Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2014

Celebs

Hii jamii ina power ya ku-normalize kila kitu, hata vile ambavyo ni normal lakini jamii nyingine hawavifanyi, wao hu-normalize. Mfano ni "attachment parenting" ambapo mama analala na mtoto wake na kumnyonyesha for as long as possible. Hiyo "attachment parenting" si ni kitu cha kawaida kwenye jamii ya Kitanzania(na Afrika kwa ujulma)....nimezaa mwanangu wa kwanza nikapigwa marufuku kulala nae ili kuepusha cot death. Nikakumbuka Mama alipozaa wadogo zangu 3 wa mwisho, wote alikuwa analala nao kitanda kimoja na hakuna aliepoteza maisha.... Aii....nikawa na lala na mwanangu ka' ifuatavyo na amenyonya mpaka mwaka na miezi 3. Siku hizi analala chumbani kwake lakini akiota ndoto mbaya anakimbilia kwetu so tunalala wote wanne. Huyu wa pili bado analala na sisi na bado ananyonya (mwaka na miezi 3) tena huyu ni king'ang'anizi kuliko kaka yake ambae hakujali kulala peke yake au kulala na sisi.. Kingine ni Kuzaa kwa kupasu

Uswahili Mzigo...

Halo, haloooo....Halo ya Mbuzi meeeeee! Kuna tofauti kati ya Uswahili way of life which ni kitu cha kujivunia, ni kama "culture"....alafu kuna Uswahili "ile hali ya kutokuwa Mstaarabu" na Uswahili simply kwavile wewe ni mwafrika(Muafirika). Wenzetu wa Kishua hawapendi Uswahili kabisa yaani! Wao wanaishi Kizungu zaidi....usiniulize kwanini wengi wao wakifika Uzunguni (Ulaya, Marekani, Down Under etc) wanakuwa Waswahili kupita wale Waswahili wa Mtaani kwetu pale KissWay(Kisarawe). "Unaedha" dhani kuwa wamebadilika, hapana hawajabadilika bali kuishi "Kizungu" Ulaya inabidi uwe Posh....U-posh waenda sambamba na Pochi(mahela).....sasa inawezekana kabisa tuhela twako + rangi yako, Elimu na ulikotoka inakuwa ngumu kidogo kuishi "kizungu" kwa Wazungu.....sijui umenielewa?!!! Sasa unaishia kuishi na Waswahili wenzako "wa Kizungu" ambao awali hukujua tofauti yao kati ya Middle class, Working class, Chav n.k Kama tunavyojitenga Tanzania

Baba zetu nao...

Wiki Mpya oyee! Nimeacha kujivunia Tanzania kama Taifa(Kisiasa) miaka kadhaa iliyopita, najivunia Tanzania kama Nchi na baadhi ya Tamaduni zake, kama vile kuvaa Vibwaya (vile vifupi, kuachia tumbo na kufunika Matiti), Ngoma na nyingine nzuri nzuri. Kuna unataratibu wa baadhi ya wanaume kudai kuwa mwanamke yeyote atakaelala nae ni Mama yako na mtoto yeyote atakaezaliwa na mwanamke ambae sio Mama yako ni Ndugu yako. Sina uhakika kama ni Utamaduni,Tabia au pure______! Mama yako ni yule aliekuzaa au "kisasa" aliekulea tangu ukiwa na umri wa masaa au siku chache.....sio random women aliolala nao Baba yako. Pia ndugu yako ni yule mliotoka tumbo Moja, wengine ni Jamaa (tena ukiamua kuendeleza ujamaa huo kwani sio lazima). Tabia ya Baba kulazimisha watoto wao kuwaita wanawake wengine Mama au watoto waliozaliwa huko (kabla au baada ya Ndoa) wadogo/kubwa zao sio haki na sio sahihi kwa mtoto/watoto husika. Huyo ni Mkeo na hao ni watoto wako w

Mkorogo...

Habari... Mkorogo ni kutumia bidhaa "illegal" au "home made skin lightening" na "kujiton" ni kutumia bidhaa zilizothibitishwa na Jamaa wa Ubora wa Viwango eti?.....wote nia yao Moja. Waafrika kwa Waafrika kwa ubaguzi wa rangi zetu hatujambo....tofauti ya Ubaguzi wetu sisi Watanzania ni kuwa hatutengani au kuuana kwa sababu baadhi yetu ni weusi sana au weupe sana. Well, isipokuwa kama wewe ni Mweusi tii alafu huna nywele laini na unaishi Somalia au Sudani Kaskazini.....oh au Chotara ndani ya South Africa. Ila Machotara ndio huwa wabaguzi zaidi kwa Weusi kuliko sisi wenyewe kwa wenyewe....Usiombe ukutane na Chotara wa Kizungu aliekubaliwa kwenye jamii ya Kizungu ayeee!! Anyway, nukta hapa ni kuwa tofauti ya weusi wetu wa ngozi ndio hutufanya tuwatanie wenzetu na kuwaita majina....Mf: Cheusi dawa, Mpingo,Cha usiku n.k Huu utani huwafanya baadhi(hasa wanawake) wajisikie wanyonge, hawavutii....inafikia mahali wa

Usinijaji....

....relax is a human nature! Tangu u-single mother umekuwa "fashion" vijana karibu wote wa late 20s na early 30s walishazaa huko nyuma, hivyo ni ngumu kweli kukutana na mtu ambae ni "m-clean" ka' wewe (hana mtoto/watoto). Shughuli inakuja kwa sie tuliozaa(Oa/Olewa) na Wanawake/Wanaume ambao washalizaaga "ujanani" huwa tunajajiwa sana yaani. Unaonekana "Mwizi" kwenye jamii na familia, hata mtoto aliezaliwa kabla wewe hujakutana na Baba/Mama yake uhisi kuwa wewe ndio sababu ya Baba/Mama yake kula Buti la pua ( I know how it feels cause I was a kid once). Unaenda mahali na Mumeo/Mkeo na tutoto twenu (bila yule wa kabla) watu wanawasonta-sonta (Shinganya Oyee!! Kusonta ni kukunyooshea kidole kama ulikuwa hujui)....anyway! Wengine bila haya wanaanza kuuliza "nanilihu na Mama/Baba yake hawajambo" mbele yako just to piss you off....Mindugu mingine Mikosi kweli!!? Inafikia mahali unajistuki

Kufananishwa/Linganishwa....

Jambo! "Baba yangu alikuwa bla bla bla kwanini wewe usi bla bla bla kama yeye" kaolewe na Baba'ko sasa (this apply to wakibaba pia, kaoe Mama yako sasa eti).... Kama tulivyozaliwa Nyakati, Siku na Dakika tofauti ndivyo ambavyo tunapaswa kuishi tofauti(na wazazi wetu). Utaishije maisha waliyoishi wazazi wako wakati wewe ni mtu tofauti na unaishi kwenye Nyakati tofauti na wao? Kuna zile "manners" nzuri ambazo ni muhimu maishani na kila familia inapaswa kuwafunza watoto, mfano Kusalimia, Kuomba, Ukarimu, Heshima, Kushukuru, Msamaha.... Kama utafananisha hizo hakunaga mashida, mengine yaliyobaki yaache yabaki huko huko yanako stahili. Ungependa kuwa au kuishi na mtu kama Baba/Mama yako? You need to go out a bit more rafiki.....by out I mean OUT OF YOUR COUNTRY!!! Kwaheri kwa sasa. Mapendo tele kwako...

Kujipendekeza Kipaji....

Helloooooo! Napenda kuandika mambo ambayo watu huogopa kuyasema lakini yanawakera...kwanini? Sababu sinywi Pombe hehehehe...! ....Kwa kawaida Ndugu wa mume hupaswa kuwa karibu na wewe (hata kwa ku-pretend) ili ujisikie umekaribishwa kwenye Ukoo eti...kwa Kacha yetu ya Kitanzania. Mwenyewe unajitahidi kuweka mawasiliano ya karibu....wao walaa(mpaka uwatafute)! Unajipa moyo labda wanashughuli nyingi na muda hawana, unasubiri siku mbili-miezi mitatu still Jiiiii....hee unaanza kujistukia, unataka kumuambia Mumeo lakini unaona noma. Maana wengine hawachelewi kukuambia "unataka kutugombanisha, we mwanamke tu....wale ndugu zangu"....so unaugulia Moyoni. Kujipendekeza mwisho mara 3(in my head), unajaribu kwa Mwaka mzima wao hawajitumi kukutafuta hata XMas to Xmas! Sina marafiki kwa ajili hiyo(sijui kujipendekeza, najaribu....usipoweka effort nafunga Ukurasa na songa mbele..... Unajiuliza nani atanizika "nikikufa

Kazi za watu...

Maoni ya Mhariri...siku hizi sote tunatoa Maoni on particular or similar issues....Teknolojia na Uhuru wa kujieleza/Changia utakacho au ulichokiona/shuhudia unaharibu kazi za watu. Mfano, kazi ya Uandishi wa Habari wa Magazeti na Radio....imeingiliwa na Blogs, Online Radios, Social Media na YouTube(is YouTube sosho Media pia?). Jamaa wanatumia Sosho Midia kama "chanzo cha uhakika" na wale Waandishi wavivu wa kukopi na kupesti ndio wamerahisishiwa kazi. Habari zenye Uzito ni zile za Uchunguzi....labda na mahojiano magumu ya Wanasiasa! Jana nipo YouTube (napenda Fashion Haul na beauty review....how sad!!?) nikakutana na Matangazo kutoka Kampuni moja kubwa ya Urembo....alietumiwa ni Vlogger na sio Model/Celeb kama nilivyozoea. Nkajisemea eeh Teknolojia imeharibu na kazi za Celebs na Model pia.....sio haki kabisa! ....Hebu ngoja kwanza! Hawa Vlogger ni real people wanatumia bidhaa na kuzi-review hivyo wao kutangaza bidhaa husika wana

Diet...

Hiya.... Utaratibu wa kula kwa kila mtu ni Asubuhi, Mchana na Jioni. Baadhi yetu tunaongeza Mlo in between na wengine hatumudu Milo miwili kwa siku. Sijawahi kujinyima ili kupungua au kukonda, nimekuwa chembamba maisha yangu yote ya Usichana mara boom nikafikia size 12(Mimba hizo). Nikajiambia, ah nikijifungua nitakuwa nakwenda Gym ili nirudie kamwili kangu ka enzi....aiii muda si ukagoma kutokea. Nikaamua tu kupiga mazoezi yangu mwenyewe nyumbani. Sikuweza ku-keep up na mazoezi kutokana na Uchovu (mother of two kids under 5 baibeee isn't as easy as Celebs looove to lie on our faces).... Nkapiga mahesabu, mmh am on my 30s nikishangaa hapa nitakuwa na kitambi for life....nifanye nini sasa wajameni? Nikapata jibu...relax Dinah Relax.....wacha Kichanga afikishe miezi 9 (atakuwa anajitegemea...kukaa peke yake na kulala vema usiku) alafu ndio uanze mambo yako. Kusubiri mpaka afikishe miezi 9, mbali alafu sio guarantee atakuwa "a

Nywele zako ni 2a au 4z?

Wenzetu ambao wamezaliwa na Mzazi mmoja Mwenye asili ya "Nywele kunyooka" wanapenda kutupeleka mbio sana sisi wenye kipilipili. Hata kama Bibi yake Bibi wa Baba yake ndio alikuwa "nywele kunyooka" na mweupe bado mtu ana-claim yeye ni asili hiyo which is Okay ila msitupeleke mbio sasa eti! Juzi nimesoma mahali, Binti mmoja anasema anamshukuru Baba yake kwa kutokuoa Mwafrika mwenzie maana angezaliwa mbaya na mwenye nywele mbaya za 4b....anampenda sana mama yake ambae ni Mzungu. Nkakimbilia ku-google ili nijue maana ya hizi namba na herufi "Nyweleni"....well nilitaka kujua namba ya Nywele zangu, aiiii nadhani ni 5z...the higher the number the Mbayest the hair. Tunanyoosha nywele sio kwasababu hatuzipendi tulizozaliwa nazo au tunataka kufanana na nyie bali ni kutaka kuzi-manage kiurahisi... Ni kipilipili cha haja lakini kuna wakati kilikua na kufika katikati ya Mgongo....HAPANA!! am not that short...am 5'4 nadhan

Ugomvi wa Ndugu...

Sie tuliozaliwa wengi (zaidi ya wawili) huwa hatuoni umuhimu wa attention ya wazazi wetu....labda kwavile hatukupewa au tulipokuwa tukihitaji kwa vile kulikuwa na Kichanga. Tuliihsia kuambiwa "acha kudeka" na kofi juu. Na baadhi yetu tuliishia kulea wadogo zetu ambao walihitaji attention zaidi yetu wakati Mama na Baba wako busy na mambo yao mengine kama sio kutengeneza mtoto mwingine. Tunapenda kuwamwagia sifa kutokana na malezi yao mema kwetu na kutangaza ni namna gani tunawapenda na baadhi hudai wazazi wao ni mifano mizuri kwao (good role model)! Wakati mwingine ni kweli ni "good role model" lakini mara nyingi ni Hatia moyoni inakufanya udhani kuwa walikuwa wazazi bora na wanafaa kuigwa....si unajua the "bila wao nisingezaliwa au kusomeshwa" sort of guilt..... Well (1)-Uamuzi wao kukuzaa (hukuomba kuzaliwa) + (2)- ;ukumu lao kuhakikisha unaishi vizuri na unapata Elimu hivyo wacha kuhisi hatia. Kuna mahali w

Pale 40something anaposhindana na 20something....

Kwa hamu nasubiri siku nitakayofikia miaka 40(God willing) ili namie nijisikie kama wanavyojisikia waliogonga hiyo namba. Natumaini Botox itakuwa imeshuka bei by then, maana Viganja kwa nyuma vinamakunyanzi ka' Bibi yangu wa miaka 90. Wengi huamini kuwa miaka 40 ndio Uzee ila nadhani Tz mwanamke akifikisha miaka 30 huitwa Mzee.....Mtukome....Mzee Mama yako (hii imetoka mchicha ka tusi eti?) Well, namaanisha mwanamke aliekuzaa ndio Mzee. Celebs waliofika Umri huo wa miaka 40 hujisifia kuwa wanajisikia kama walivyokuwa kwenye umri wa miaka 20s ila tofauti ni kwamba sasa wanajijua, wanajiamini, wanajua watakacho nakadhalika.... .....well inawezekana kabisa sio kweli ila ni mikakati ya kutaka kuendelea "kuonwa" kijana. Hakuna haja ya kuendelea kufanya uliyoshindwa kuyafanya enzi zako za Yahoo na Hotmail, relax na uwaache watoto wa 20something wafurahie Era yao. Tunafanikiwa sana kuficha au kudanganya Umri lakini sura siku zo

Tunapenda kufanana...

Heri ya Alhamisi.... Katika kupitia Vlogs (nilikuwa nanfanya uchunguzi kuhusu nywele) nikagundua kila chumba au Vanity room (where they film) vinafanana....Nikatafuta ukweli kwanini wote wanafanya hivyo? Nikagundua chanzo ni Kadashianzi. Mara nikakumbuka watu wa kawaida tu kwenye jamii pia hupenda kuigana kuanzia Nyusi, Fashion mpaka mapambo ya nyumba/ndani....Blogs na Sauti (bwahahahaha) Najua kwa baadhi ya watu ni muhimu kufuata "trends" na hivyo kufanya kama wanavyofanya wengine.....kama inakupa furaha maishani why not eti? Dressing table yangu ni ile ya kizamani, kabati upande mmoja, chini na juu droo katikati kioo chenye kijisehemu cha kuweka Manukato, Wanja n.k!...Vanity/Dressing Room? Aii only in Amerika na Kanada (majumba yao makubwa) or Mamilionea wa Bongo na Ulaya.... Tangu nilipokuwa Mdogo nilikuwa sipendi kufanana na watu wengine, si unajua midosho nini na nini....Dar combine...hihihihihi. Ndani kwangu hakuna Picha ukutani k

Changudoa...

Kwa kawaida jamii hushupalia ikiwa mhusika au wahusika ni Wanawake. Tena wanawake wenyewe ndio wanaongoza kuwakandamiza Machangudoa. Katika hali halisi Machagudoa hasa kwenye maisha ya Chuoni ni kitu cha kawaida, haina maana mimi nimewahi kufanya hivyo bali kuna wake kwa waume niliosoma nao walikuwa wakifanya kazi hiyo ili kujimudu. Siungi mkono kazi yao na wala sipingi kwasababu sijui ni circumstances gani(ukitoa tamaa ya high life) zimepelekea wao kufanya uamuzi huo huko Nchi za watu.... Tambua tu kuwa wanaume pia wanafanya Uchangudoa Nchi za nje na sio Wanawake pekee. UK ya leo sio ile ya Tony Blair na kama UK maisha magumu huko kwingine si ndio basi tena (in my head). Kwenda "Majuu" is not as cool as it used to be....ndio maana watoto wa Vigogo siku hizi hawaendi Nje (hawaishi Nje), wanafungua mabiashara makubwa au wanakuwa Wanasiasa..... Uanasiasa na kumiliki Biashara yenye mafanikio is new Cool. Kwaheri kwa sasa.

Uchungu wa Kuzaa + Kujizuia usi-Push = Near Death

Mimba ya mwanangu ya Pili Iman haikuwa enjoyable + alipitiliza. Mkunga kanaipangia siku ya kuwa "induced" ili nipate Uchungu. Binafsi sipendi vitu ambavyo sio asili kwenye mwili wangu na hakika sio Uchungu, pia ni Mpinzani wa kuzaa kwa. C-section. Kwabahati nzuri (Mungu alijibu maombi) Asubuhi ya kuwa induced "chupa" imepasuka, nikawapigia simu wakunga wakasema wanajiandaa kunipokea wakati wowote. Mimi being mimi, nikasema nitavumilia mpaka maumivu yachanganye ili nikifika tu Hospitali nijifungue....maana kwa Barack ushamba/kutokujua tulienda Hospitali mapema....uchungu ukachanganya Saa saba....Lol! Anyway, nikapata uzoefu mpya sasa....kama unadhani Uchungu wa Kuzaa ni kamambe!!....Usiombe Kuumwa uchungu huo + juhudi za kuzuia mtoto asitoke. Mambo yakaenda vizuri, Uchungu unakuja unarudi....ikafika saa Kumi na mbili Jioni, mara booom! Mtoto namhisi huyu hapa....naita baba mtu, kusanya Barack....hao garini. Najisemea &q

Nywele....

Baada ya kujifungua Barack na kupoteza nywele za kutosha, nikavumilia mpaka nilipomaliza kunyonyesha. Niliposhika Mimba ya Iman nikaamua kukata nywele hivyo nimekuwa na nywele fupi kwa miaka 2. Siku moja nika-google kujua "Tiba" ya nywele zangu "kumwagika" kutokana na kunyonyesha(mabadiliko ya Homono). Nikakutana na Vlogs za hair journey bana...hee! Nikagundua mafuta yanaitwa Castor (mafuta ya Nyonyo) mwanamke si nikakurupuka....nikawa naosha nywele kila siku na kupaka Mafuta ya nyoyo + leave in + hair cream za kutosha, Wacha nywele ziendelee kukatika mpaka nikawa kipara hihihihihi (I was crying actually). Nikaendelea kufanya Uchunguzi kwa kusoma na kusikiliza Shuhuda za watu nikagundua kuwa nakosea na nywele zangu zilikuwa zinalainika zaidi(too much moisture) bila kupata nguvu kutoka kwenye Protein (nywele zinahitaji balance ya vyote). Ndio nikakutana na wadada wakitoa shuhuda kuhusu Aphoghee Step 2 treatment ambayo unatu

Matumizi ya Tablets kwa watoto....

Mambo! Nitakuwa naandika chochote kinachonijia kichwani kwa wakati huo.....kuanzia malezi ya wanangu, habari itakayogusa Mtima wangu (usijali sio habari za Tz) na siku husika kwa ujumla. Hali ya hewa leo ni ya Unyevu na Mvua kwa mbali, Wataalam na wachunguzi wa huku wanalalama kuwa watoto wasitumie Tablets kwa vile zinawafanya wasiweze kutumia mikono kuandika au kuchora kama ilivyokua kwetu enzi zile. Lakini Enzi zetu si zimepita? hizi enzi zao waacheni ila tuwe responsible na wanachokifanya kwenye Tables, Fundisha mwanao....usitegemee mtu mwingine (Yaya/Mwalimu) akufundishie just because you pay them to do so. kwaheri kwa sasa.