza kumudu gharama hizo za ghafla lakini kwa upande mwingine(tunza, andaa mwili kwa muda mrefu, nauli, Maturubai na kulisha watu huku na kule) ni kujitakia.


Ifike mahali "Dayaspora" waridhike kuzikwa kwenye Nchi wanazoishi ili kurahisisha ukaribu na Familia zao walizoanzisha na sio zile za Wazazi wao(origin).


Familia yako uliyoitengeneza ina Haki ya kuwa karibu nawe hata katika Ufu(ukiwa Kabirini) mara nyingi iwezavyo bila kufikiria Nauli/Usafiri na Hotels.


Nikukumbushe sehemu ndogo ya Umuhimu wa kufunga Ndoa. Kama mmefunga Ndoa, wewe ndio una Haki na Mamlaka ya kuamua Mwenza wako azikiwe wapi, na sio Wazazi/ndugu zake.


Ikiwa unaishi mwenyewe na hivyo kurudi Nyumbani ni Muhimu(huna Familia Ulaya) hakikisha una Bima ya Afya/Maisha(na Mazishi) kwenye Nchi uishiyo, ili kuwapunguzia Mzigo Wazazi wako "Nyumbani".


Nathamini Muda wako, ahsante.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao