Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2014

Umewahi ombwa Mchango wa Birthday?

Huu ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa heshima wa Vipato vya watu....hii kwa Michango yote isipokuwa Ada ya Shule. Kama humudu kulisha watu kwenye sherehe ya kuadhimisha siku yako ya kuzaliwa si uachane na issue nzima ya Sherehe!! Kujitegemea Kiuchumi kumegawanyika katika makundi mbali mbali ujue...(sina uhakika, najaribu kulazimisha tu hapa hihihihihi).....! Kuna baadhi ya watu ambao huishi kutegemea wenzao ili kufanikisha mambo au jambo kwa faida zao Binafsi......wandugu jitegemeeni kiuchumi EBO!!! Mchango wa Harusi: Wakati harusi(Bikira) yenyewe wewe na mtarajiwa wako hamna hiyo HARUSI. Kama hamuwezi kulisha wageni wenu kwa kutumia vipato venu basi fungeni Ndoa mkiwa peke yenu wawili na mashahidi....eti? Siiiiiiimple + no stress. Birthday Party: hii sinimeisha isema kule juu? Eeeh kuna hii hapa chini: Michango ya Baby Shower: Kwa kawaida ukialikwa unaenda na Zawadi inayomhusu Mtoto mtarajiwa si ndio? Sasa hii biashara

Religious vs Believe in God

Nilikuambia nipo Michezoni Glasgow-Scotigo, basi bwana si nkakutana na jamaa wakaniuliza kama mimi ni Religious, nkasema hapana ila naamini Mungu.....acha washtuke!!! Udini unatutenga, Udini unasababisha watu wasifanye mambo kwa uhuru, Udini hukosesha watu wake/waume wema n.k. Hivi unajua kuwa Dini zililetwa na Wageni ambao sasa ama hawazifuati au wameamua kubadilisha waliotuaminisha kuwa "yaliandikwa" na nani sijui nani. Halafu Waafrika tunaanza kuwaona namna gani vipi hawa jamaa wanatubadilishia Maneno ya kwenye Vitabu vyetu vitakatifu ili kuendana na "maisha" ya sasa! Ama kweli Dunia imefikia mwisho. Tunajipa Moyo na kushikilia Imani zetu tukiamini kuwa ni za kweli na kuponda hao Wageni (Wamagharibi na Waarabu waliotuletea hizo Dini) kuwa ni Wafuasi wa Shetwani. Baada ya wao kuchoshwa na Imani mbili tangu Miaka 2000 iliyopita wengi wao wakaamua ama kuachana nazo au kuanzisha nyingine ili ku-suit maisha yao ya Nyakati hizi. Sasa wewe unapoteza Muda wako wote kuja

Review Undugu wako...

Familia/koo nyingi huwa kuna mtu ambae karibu wote wanaMshuku....wanamuona hatari....kutokana na mambo yake Kiuchumi kuwa safi na kila anachosema basi ni "sheria" au hupewa "umuhimu" au "umakini" hata kama alichosema ni upuuzi! Yaani watu kwenye Familia\Ukoo husika hawaishi kwenda kwa huyo mtu, watoto wake, Mke/Mume wake wote wanapewa attention tofauti na akina nyie Hohehahe. Mtu huyu na Familia yake hufurahia yote hayo na huwa on the look out kuona nani anakuja speed ili kuwa kama yeye au kumpita Kiuchumi....basi akigundua atafanya kila alijualo kuzuia Ndugu (tumbo moja) au Jamaa(ndugu wa mbali wale wa kuunganisha mjomba, binamu etc) asifanikiwe. Umewahi kumpa Ndugu yako wa hivyo idea ya Biashara au Mradi halafu akakukatisha tamaa kisha yeye anaifanya hiyo Biashara au ule mradi ambao alikuambia kuwa huwezi kufanikiwa ukiufanya, kwamba utapoteza pesa tu??.....hihihiihi sasa amka na review Undugu wenu! Mtu

Glasgow 2014....

Siku ya Pili ya Mashindano ya Jumuiya ya Madola, nipo eneo la Tukio kwa Wiki 2....interested?....me neither! Kama umewahi kufanya kazi au kutembelea Jiji la London au NY au hata Dar(City Centres sio Keko sijui Masaki huko, nazungumzia "kiini")....ukija Glasgow bana.....ka' sio Jiji, yaani hakujachamgamka kiviiiiiile(ka' Jiji)..... Ila kuna kama "fun fair" kwa kids(sijui wanaitaje bana), nadhani hiki ndicho kitakachonileta huku mara kwa mara. Michezo imeingiliwa na watu kutoka "Makabatini" bwana, wamefanya watu tushindwe ku-concentrate na Mashindano.....yaani "ukorosho" wao una distract kimtindo....maana wengine tulikuwa tunapenda Mbio na Kuogelea....kuangalia "zile maumbile" za Wakaka pale kati na Miguu (au ni mimi tu nakua pervert wa Kike....hihihihi). Siku hizi bana mtu unajisikia vibaya hata kuangalia mchezaji, akili kama inahamia kwenye akifanyacho private! Kwani lazima watuambie wao wana

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Chuki....

Ni sehemu ya Ubinaadamu si eti! Kama unaweza kupenda basi ujue unaweza kuchukia pia....zote ni hisia! Mie bana ukiniudhi kwa kiwango cha kutosha na ukijaribu kuingilia Maisha yangu binafsi nakuchukia wewe, Familia yako, Ukoo wako, Jamii yako, Kabila lako na Nchi yako kwa Ujumla. Yaani watu wanaotoka huko unakotoka wewe wote wanakuwa Maadui, yaani siwaPENDIIIIII mf ni Wanajeria.....Mungu anisamehe ila daa! Nawachukia balaa.....wengine ni wale Majirani zetu waliozima ka' umeme wa Tanesco (what does it mean) ambao hatutaniani na Kiswahili kwao ni sawa na kuwa Malaya the Nigerian of East Africa....BOY I HATE THEM. Alafu kuna Wazimb hihihihihihi nikupe stori? Ni washenzi.....hapa hapatoshi kwa stori, maana ninazo nyingi. Huyo mimi, halafu kuna wewe (sio wewe bali yule)....ambae unamchukia tu mtu wakati wala humjui, hujawahi kukutana nae na wala hajawahi kujihusisha na lolote linalokuhusu! Unaanza Vita!.....aah! Kuna jamaa namkumbuka alikuwa namuandama mwenzie kwa chuki ya wazi kabisa ha

Nipo mtaani kwako, upo home?...

Sipendi hii tabia kwa Moyo Mkunjufu kabisa!!! Nilikuwa namkimbia rafiki yangu Mghana kwa tabia hii....niambie basi siku moja kabla hujaja kuwa unapanga kuja kwangu....sio unafika Mtaani kwangu au pengine Mlangoni halafu ndio unaniambia kwa Simu! Sio peke yake, hata ndugu (wa mbali) na jamaa wanatabia hiyo....kuna siku (nikiwa bado Nyumbani) nilimrudisha mtu kwao on next flight....the next Bus bana, hela ya next flight mie ninayo?!!....nikaambiwa nina Roho Mbaya. Katoka huko Mwanza sijui wapi eti kaja kutafuta Kazi, asa kwanini usituambie mapema tujiandae na Bajeti!....anyway achana na hilo. Mie huwa sifanyi jambo ambalo najua sipendi kufanyiwa, tatizo linakuja pale Mwenza wako sasa anatabia hiyo....hehehehe Baba Babuu Asali wa Moyo wangu bana anaudhi kweli!!! Mnaweza mkawa safarini mara akakumbuka fulani anakaa karibu na hapo mnapopumzika labda....ananyanyua simu "eh bwana fulani! Upo nyumbani?....tupo hapa karibu kama vipi tuje kuwasa

Make up artists....

Ukiingia kwenye Department stores au Boots (Duka la Dawa na Vipodozi) kubwa kwa sie wa Ulaya hii hapa....unakutana na MUA kwenye "viOSK" vyao wenyewe wamejiremba wamependeza....er kwa mbali! Asa sinilikuambia tangu nigonge miaka 30....sasa ni 30na nimeanza "kuipenda" ngozi yangu ya usoni! "Mambo ya mwanamke reception".....sasa kama mtu hukujaaliwa "reception" nzuri au kurembeka(mimi) basi angalau Ngozi iwe nzuri na yenye afya kuwapotezea watu "focus". Mwanamke nimejaribu bidhaa kibawoo za kufanya Uso wangu uwe laini na wenye rangi moja....maana...mmh! Sijawahi kutumia Mkorogo (na sina mpango huo), sina tatizo na Chunusi (mpaka nile Chocolate), yaani ngozi yangu inakaribia ukawaida tu japo inatoa mafuta ya kutosha kukaangia Vitumbua....anyway! Nimejaribu skin care nilizokuwa nikitumia miaka ya nyuma in my late 20s, sasa zinadunda, kitu cha uso ama kimekomaa au kimekuwa Sungu (Kisayansi ngozi hupoteza n

Kabla hujafa, hujaumbika!

Ni kawaida ya watu (wengi) kucheka matatizo ya wenzao au kuyazungumzia katika mtindo wa "kichekesho". Mimi napenda sana kucheka na kuchekesha (japo kuwa sichekeshi....yaani nikitoa kichekesho watu hawacheki mpaka nielezee kwanini nilichosema kinachekesha)....hihihihi achana na hili! Matatizo nayogusia hapa ni yale ambayo mtu hana uwezo wa kuyazuia, sio matatizo ya kujitakia(kuchagua) kama vile Utumiaji wa Madawa (japokuwa hata hawa mie huwa siwacheki). Kama huna utu na huna mpango wa kumsaidia mwenye matatizo kwanini uzungumzie matatizo yake kwa watu wengine katika hali ya "kumcheka"? Wengine wanapoleta habari za mtu za kusikitisha kutokana na matatizo yake yaliyobadilisha Mwili au Akili (Ulemavu) yake hawacheki kwa kukenua Meno, lakini jinsi wanavyoelezea unagundua kabisa wanamcheka mhusika. Mf; "Eh bwana unamkumbuka Elia? Daah jamaa yaani kaisha halafu sasa anatembelea Mgongo. Yule jamaa alikuwa anajifanya mjanja sana"....umeona? Hakenui meno laki

Kuvaa Wig!

Nimekugaya eti?!! Well kwani tulisaini mkataba wa mimi kuwepo hapa kila siku? Hihihihi usiache kusoma bana, hebu baki hapa upate stori ya Wig. Ujue kuna siku akili inachoka alafu kunakuwa kama "empty" hivi kichwani kwa ndani, yaani hata yasiyo na maana nayo huondoka basi inakuwa ngumu kidogo kuandika ili ueleweke. Ikifikia mahali unaandika (huku unasoma bila shaka) lakini unahisi hakileti maana....basi tambua kuwa unahitaji Mapumziko kiakili! Anyway.... Wanangu na Baba yao wamelala....Joto limewachosha, maana leo ka' tupo Kisarawe.....achana na hilo. Nimekaa hapa nikakumbuka Wig langu la kujinyonga wenyewe mnaita Curl sijui Karikiti. Kwa kawaida mie sio mvaaji wa hayo mavitu, ila baada ya "issue" ya nywele nkasema ngoja nami niwekeze kwenye "Afro Wig". Siku (2.5yrs ago) nkalivaa, baada ya kutoka Kazini nkaenda Chekechea kumchukua Babuu ....hee! Mtoto wacha alie alafu anaangalia juu (lilipo Wig) hehehehe....nikazuga bana mbele ya Wazungu as walijua nim

Mama yangu alikuwa Kimada!

Uishie hapo hapo!! Najua umekuja mbio hasa kama wewe ni Kimada aka Mwizi au mtoto wa Kimada. Mama yangu alikua Mke wa haki na sote tumezaliwa Ndoani.....alikuwa* kwasababu Baba ni Marehemu, huko Ahera sijui kaoa tena? Roho itaniuma sana nikijua kaoa tena. Anyway. Kuna wale watoto wa Vimada ambao huja na mijisababu kibao ili kutetea Mama zao Vimada au Baba zao Malaya....wengine wanakuja na "Wake wanajibana wakati Vimada wanajiachia miili yao"....wengine wanajifanya wamefanya "Utafiti" na kugundua kuwa Vimada wanajua Mapenzi kuliko wake n.k. Hakuna ku-justfy hapa, kama wewe ni mtoto wa Kimada utabaki kuwa hivyo!! Tena ngoja nikolezee Mama yako ni kamwizi na baba yako ni kamalaya....tuliache hilo kwanza. Hivi unajisikiaje kwa mfano Umeolewa/Umeoa mtoto wa Kimada, yaani Mama mkwe wako ni "mwizi" wa mume wa mtu na huyo Mume(Baba mkwe) ni Malaya.....hihihihihi mie nisingekuwa comfortable yaani ningekuwa nawakwepa m

Kupotea Suna!

Mara ya kwanza kumiliki "SmartPhone" ndio ikawa mwisho wa Mimi kupotea(in my head)....leo 2014 na Tech yote ya Ramani na Gadgets zote zilizopo za "Directions" bado napotea.....Hapo ndio Suna inakuja sasa(sina sababu nyingine). Kwa kawaida nikipotea huwa sioni aibu kumuuliza mtu au kuomba anielekeze....tofauti yangu na wewe ni hivi; huwa sisimamisha mtu yeyote tu, nategea wale ambao sio attractive (at least machoni mwangu). Kwanini nachagua unattractive watu(Wake kwa Waume)? Hata sijui....ila nahisi kama wao ndio wanatoa maelezo vizuri kuliko wale "attractive"....wanakuelekeza utadhani unawatongoza(mie mwanamke, mke na mama nikutongozee nini wee fala...). Naweza nikaenda mwendo mrefu kutoka sehemu niliyopotea mpaka nikutane na unattractive person ndio nimuombe "directions". Nishakuwa stereotyped sana, hivyo wala siogopi kustiriotaipu watu.....ndio maisha...heri umejua kuliko ningekudanganya. Si eti?

Macho yane...

Jana si nilikuambia "nalikizoka" sehemu- sehemu ya Ulaya?....nkaenda kwenye Shopping Centre yao kubwa na wanangu wawili! (Siku zote huwa napita kwa nje tu). Simlituambia wa Ulaya hatuwezi "kulikizoka" Tanzania, sababu tukija huko sio Likizo tena bali tumerudi nyumbani, ni ukweli kabisa (sijui hili limekujaje hapa, tuliache)! Basi humo ndani (shopping centre) Macho yangu yamesifiwa na watu kibawoooo....hee! Mwanamke nikashanga....(Najua nina tumajicho tuzuri ila sio kiviiiiile)! Mkaka mmoja akashindwa kujizua akaniuliza "where are you from"? Nkamwambia "England" hihihihiihi nkaona NOMA! nkasema Tanzania, East Afrika, I have 2 kids and a husband....akasema "are all grown women look like you?....Fit, Nice skin and beautiful eyes?" Nkasema Yes! (Nimeitangaza Tanzania hapo) England hawayaonagi Macho yangu au dharau tu washenzi kabisa wale, mmmh! Ila inawezekana ni u-busy wa Maisha. Watu hawana habari, akili yote ina-focus kwenye £ ili kulipa

Siri...

Unawajua wale akina "nilificha/nilifanya SIRI kwasababu nilikuwa nalinda hisia zako"....."Kwasababu sikutaka kukuumiza" mifano ya watu the shenzi kind of people? Halafu sasa umejua! maumivu ni zaidi kuliko ungejua siku aliyoifanya hiyo siri....well in my case, reaction yangu ni ileile ufiche siri kwa miaka 10 au uniambie masaa machache yaliyopita....AM GONE!! Siri uliyofichwa kwa Miezi/Miaka huuma zaidi kuliko kuambiwa moja kwa moja! The thing is kuendelea kuishi na mtu huyo ni sawa na kuishi maisha ya "Uongo". Usikute hapa nafichwa mambo kibao alafu kimbelembele na-blog hihihihihi, siku nikijua hata kama nimefikisha miaka 50, sisamehi aisee...hii ni karne ya 21 sio Enzi za Yesu!! Aah. Kuna mambo ya kifamilia hupaswi kumueleza mwenza wako unless unajua kabisa yatamu-affect yeye na watoto. Vinginevyo yaache huko huko "familiani". Sasa hizo sio Siri ninazozungumzia hapa, maana hazikuhusu! Si

Karibu, jisikie upo Nyumbani....

Utawekewa "Maeneji" mabaya nyumbani kwako na maukarimu yako yaliyopitiliza yasioyojua mipaka, shauri yako! Unawajua wale wageni wanakuja kwako alafu wanaaza Ziara rasmi ya Chumba hadi Chumba, Droo hadi Droo, wanajipulizia Manukato yako na kujaribishia Viatu na Nguo zako.....WANANIUDHI sana. Wazungu wao huona sifa au sijui ni Kacha yao! Hata sielewi, kama ni mara ya kwanza kufika kwake atakupa Ziara ya nyumba yote mpaka Stoo kwa hiari yao....(Tuwaache). Ujue hapa Duniani bana kila mtu anamikosi yake, shida, raha na tabu zake. Hujui kapita wapi kutegemeana na "Imani" yake ili kujaribu kuiondoa Mikosi (kila mtu na siri yake bana). Siku unamkabidhi Nyumba yako unaanza kuona mambo hayawi mambo. ....usikute "eneji" yangu nzuri kwangu mimi na familia yangu, sasa ukinikabidhi nyumba yako nijisikie ka' kwangu alafu "eneji" yako mbaya ikai-triger "eneji" yangu nzuri na kuzalisha "sumu" yakawa mambo sio mambo usilalamike....Mfano tu