Skip to main content

Wanaume hawajui kunung'unika/kukaa na Kinyongo....


....Sosho Midia si imewabadilisha? Hakika bado wapo hivyo ila namna wafanyavyo ni tofauti na walivyokuwa wakifanya kabla ya Sosho Midia(nionavyo mimi).



Unakumbuka ulipokuwa mdogo(au ni mimi tu), Baba yako akisikia jambo kutoka kwa Mwanaume mwenzie halizungumzii ila anakwenda kwa huyo Mtu na kuzichapa/kumkung'uka Magumi? well Baba yangu alikuwa mtu Mwema na Mtu wa watu lakini alikuwa Ngumi Mkononi, anakutandika halafu yanaisha. sasa hii ndio "Wanaume hawakai na Kingongo" niijuayo mie. Niliendelea kuona hiyo  kwa Kaka zangu na rafiki zao pia na hivyo kuweka Sementi kwenye hilo.




Siku hizi Waanaume, wanaanika mambo ya wenzao nje (mitandaoni)ikiwa wamekorofishana, kwamba mmoja akiudhiwa/kasirishwa na mwenzie basi Jamaa wa Shosho Midia wote watajua. Kwa sisi Wanawake ambao hufikiria baada ya action(sio kabla) na kisha kuomba msamaha baada ya kuharibu ni Kawaida(ilizoeleka hivyo), lakini sio kwa Wanaume.




Sio kwamba  nasikitika kuwa Wanaume wamebadilika na wala sisemi wakarushiane Magumi, bali nasema Unapotoa Siri ya Mwenzio  adharani kama sehemu ya "kutokukaa na Kinyongo" haikusaidii in a long run, kwasababu  unajitia aibu wewe mwenyewe na kuondoa Imani/Heshima kutoka kwa watu wengine(sio muhimu lakini can be muhimu huko mbele)na baadhi kukuogopa kwenye Issue zao za kimaendeleo labda....?



Aibu hiyo husambaa kwa Familia yako ikiwa una Mke na Watoto, Mpenzi.....ikiwa Wewe ni single kwa mfano, inakuwa kama vile unakimbiza  potensho Mpenzi. Inawezekana bado unaamini kuwa hizi Sosho Midia ni Apps tu, lakini kumbuka kwa karne hii ni sehemu ya Maisha. Picha zako na short vid zipo kwenye "www", mtu akikuona Mtani au popote "wachumba" wanapopatikana sio ngumu (kama unavyodhania) kutokukutambua/kumbuka upuuzi wako Online.



Mie Binafsi nafanya  karibu kila kitu Online kuanzia manunuzi yangu, na-chat na watu nsiowajua juu ya bidhaa fulani, naweka mihadi na Daktri online, Na-book holiday online, nafanya kazi online,.....so online is "part of life".....huwezi kuendelea kufanya mambo ya kudhalilisha mwenzio (hata kama kakukosea) ukijitetea kuwa ni online so sio that serious!




Mie sio Mama yako so sitokufundisha Manners ambazo Mama yako labda alishindwa au alisahau au pengine Baba hakuwa na Muda na kukuweka sawa namna Wanaume wanamaliza "tofauti" zao. Ila nitakuambia kuwa, ni vema na ni Uanaume(whatever Uanaume is).....kumuita aliekukosea na kuzungumzia Issue iliyokukwaza na kuyamaliza pmbeni.




Ikiwa aliekukosea ni wa Online, kwa kawaida kila Sosho Midia ina mahali faragha, basi na muitane huko yaishe. Huu sio ushauri bali ni maoni yangu kuhusu sehemu ya  tabia za Wanaume tulizozizoea kubadilika kutokana na ukuaji wa Maisha ya Online.


Nathamini, muda wako hapa na ahsante kwa kuichagua blog hii.

Babai

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao