Skip to main content

Posts

Showing posts with the label kiswahili

Sababu nyingine kwanini tunawachukia Mawifi....

....(Dada wa Wenza wetu) wa sasa au waliopita(Ex), hasa kama mlizaa kabla hamjakutana au  kabla ya kuachana. Kama uliikosa ile ya mwanzo isome hapa . Hello, ipo jambo? Madada huwa na viherehere bin vimbelembele vya kutaka kujua kila kitu, hasa Uhusiano ukiwa bado Mpya tangu kuanza/kuisha. wanaweza kujifanya wapo karibu na wewe na wanakupa support, wanakujua na kukupoenda blablabla. Mawifi hao hao bado ni Shangazi wa Watoto wenu na ni Kaka wa Ex/Current Mumeo,  kwa maana hiyo bado watakuwa karibu na yeyote atakae kuwa na Kaka yao. Hivyo basi kuambiwa/shuhudia mambo mengi/kupewa ripoti kuhusu Mjaza nafasi(mke/Mpenzi mpya) na watoto wake na wakati huohuo wapo karibu na wewe Ex na Watoto wako. Sasa kama wewe ni Ex au Current one mwenye utimamu hakika utaanza kujiweka  mbali na Mawifi kwa sababu chache zifuatazo:- -Hawachelewi kukulaumu kuwa umembadilisha Kaka yao. -Watakuwa wanazungumza na Kaka yao kuhusu Wifi yao wa Sasa na watoto wake na kamwe hawatokuambia(kama wewe ni Ex).

Rudisha Heshima ya Ndoa: Mfanye Mkeo ajihisi Malkia...

...Mengi ni yaleyale yanajirudia.....kukumbushana sio mbaya, kwavile tunatofautiana ni wazi kuwa Mkeo atakuwa  na vijimambo vyake ambavyo anapenda kufanyiwa ili kujihisi kuwa yeye ni "Malkia". Umalkia ninao uzungumzia hapa sio ule wa kuishi kwenye Jumba kubwa zuri lililojaa watumishi au kumfanya Mumeo kuwa Mtumwa kwako....la asha! Habari gani? Kwa kawaida Wanawake(wake) huwa na tabia ya kujitahidi kuwa Wake wema, tunafanya mengi sana kwenye Ndoa(au Uhusiano) na Familia(kama mmebarikiwa Watoto) wakati mwingine kama sio mara zote huwa tunasahau kuwa nasi pia tunahitaji kujisikia kama ambavyo tunawafanya Waume zetu kujihisi Wafalme. Soma Jinsi ya kumfanya Mumeo ajihisi Mfalme  kama uliikosa. Kama kawaida kwenye haya mambo hakuna Kanuni hivyo jaribu haya kama hujawahi na hakikisha unamsoma Mkeo vizuri ili kujua ni kitu gani hasa anahitaji kutoka kwako kama Mumewe. -Pamoja na kuwa anapesa zake, mgawie kiasi cha Pesa  zako bila sababu.....weka mahali ambapo ataziona kwa

Wenye Ndoa, tuache kuwabadilisha Waume Zetu.

Sasa kabla hatujaanza kumsimamnga Wifi kambadilisha Kaka yetu, tuangalie kwanza Wifi alikuwa nani kwao, na je uamuzi wa Wifi kupumzika ki-career baada ya Kuzaa ni kum-support Kaka yenu(Mumewe) ki-career au ni njia tu ya yeye kula Mahela ya Kaka yenu? Je ndugu zake waliokuwa wakimtegemea hawateseki kwa kukosa "kipato" kutoka kwa Dada/Mwana wao? Kwenye era hii ya Sosho Midia inabidi uwe makini sana maana info ni za kumwaga(tofauti na 2007 nilipoanza  kublog), ni kweli baadhi zinasaidia hasa zile za Medical kutoka kwenye Site za Shirika la Ugojwa husika au Shirika la Afya Duniani. Lakini linapokuja suala la Ndoa au mahusiano, ongeza umakini kwasababu Ndoa hazina Kanuni Moja na watu hatufanani hata kama tulikaa tumbo Moja Miezi 9 na kuzaliwa kupitia Njia mooja na siku Moja bado tutatofautiana kwa kiasi fulani. Maisha magumu, kila mtu anatafuta views na clicks siku hizi, mara zote(kama Wanasiasa) watu huamua kuongea au kuandika mambo ambayo wanajua watu watakuja mbio ku

Akisema "tafuta mwingine, mie siwezi/nimechoka"....

...hamaanishi kwamba ukatafute  kweli mwingine, anachomaanisha ni kuwa "nibembeleze na unihakikishie kuwa utanivumilia" mpaka nitakapo kaa sawa Kihomono au kupona(kama alikuwa anaumwa)....Za Miezi Miwili/Mitatu? hello, jambo jambo!! Kwa kawaida Mume anapopatwa na tatizo kubwa litakalomfanya ashindwe kutekeleza Majukumu yake kama Baba na Mume, Mwanamke atavumilia na kumuuguza, kumpa Moyo na Matumaini. Lakini Mwanamke akijifungua(zaa) achilia mbali kuugua....katoa Uhai wa Mtu salama baada ya Miezi 9 kukaa na kulala kwa tabu. Mara zote kipindi hiki huwa Kigumu sana japokuwa kasumba ya Jamii "kukuharakisha" upone haraka huficha ukweli kuwa Mwanamke anapojifungua hukabiliana na mambo mengi Kiafya(kimwili, kihisia na kiakili). Hali ambayo hufanya baadhi ya Wanaume kuamini kuwa Mimba na kuzaa ni "cha mtoto" tu, sio kazi(kama alivyo pizi ndani ya dakika zake 3 kwa utambu uliodumu kwa sekunde 90)....hakuna ugumu wowote, fyatueni tu. Kwa kawaida(uzoefu wa

Rudisha Heshima ya Ndoa: Mfanye Mumeo ajihisi "Mfalme"....

Waliposema "ajihisi Mfalme" hawakumanisha akutawale na kukutumikisha wewe Mkewe kama Mtumwa wake na hivyo kukosa sauti na kubaki "Ndio bwana", bali kufurahia maisha ya Ndoa na hivyo kurudisha ufanyao ili na wewe ujihisi "Malkia"......Heri ya Mwaka mpya 2017!! Mie kama Mwanandoa wa "Kitambo" sasa nimeamua Mwaka huu kurudisha Heshima ya Ndoa baada ya kuona kuwa watu wanapotosha na  hivyo Ndoa kuonekana kuwa ni Kazi...well ni Kazi ya pili baada ya ile uifanyayo kukupatia Kipato au ya Tatu ikiwa mna watoto, lakini sio Kazi kwamba ni ngumu na ukibaki humo basi wewe ni Shujaa. Hapana! Upotoshaji huo unapelekea baadhi ya watu waliokwisha "onja" Ndoa na baadae kuharibika kuchekwa/shangawa kwanini wanarudi tena Ndoani(na watu mwingine) wakati tayari wanajua "maumivu" ya Ndoa....Vijana wamekuwa wakiiogopa Ndoa. Kwasababu Ndoa moja imeharibika haina maana zote zitakuwa kama hiyo iliyopita. kumbuka watu wanatofautiana na pia kuna

How to kaza K baada ya Usiku...

...wa Tendo tayari kwa "cha" Asubuhi. Niligusia kuwa baadhi yetu(mie) huwa hatuogi baada ya Tendo Usiku, tunalala nayo ili kuachia "nature" ifanye yake(itoke yenyewe) pia  ili kutunza Utamu si eti! Maana ukikimbilia kuoga unasahau hata kama ulipata! Inategemea na Imani yako, pia inategemea unaichukuliaje Manii. Mie Binafsi Manii sio Uchafu ikiwa mwenye nayo ni Mume wangu. Ikiwa ni Mpita Njia kwamba hamna uhusiano ambao ni  "exclusive na serious" hakika Manii ni Uchafu na kamwe Usikubali yabaki Ukeni which means post hii haikuhusu hihihihi  natania usiondoke mwaya! Sijui kama unajua ila Ukikaa na Manii K-ini unakuwa hatarini kuwa "over relaxed" huko chini hivyo ikifika Asubuhi  hutofurahia Tendo kiviiiiiiiiile! Hata wakati wa kusaka Mimba hunashausiwa kukaa nayo kwa Dakika 5-15 ukiwa umejinua ili kuharakisha prosesi. Pia ukikaribia kujifungua unashauriwa kucha Manii humo muda mrefu uwezavyo ili kukusaidia wakati wa kujifungua...kwamba

Mwenza Mshindani/Mpinzani...utamjuaje?

Kuna baadhi ya watu wameumbwa/zaliwa kuwa Washindani na hivyo kwao ni kawaida(pia ni vizuri), mara nyingi huliweka hili wazi mwanzoni kabisa mwa Uhusiano. Wakati mwingine wewe mwenyewe unaweza tu kugundua kuwa Mpenzi wako ni Mshindani kwenye shughuli zake za Kibiashara/Kazi, Masomo, Utunzaji wa Pesa, namna anakutunza n.k. Lakini hutofikiria hata siku moja kuwa mkifunga Ndoa hatokubali wewe "umshinde" kwenye jambo lolote. Ukiachilia mbali mtu kuzaliwa hivyo(mshindani) pia Ushindani unaweza kusababishwa na Mazingira, Uzoefu au Malezi. Kwa wale ambao wamezaliwa wachache au wengi (Mtoto wa  Pili, Mtoto wa 3 au 5 kati ya watoto 8-10) au yule wa Pili kutoka Mwisho kati ya watoto zaidi ya 5(hii ni Uzoefu wangu binafsi mie sio Mtaalam). Pengine unaweza usigundue mpaka mtakapokuwa na Watoto, ambao huibia mambo mengi sana kati ya Wewe na Mwenza wako. Kumbuka Watoto huwarudisha nyote wawili kule mlikotokea(utotoni) na hivyo  kutaka kulea wanao kama ulivyolelewa wewe

Sio lazima wote tuseme "Nakupenda"...

...halafu inatumika ovyo sana mpaka imeanza kupoteza Maana kwa Kiswahili(hatuna "like" au hatutaki kutumia kupendezwa) na kwa Kiinglishi. Mtu humjui...ndio kwanza mmekutana, baada ya  kubadilishana Salamu, mnaagana na kuambiana "nakupenda".....wengine mnakutana tu anakuambia "Jamani Dada nakupenda". Hujambo lakini? Pia kuna wale Ndugu...."nawapenda kweli wanangu(yaani wanao)"...akiishi nao masaa 24 lazma abadili usemi wake(au hisia zake). Pamoja na kusem ahivyo bado Uzito wa neno Nakupenda upo palepale....mtu akikuambia hivyo lazima karoho karuke kwa Mshangao au kwa Uoga(kama mna-date)....Kama nilivyoahidi kutoka Post iliyopita (bofya hapa  ) leo tukumbushane namna tofauti ya kusema "nakupenda" bila kusema neno hilo. Umewahi kuambiwa nakupenda na Mke/Mume wako ukaangua Kicheko halafu unajiuliza Kasoma Blog gani leo? hihihihihi au ni Mimi tu!! sio kwamba neno hilo linachekesha bali huwa hulisikii  kutoka kwake. Wapo ambao hu

Nini Mbadala wa kuomba radhi kwa Mwenza?

Kawaida sisi Wanawake huwa tunanuna pale tunapokoseawa tukitegemea kuwa Jamaa anakereka kwa kuchuniwa na hivyo ama kukuuliza tatizo ni nini ili umpe Risala au straight up agundue kosa alilokufanyia na akuombe Msamaha. Wengine hawajali hata ukiwanunia, wanachukulia ni "mambo ya Wanawake" na Baada ya Muda utakuwa "fine". Wengine hata ukiwaambia kuwa umehisi kuwa amekukosea/umiza hisia zako na hivyo ni vema akuombe radhi bado ataendelea kujitetea, matokeo yake Ugomvi unaibuka. Sasa unakabiliana vipi na Mwenza kama huyu? Kama nilivyogusia kwenye Post iliyopita hapa  Malezi ya Mwenza wako yanahusika zaidi kwenye suala la kukubali Kosa na kuomba radhi. Baadhi ya Wanawake wapo hivyo pia lakini tofauti ni kuwa baadhi yetu huwa tunapewa Elimu ya Awali ya Maisha ya Ndoa hivyo hata kama Mama na Baba walijisahau au hawakujali kutupa malezi mema bado tutajifunza Ukubwani ili kuwa tayari kuishi na Mtu Baki(Mume). Makosa ninayoyazungumzia hapa ni yale madogo-madogo na

Jinsi ya kumfanya Mumeo kuwa kama "Romeo" kwa Juliet...

....sio kiviile ila close(I promise)....Jello! Kama Jojoba ni Hohoba kwanini Hello isiwe Jello? Ni kawaida kwa wengi kutafuta "namna ya" kupenda, kuridhisha, kuonyesha mapenzi, kujali n.k. Kuna siku Mtu aliniuliza  afanye nini ili Mumewe amuombe radhi? nikashangaa...kuna watu hawajui kuomba Radhi Wenza wao? Hakika hakuna Kanuni kwenye Maisha ya Ndoa  lakini kuna yale mambo "basic" ambayo ni lazima kila mtu ayajue na kuyafanya/tenda. Mambo hayo huwa tunafunzwa tukiwa angali wadogo, tukianza Shule na kuendelea kuona Wazazi na watu wetu wa karibu wakiyatenda/fanya . Bila kusahau kutukumbusha pale tunaposahau kuyafuata/tenda/fanya.  Ndio maana siku zote huwa nasema kuwa Mwenza ulienae hivi sasa ni Matokeo ya Malezi/Makuzi yake  bila kusahau Mazingira aliyokulia. Kiongozi kwenye Malezi hayo mambo huwa ni Mama (au Msaidizi mwenye Values kama wewe au bora Zaidi) kwavile ndio huwa anakaa na Mtoto kwa muda mrefu kuliko Baba. Sasa pamoja na

Kukabiliana na Mwenza/Mpenzi "mpya" baada ya Miaka kadhaa...

....kwa maana ya yeye kubadilika/shwa na "Rafiki" zake kama niliyogusia Post iliyopita, ikiwa hukuisoma basi bonyeza hapa . Upo salama lakini?....twenzetu! Kwanza kabisa usimwambie kuwa umebadilika, lakini akikujia na mambo mapya ambayo awali hakuwa akipenda/fuatlia then hoji kulikoni? mf: tangu lini Mpenzi unatazama Eastenders? Hee siku hizi unafuatilia hiki/kile? hii itamfanya atambue kuwa unaona mabadiliko. Pili, Jiweke mbali, yaani mbaaaaaali na hao/huyo "Rafiki" unaedhani ana/amembadilisha Mwenza/Mpenzi wako. Usimuulizie, akianza kukupa stori bila kutaja jina la Mhusika, wewe sema tu "tunamzungumzia John"(taja jina la huyo rafikie mpya)? Halafu onyesha kuwa huna "interest" ya kujua zaidi.(hii itafikisha ujumbe na hivyo kuacha stori za huyo mtu/watu). Tatu, Ataanza kutaka kukutanisha wewe na huyo "Rafiki" kwa kisingizio chochote tu, kuanzia "ametualika kama familia" au "anataka kuja kututembelea ili awaone

Pale Mwenza wako anapobadilishwa tabia na "Rafiki"...

...Mara nyingi watu husema au kuamini kuwa Mtu anapopata Pesa au Kazi mpya inayolipa Vizuri kuliko kazi yake ya Awali huwa anabadilika(nadhani niliwahi kuzungumzia kwanini watu huwa hivyo mwaka jana/juzi). Habari? natumai Uumzima wa Afya. Nirahisi kutodhani kuwa Mtu Mzima hawezi kuwa "influenced" na Mtu au Watu wapya wanaomzunguuka....kwasababu amepita Umri wa miaka 30...lakini kihalisia bado wapo Watu Wazima ambao wamekua Miili tu na Namba zimeongezeka lakini Akili zao bado ni za Kitoto. Bado wanapata hitaji la  kutaka kufanana, ku-fit in, kuwa kama yule/huyu,kukubalika n.k. Inasemekana hali hiyo  hutokana na Ukosefu fulani wa "attention" kutoka kwa Walezi/Wazazi kipindi ambacho Mhusika alikuwa chini ya Miaka 10. Kumbuka matokeo ya Malezi  tuliyopata kutoka kwa Wazazi/Walezi wetu  huwa yanaathiri maamuzi (mabaya/mazuri) na Maisha yetu ukubwani. Mtu anahitaji kitu kidogo tu ku-triger alichokosa Utotoni. Achana na hili. Sasa kwa baadhi mabadiliko huwa Waz

Mtindo 1-10 with a twist....(requested)!!

Mwenye Kwao haachi Jadi si eti? Sasa wewe(na wenzako) "mmepitilizishwa" na Umarekani sijui Usasa bin Usawa mnasahau mpaka Jadi zenu na Maana yake...sio mnasahau bali humzijui na hivyo unakurupuka tu na kusema "Kutoa Mahali ni sawa na Kuuzwa/Nunuliwa"....Hujambo lakini? Sasa ni hivi; kuna mitindo Mingi sana na kumfurahisha Mwenza wako wa Kiume kunako Faragha, kama ujuavyo mwaka 2008 niliandika Topic ya Mtindo wa 1-10 na ikiwa hujui basi endelea kusoma ili uweze kujiongezea au kujifunza "kaujuzi". Mtindo wa  "Moja mpaka Kumi" unafanyika katika Mkao wa Kifo cha Mende Mwanamke juu, Ukishakuwa tayari Bibie weka Mzigo ndani na uingie mpaka Mwisho kisha ujilaze sambamba na Mwili wa Mwenza wako ambae ni Mwanaume(nitatumia Mkibaba kuokoa Muda). Wakati upo kwenye Mkao huo tumia Misuli yako ya Uke kubana na kuachia a.k.a "Piga endiketa", baada ya hapo njoo juu na rudi chini(piga takoz hihihihi) mara Kumi....kwamba kila ukienda chini n

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao

Kufanya Mapenzi(Ngono) Hakujengi Ndoa yenye Furaha......

....lakini ni "Madhara" ya Ndoa yenye Furaha! Nimekuchanganya si eti? hata mie sielewe nilichoanza kuandika ila endelea kusoma na mimi niendelee kuandika na kwa pamoja tunakuwa kwenye Mstari na hivyo sote kuelewa. Hujambo lakini? Ngono au Kufanya Mapenzi(kama tunavyopenda kuita sie tulio Ndoani ili kuhisi "Utakatifu" wa Ndoa zetu) sio Muhimu kiviiiiiile, Muhimu ni kutunza au kuendelea kuwa na  ile hali ya kuvutia/vutiwa na Mwenza wako. Kwamba, sasa ni Miaka 8 ya Ndoa yenu lakini bado unapata misisimko uleule uliokuwa ukiupata pale anaposema "kesho nakuja"....tofauti sasa unajua anarudi saa ngapi nyumbani kwenu....Sauku ya kumuona inakupa tabasamu kuu. Wakati mwingine Unajiambia/jisemea ni jinsi gani unampenda Mume/Mkeo bila yeye kukusikia. Wakati mwingine wala huamini kuwa unaishi na Mwenza umpendae hivi(japo huwa anakuudhi na unamnunia)....Ukimuona Mkibaba unahisi "kunyetukanyetuka" na yeye akisikia sauti yako  Mkimama basi tena hana Ha

How to(Jinsi ya) kumheshimu Mumeo...

...muendelezo wa Post ya jana, kama hujaiona bofya hapa . Najua ungependa kujua namna ya kumheshimu Mumeo zaidi badala ya kuwa Chini yake si eti? Kama ujuavyo sote tumepetia Mazingira/Malezi/Makuzi tofauti na hivyo hatufanani Kitabia, hivyo basi Kuheshimu Mume nijuavyo mie huenda ni tofauti na ujuavyo wewe.,...sasa labda chukua ambalo ulikuwa hulijui na ongezea kwenye yale uyajuayo? au acha kama yalivyo ila ukiweza share yako na mie "niangalizie". Kumbuka Heshima ni muhimu kwa pande zote mbili lakini leo tunaegemea kwa Mwanaume kwasababu mimi ni eerrrr Mwanamke? also Topic ilikuwa Mwanamke kuwa Chini ya Mwanaume? Sasa kama tumeelewana hapo, twenzetu; Muachie maamuzi Makubwa- Hata kama Kipato chako ni Kikubwa mara Nane kuliko chake, Sio unajiamulia tu kununua Nyumba au kupeleka Watoto Private School kwa mfano..... kwasababu tu unaweza. Mpe Mumeo nafasi na mjadiliane. Unaweza kuweka Mezani aina/sehemu 3 za Shule/Nyumba na kisha muache yeye afanye Uamuzi wa Mwisho kisha

How to(Jinsi ya)...kuwa Chini ya "Mumeo"....

....imekuwa kawaida kwa Wanandoa Wake kwa Wame kutafuta "jinsi ya" kufanya mambo mbali mbali ili kuifanya Ndoa kusimama Imara na kuepusha misuko-suko ya kihisia na hivyo kupelekea Ndoa kuwa Ndoano na pengine kuharibika. Hii kuwa "chini ya Mumeo" hata mie siijui na vyovyote ilivyo kamwe sitokubali kuwa "Chini" ya  Mtu yeyote achilia mbali Mwanaume ila nitakuambia ninachokijua ambacho huenda ni tofauti lakini bado kinamrudishia Mwanaume hali ya kujihisi/sikia kuwa anaheshimika/heshimiwa na Mkwe. Tatizo kubwa linalofanya Wanawake kukumbushwa au lazimishwa na Jamii kuwa ni LAZIMA wawe chini ya Wanaume (asiwe na Sauti) pale wanapoamua kufunga Ndoa ni kutokana na Imani kuwa Mwanamke anaposimama na "kujitetea" na/au kum-challenge Mwanaume basi huesabika kuwa hana Adabu, hana Heshima kwa Mwanaume husika. Ukweli ni kuwa unapokuwa kwenye Ndoa ya "ndio Bwana"  kwamba kila anachokisema Mwanaume wewe unakubali tu....huondoa Changamoto

Kubishana/Fokeana Mbele ya Watoto...

....kuna Ubaya? Baadhi ya watu wanasema SIO vema kwa Watoto wenu kuwaona mkigombana iwe ni Ugomvi Mkubwa(Pesa za Savings acc zimenda wapi?) au ule mdogo(kwa makusudi hujasafisha Bafu). Nyie huwa hamgombani? Kama hamgombani basi mmoja wenu anaishi "kisiri", ulie nae sio yeye...au mmoja wenu anamuogopa mwenzie. Mie ni that Woman ambae nina Sauti kali/ya juu which is a shame kwasababu huwezi kujua kama ninafoka au ninaongea kawaida, sasa ukitaka kuongea kama mimi ni wazi kuwa Utakuwa unanifokea kitu ambacho kitanikera na hapo moto kuwaka...umeona? hihihihihi nataia!! Wazazi wengi hujizuia  kuanzisha "Mabishano" mapema na hivyo, husubiri mpaka Watoto watakapokwenda Kulala ndio wanaanza kubisha/fokeana. Nakumbuka wakati nakua Baba na Mama walikuwa wakifokeana Chumbani kwao(wakiamini tumelala) kumbe some of us (Mie) tulikuwa tunaenda kusimama Mlangoni na kuwasikilia ili tujue kama wanabishana/gombana au wanaongea kawaida tu na kama wanagombana, wanagombania n

Je ni Muhimu kurafikiana na Rafiki wa Mumeo/Mpenzio....

...just incase? Mie binafsi siwapendi Rafiki zake wote...well sio wote, wapo  ninaowapenda ila Asali wa Moyo hayupo karibu nao so nimebaki na nisio wapenda which means siwapendi WOTE!! anyway... Siku nkaenda shiriki Semina ya Wanandoa Wachanga(mie mepita Miaka Saba so nilienda kama Mzoefu). Dunia ya leo watu wanadanganyana sana aisee. Mke wa Pastor aliedumu kwenye Ndoa kwa Miaka 28, akawa anashauri Wanawake walio Ndoani ambao hawana "uzoefu". Mengi yalisemwa ila lililonigusa ni hili la LAZIMA na MUHIMU sana kuwa karibu na Rafiki wa Mumeo, just incase siku moja mkikorofishana na wewe ukashindwa kuongea moja kwa moja na Mumeo. Kwamba unaenda kwa Rafiki yake/zake na kuwaomba wamfikishie ujumbe....au "Ongea na mwenzio, maana mimi hanielewi" Kweli Mama Pasta? kweli kabisaa?? Huyu ni Mume wangu(najisema kimyomoyo Seminani), tulipokula Kiapo ilikuwa kati yake Yeye, Mimi na Mungu  na tuna-share kila kitu(isipokuwa Miswaki na DNA?) ikiwa kuna issue kati yetu Mam

Faida za Kumnunia Mwenza wako....

...Habariyo? Wanawake tunajulikana kuwa tunapenda  sana kununa-nuna si eti? Lakini hata Wanaume pia hununa, ila wao huwa hawaiti "kununa" bali "nataka kuwa peke yangu ili nifikirie" au pengine anaweza kukuambia hajisikiii vizuri au anamawazo. Sote tumetofautiana, jambo dogo kwako linaweza kuwa kubwa sana kwangu, hali kadhalika kauli yako ambayo wewe unadhani ni ya kawaida inaweza kuwa Tusi kuu kwa mwenzio na hata kuhatarisha Ndoa/Uhusiano wenu. Inategemea na Malezi/Makuzi, Mazingira, Uzoefu n.k. Wakati mwingine Kununa is all you need! Biga Mnuno kwa Siku 5(ukizidisha Mkeo/Mumeo ataku-cheat hihihihihi siku ya 6 kidate na ya Saba one night stand....Hisabati Muhimu).....the rule(Bibi yangu alisema), nuna  Maximum Siku Tano tu ukizidisha huna Mume/Mke! Kununa huko hupunguza ukaribu kati yenu kama Mke na Mume, unapokea majibu kwa mkato, ukiingia tu ndani, mmoja anahisi usingizi  ghafla hihihihihi....pia hukupa hisia ya "nampenda" lakini sipendezwi