Skip to main content

Nini Mbadala wa kuomba radhi kwa Mwenza?


Kawaida sisi Wanawake huwa tunanuna pale tunapokoseawa tukitegemea kuwa Jamaa anakereka kwa kuchuniwa na hivyo ama kukuuliza tatizo ni nini ili umpe Risala au straight up agundue kosa alilokufanyia na akuombe Msamaha.



Wengine hawajali hata ukiwanunia, wanachukulia ni "mambo ya Wanawake" na Baada ya Muda utakuwa "fine". Wengine hata ukiwaambia kuwa umehisi kuwa amekukosea/umiza hisia zako na hivyo ni vema akuombe radhi bado ataendelea kujitetea, matokeo yake Ugomvi unaibuka. Sasa unakabiliana vipi na Mwenza kama huyu?



Kama nilivyogusia kwenye Post iliyopita hapa Malezi ya Mwenza wako yanahusika zaidi kwenye suala la kukubali Kosa na kuomba radhi. Baadhi ya Wanawake wapo hivyo pia lakini tofauti ni kuwa baadhi yetu huwa tunapewa Elimu ya Awali ya Maisha ya Ndoa hivyo hata kama Mama na Baba walijisahau au hawakujali kutupa malezi mema bado tutajifunza Ukubwani ili kuwa tayari kuishi na Mtu Baki(Mume).



Makosa ninayoyazungumzia hapa ni yale madogo-madogo na yanasameheka. Sizungumzii Usaliti wa Uhusiano(which sio kosa ni Ushetani bin Dhambi)....Usaliti hausameheki unless wewe mwenzangu ni Yesu/Mungu!!



Kabla hujaanza kumlaumu hajakuomba msamaha, anza kuchunguza Matendo yake kwako tangu mpishane/gombane. pamoja na kuwa umemnunia/chunia je amefanya nini ndani/nje ya nyumba? Mara nyingi utaona anasafisha vyombo, au anapika....inawezekana akafanya Usafi, kaamka mapema na kuwapa watoto kifungua kinywa? kakununulia kijizawadi na kukiweka mahali bila kukusemasha? Mkilala anakukumbatia(halafu wewe unamsukumia mbali), ana-over-sifia Chakula ulichopika ambacho huwa unapika mara 3 kwa Wiki n.k.



Ikiwa hajafanya lolote kama nilivyotaja hapo juu basi ujue kuwa haamini/hajui kuwa alichokisema kwako kimekuumiza hisia na unastahili Radhi yake. Kitu cha kwanza kabisa kufanya ikiwa Mwenza wako sio "kuomba Msamaha" kind of a person, ni wewe kuwa Mfano(kama Mzazi kwa Mtoto). Irudishe Issue mezani na uizungumzie tena.


Omba msamaha kwa kumchunia kwa siku kadhaa, ni kwasababu ya Maumivu aliyokusababishia. Ulimnunia ili kufikisha ujumbe kuwa amekukosea na hivyo akuombe Msamaha(ambao hukuupata), mwambie kuwa kama watu Wazima ni Muhimu sana kuwa Mfano kwa Watoto(kama mnao) kwa kugundua Kosa, kukubali Kosa na kuomba Radhi na kurudisha Uhusiano kwenye hali nzuri ili kuishi kwa Amani na Upendo.


Hakika hatokuambia Nisamehe Mke wangu....akijitahidi sana "atasema nimekuelewa basi yaishe", sio kwamba hataki kukuomba Msamaha isipokuwa hawezi na hajui aanzaje kusema "samahani" ni neno ndogo lakini linauzito mkubwa na ndio maana kwa baadhi ya watu huwa ni gumu kulitoa/sema.


Wanaume wengi (hasa wa Kwetu Barani Afrika)huamini kuwa Kuomba Msamaha ni kama vile kujishusha kwa Mwanamke. anaona bora afanye hivyo kwa vitendo kuliko kutamka neno hilo.


Siku nyingine akikukosea, mueleze hapo kwa hapo na hakikisha ni ana kwa ana. Usifoke na wala usionyeshe Hasira....mwambie ulichokifanya/sema kimeniudhi na kuniumiza hisia zangu, ikiwa kama nimekuumiza wakati nakuelezea naomba unisamehe. Endelea hivyo kila mnapopishana na atajifunza umuhimu wa Kuomba radhi.


Njia nyingne na kumfunza Mwenza wako kuomba Msamaha ni kuwatumia Watoto wakati Baba yao yupo around, wakikoseana waambie waombane Msamaha, wakikukosea waambie wakuombe Msamaha, wakimkosea baba yao watume wakaombe Msamaha/Radhi. Kila mara unawaambia watoto waombe Msamaha/Radhi, waeleze umuhimu wake Maishani, hasa maisha ya ukubwani. Itachukua muda lakini atakugua Umuhimu wa kuomba radhi.


Post ijayo nitagusia Mbadala wa kusema "Nakupenda"....Usikose. nathamini na kueshimu Muda wako hapa, Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao