Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2014

Uelewa na kumbukumbu ya Mtoto.

Nilipotobolewa Masikio nilikuwa na Miezi Sita (kwa Mujibu wa Mama), alienitoboa ni Mama wa Kimasai na aliekuwa kanibeba/shika ni Bibi yake Mama. Sikumbuki maumivu, lakini nakumbuka nililia sana nilipomuona Mama wa Kimasai na Shanga zake na Masikio yakiwa marefu "kwenda chini". Siku niliyomsimulia Mama kuhusu hiyo siku ya tukio (nilikuwa teen na bado naikumbuka)...alinishangaa na kusema kuwa lazima nilisikia akisimulia watu, mtoto wa miezi Sita hawezi kukumbuka. Nilipokuwa na miaka 3 au zaidi, tulikuwa Mjini Mbeya....Mama, Mimi, Mjomba na watu wengine tulikuwa tunapita pembezoni mwa Mto. Mjomba wangu alinibeba na kutishia kunirusha kwenye Maji(Mto)....Nadhani ndio maana naogopa Maji....Safari zangu ni za Anga, Reli na Barabara, mie Meli sijui Boti sipandi....Mtumbwi? Bora uniue. The point is, Mtoto anauwezo wa kutunza kumbukumbu kuanzia umri mdogo sana kuliko tunavyoaminishwa na "Mzungu" the Shenzi. Sio unafanya mambo u

Kaja for a reason....

Wacha kujipa Moyo.....hakuna mtu anajiijia tu maishani mwako isipokuwa wewe unaruhusu awe/aingie Maishani mwako. Ukisema umefanya maamuzi mabaya ya kuruhusu huyo particular mtu maishani mwako nitakuelewa. Kumbuka wewe ndio responsible kwa kila kinachotokea maishani mwako iwe ni maamuzi mazuri au mabaya.....beba mzigo na ujipange upya, sio kujipa-jipa moyo...eti sababu Mzungu anakuaminisha kuwa "people come in your life for a reason". Kuna watu wanaishi ili kuharibu maisha ya watu, ndio furaha yao. Wengine walikosa mapenzi na malezi bora kutoka kwa Wazazi/Walezi matokeo yake wanayatafuta waliyoyakosa kwa kuharibu maisha ya wenzao.....nakadhalika. Sasa ni juu yako kumsoma yeyote anaekuja maishani mwako na kumruhusu aingine kama Rafiki, Mpenzi, Jamaa ( wale mliooa/olewa Ukoo Mmoja), ukigundua tu kuwa umekosea basi haraka muepuke kabla hajaharibu zaidi. Nikupe mfano?....I looooooooooove mifano hihihihihi(watu tunauelewa tofauti, bila mifano wengine tunatoka kapa). Unaishi maisha

Mali ya Familia...

Kuna baadhi yetu tunatabia/kasumba ya kuita Mali za watu kuwa zetu na pengine kuanzisha fujo na kupelekea Vita kubwa ili kila mmoja apate "mgao" wake. Kwasababu tu Mali ni za Baba/Mama yako au Kaka/Dada yako haikupi haki ya wewe kupata Mgao....wacha papara za kutaka kunijibu, nitakupa mfano ili unielewe vema. Baba na Mama wameachana wakiwa hawana kitu, Baba kaanzisha uhusiano mwingine na kupata familia "mpya"....mambo yakaenda vema wakawa na Mali za kutosha....wewe uliezaliwa na Mama wa kwanza unadhani una unahaki na Mgao sawa kama watoto waliomo kwenye "familia Mpya"? Upatikanaji wa Mali za Baba yako na familia yake Mpya unamchango Mkubwa wa Mama yao (familia Mpya) na sio Mama yako (alieachana na Baba yako akiwa hana kitu)....sehemu ya mali utakayoipata ni ndogo sana, tena kama Mke atakubali upatiwe. Mf; wa kwanza. Mf wa Pili: Dada/Kaka kajipinda na kujituma yeye na Mume/Mkewe na sasa wanamiliki Mali nzito, inakuaje wakubwa/wadogo watu mhesabu kuwa hizo

Weusi mzuri...

If you have to tell us then it isn't....Mambo vipi? Weusi wa Afrika tuna issues zetu ambazo zinasababishwa na Watawala wetu(Siasa)....ila Weusi wa Wamarekani wana issues vichwani mwao kuhusu Weusi wao, yaani wapo ka' Mikorosho vile. Ujue kunatofauti ya kujivunia ulivyo na kulazimisha watu wajue kuwa unajivunia ulivyo. Mf: Kuna ulazima gani wa kusema "mimi ni mweusi na ninajivunia" wakati tunakuona wewe ni mweusi, unajipenda, unapendeza na unafanya mambo yako kama watu wengine. Kwanini utulazimishe kutambua kuwa "unajivunia"? Mf wa pili; Kitu gani kinakufanya uweke "kichwa cha habari" cha video/picha na kusema "beautiful black baby"....kwani ukiandika "baby" au "beautiful baby" haileti maana au hakuna watoto weusi na wazuri isipokuwa huyo wako? Unatulazimisha kutambua kuwa unajivunia Weusi wako alright, lakini picha/video "unazipausha" ili zionekane na karan

Kumbukumbu...

Nimekaa hapa nakumbuka watu wote niliosoma nao Msingi na Sekondari kwa Majina yao yote Mawili(la mwanzo na la Mwisho).....nimeambulia kusisinzia. Darasa Moja tulikuwa. Wanafunzi 200na! Tuligawanywa katika Mikondo 5 yaani A-B-C-D-E-F....shule kubwa ka' Kijiji....hiyo Msingi. Sekondari hatukuwa wengi sana Mikondo ilikuwa Minne. Sasa mwanamke nkasema ngoja nipime uwezo wa akili yangu sehemu ya kutunza kumbukumbu....nimefeli yaani nimepoteza kumbukumbu hata Miaka 40 sijafika!. Nikajipa Moyo; labda niagize picha za enzi za shule ili nikiona sura zao niwakumbuke vema, lakini hata hivyo sikupiga picha na kila mtu niliesoma nae kwahiyo haitosaidia. Yaani ndio basi tena. Nimejisikia vibaya sana....yaani kupoteza kumbukumbu ya sehemu ya Maisha yako ndio inauma hivi?!!! Kama ulisoma na mimi na unanikumbuka eeh! Drop me a line. Babai... Mapendo tele kwako...

Msingi/Malezi bora...

Habari gani? Kuna watu walikosa Malezi(Msingi) bora utotoni, malezi bora sio kula vizuri, kuvaa vizuri na kusoma shule nzuri bali kulelewa katika Mazingira ya Heshima na Adabu (kwako na kwa watu wengine), Staa/Stara, Uvumilivu, Kuridhika, Kutokata tamaa, Utu na Haiba. Hivi majuzi nimekutana na mtu akaanza nipa stori za mambo na vitu Ghali anayomfanyia Ex wake....nadhani alitaka kufikisha ujumbe kuwa yeye ni mtu wa kujali sana na kutumia Mahela kwakwe sio tatizo. Kwa bahati mbaya alikuwa hajui kuwa mimi ni Mwanamke (a bit tofauti) sibabaiki na Mahela ya watu kwani naamini ninauwezo wa kutafuta na kupata zangu.....pamoja na kusema hivyo zawadi napokea hihihihihi! Stori zikaendelea huku nami (kama kawaida) nikiuliza maswali...."Kwanini unamhudumia Ex wakati una mwanamke mpya?"...."Kuna kitu unataka au unapata kutoka kwa Ex"..."Je, Ex ana siri zako nzito unaogopa atazitoa"? n.m(na mengineyo). Kabla hatujaagana chi

Phd...

Naitaka sana yaani, sitaki kuzeeka bila kuipata....shughuli inakuja ni lini hasa nitarudi "shule"? Baada ya kupiga mahisabati nadhani by the time nagonga Miaka 50 Mwenye enzi Mungu akibariki mwanangu wa Pili (mwisho) atakuwa kwenye Teen kati hivi na huo ndio utakuwa muda mzuri. Nia sio kupanda Cheo au kugombea Uwaziri(Ubunge) la hasha! Ni kutimiza Malengo niliyojiwekea kuwa kabla sijazeeka niwe na kaelimu katika levo ya "Udaktari" Dk Dinah blablabla. Sasa angalau mie nilisomaga (si ndio nkachelewa kuzaa!Nilitaka kula life kabla ya Majukumu).....Mambo ya kutoka Binti wa_____ to Mke na Mama wa_____ in my early 20s haikunivutia....Ningeishi Mimi kama mimi lini sasa eti?!!! Anyway, kwa wale "baadhi" walioamua kuanza na Mke na Mama wa_____ hu kurudi "shule" baada ya watoto kukua which ni kitu kizuri ila unakuwa "hujayafaidi" maisha ya Usichanani....ule uhuru wa kutokuwa na Majukumu au kufikiria watoto na Mum

Pale Mwenza aongea kwa Code na rafiki zake....

Alafu mkifika nyumbani anaku-de-code-a yote....hapo sasa ama utadanganywa kabisa au utapewa robo ya ukweli(utadanganywa kwa robo tatu). Unajua upokwenda kutembelea watu mnaofahamiana au unapokuwa kwenye shughuli kwa kawaida inayojumuisha watu mbalimbali baadhi yetu tunaofahamiana/juana sana huongea kwa "Code" au unavutwa pembeni kisha unaambiwa jambo au kuombwa Msaada. Nia na madhumuni ni ili watu wengine wasielewe, wanasahau kuwa watu tunaupeo tofauti, baadhi "tunadikodi" hapo hapo......wengine ndio mpaka wasubiri "wadikodiwe" na Wenza wao watakapofika nyumbani. Natumai unaendelea vema, mimi leo bana sijielewi-elewi, yaani ka' nimepigwa au nimefanya kazi ngumu sana ningekuwa kwetu(KissWay) ningesema "nililimishwa" Usiku wa kuamkia leo. Heri ya Wiki Mpya! Babai. Mapendo tele kwako...

Ugumu wa Masomo...

Hisabati....Hisabati....Hisabati! Sikufanya Mtihani wa Mwisho kwasababu nilijua nitapata LieFu.....sikulitaka Li-F kwenye Cheti changu. Nikapiga Mahesabu ya namna ya kuepuka F kwenye Cheti changu cha Fom Foo....nikapata jibu deshi-deshi, ila mie nilitaka Deshi moja tu so siku ya Mtihani sikutokea.....nikajipatia Mathematics-!! Nilifurahiiiiiii. Nazipenda Hesabu (kuhesabu hela na Pea za viatu tu) ila kama somo hapana, sio kwamba nilikuwa siziwezi la hasha! Nilikumbuka Kanuni zote, nilifuata na kupatia njia ili kupata jibu. Tatizo lilikuja Muda napoteza muda mwingi kuhakiki jawabu matokeo yake najikuta nimefanya Maswali 5 out of 25=Efu...SIPENDI Somo la Hisabati sababu speed ya akili yangu ni a bit slow. Hakuna kitu kinachoniudhi kama kuishiwa Muda wakati wa Mtihani......Baba (Merehemu) alikuwa ananiambia "ukitaka akili yako iwe "sharp" na kuongeza uwezo wa ku-focus kwenye hesabu, fanya Mzoezi ya Hesabu mahali ambapo kuna k

Michezo ya Utotoni 90s

Jambo! Msita (Mdako), Dama, Marede, "Amina sasa naomba, turudiane...hayo yamekwisha kipenzi changu" yaani kuruka Kamba....don't you miss them au wewe ulikuwa wa Kishua unashinda kubebelea ma VHS ya akina Comando Kipensi....?? Usiseme ulikuwa unacheza Game, enzi hizo Bongo hakukuwa na Games za Tv achilia mbali PCs....Tv zenyewe zimechanganya 1994. Nilikuwa mzuri sana kwenye Marede na Mdako(Msita kwa wale wa pande za Shinyanga na Mwanza). Nikikamata Jiwe kwenye Mdako sikosei....kwenye Marede kila Timu ilinitaka mimi (niligombaniwa). Marede ya kujaza Chupa kwa mchanga niliipenda lakini sikuruhusiwa kuicheza kwasababu ya vumbi(Nilikuwa na Pumu). Ila nilikuwa naibia....kisha narudi ndani nimebanwa....kupumua siwezi....jicho limetoka ka' Ndula(unazijua Ndula weyeeeee)....hehehe. Naishia kuonewa huruma na kupewa na kupewa ile Inhaler, kisha nakuwa nimerudishiwa Uhai.....Nashukuru Imeisha (sijabanwa Tangu nilipofikisha miaka 21).

Heshima kwa Maiti...

Imepotelea wapi? Au ndio kwenda na Wakati? Juzi kati nimekutana na Picha ya Maiti ya Mpendwa wangu....pamoja na familia kufanya kazi ya ziada kuzuia upigaji Picha wa shughuli nzima ya Mazishi achilia mbali Mwili wa Marehemu wa mpendwa wetu zaidi ya alieajiriwa kwa ajili ya kazi hiyo....bado kuna jitu likapiga picha na ku-share online. Kwasababu hana Uhai tena haina maana kapoteza Haki zake kama Mwanadamu mpaka atakapozikwa(Fukiwa). Maiti ingeweza ingejisitiri na kupozi ili apendeza au kutokea vizuri zaidi....pia angechagua ni Picha gani itumike kutangaza Tukio lilipolekea Mauti kumfika. Unapata faida gani ku-publish au ku-share picha ya Maiti?.....kwanini unataka tumkumbuke Marehemu kama Maiti na sio alivyokuwa Hai na mwenye furaha?!! Unaweza kusema naegemea kwa Waingislishi kwa vile naishi huku na wao hawana utaratibu wa kuonyesha Maiti au kuiaga zaidi ya Jeneza na Picha ya Marehemu alipokuwa hai....nia ni kubaki na kumbukumbu ya yeye

Radio za Dini

Hiyaaaaa! Umewahi kuzungumzia Sheria za Dini ya Kiislam dhidi ya Wanawake kwa Binti wa "kisasa" wa Kiislamu ukasikia anavyojitetea!....Hadi huruma. Kuna siku mmoja aliniambia Uislamu hauna budi kubadilika baadhi ya Sheria na kwenda na wakati.....sizungumzii wale Waislamu wa Mwezi wa Ramadhani to Ramadhani....la hasha! Nazungumzia wale Mabinti ambao wanaipenda na kuifuata Imani yako kwa Dhati lakini wanahisi kuna mambo kwenye Sheria ya Dini yao zinawakandamiza. Nimekuwa nasikiliza sana Radio za "Kiislam" (za Kikristo miyeyusho,kazi kuomba Michango tu).....napendezwa sana na Mafundisho yao ya Maisha, kitu pekee kinachonikwaza ni pale wanapozungumzia Wanawake....Mwanamke kwenye Imani ya Kiislam bana....daaah!(Naachia hapa). Radio za Kikristo nazo zimejaa Ushuhuda wa kipuuzi tu yaani....alafu wanaomba Michango kuliko kufundisha wasikilizake wake namna ya kuishi Kikristo.....Maombi ya Michango ya pesa 90%....Shuhuda 7% na 3

Kuchapia...

Ni Sunna....Relax! Enyi Wakaguzi wa Lugha Fasihi sijui Fasaha Mtandaoni mnahitaji kwenda kunywa dawa zenu....(Lazima mna some sort of Mental Disorder). Ailimradi unaelewa kinachozungumziwa au kilichokusudiwa unapaswa kurekebisha kichwani mwako kisha endelea na mambo mengine... Wengine tunachapa/ongea haraka na muda wa kuanza kuhariri hatuna....Mimi binafsi ni Bingwa wa kuchapia....mara nyingi nikisoma (kesho yake) nagundua kuwa nimechapia lakini bado naeleweka. Huwa nachapia hata nikiongea na watu japo sio sana, labda maneno mawili kwa siku....aiiii hebu ngoja kwanza....sasa nina watoto which means naongea zaidi....usikute nachapia zaidi ya maneno 10 kwa siku! Haulipii kusoma na alieandika halipii Kodi kuandika....tulia na furahia uwepo wako Online. Kumcheka mtu kwa vile nimekosea/chapia is bullying/Trolling.....hihihihihi! Happy new Week! Babai... Mapendo tele kwako...