Skip to main content

Posts

Mke anafanyiwa mapenzi, sio the other way around!

Umewahi kusikia au kusoma mahali Wanaume wakisimulia namna wanavyowafanyia Wake zao na kuapia kuwa Mwanamke nahaitaji kufanyiwa mapenzi zaidi kuliko wao Wanaume, halafu uka-wish kimoyo-moyo Mumeo aje mahali hapo asome na ajifunze?!! Kama ilivyokuwa Dinahicious Blog, kwamba kuna baadhi ya Wanaume walikuwa wakitaka Wake zao wasome Baadhi ya Makala zangu ili wajifunze. Nakumbuka wapo walioniandikia wakisema huwa wanaacha Blog wazi kwenye Simu/Laptops kwa Makusudi tu ili Mke/Mpenzi apitie. Ni muhimu kumfanya Mumeo/Mpenzi wako ajihisi  kuwa ni Mfalme hapo nyumbani kwenu na unaweza kufanya ajisikie hivyo kwa namna nyingine  nyingi na sio kwenye Kufanya mapenzi kila anapokuhitaji/mnapohitajiana/unapomhitaji(siku hazifanani si unajua Homono nini  na nini).....Mwanamke huwezi kufanya yote, mengine mwachie na yeye! Imekuwa ni kawaida kwetu sisi wakimama kutafuta Mbinu za kumfurahisha Mwanaume Kingono zaidi kuliko wao.....wao wakibaba ni kama vile wametulia tu yaani wanasubiri k

Siku ya kwanza Kidatoni...Miaka 20 tangu Secondary!

Mwaka huu November inatimia Miaka 20, sasa sio mbaya kama nikiweka kumbukumbu zangu za safari yangu ya Shule kuanzia Msingi mpaka Secondari(intro hiyo hihihihi). Siku ya kwanza naingia kama Mwanafunzi wa Kidato cha kwanza ili kuwa ngumu maana hakukuwa na mtu nilietoka nae Msingi. Wengi walikuwa wanajigawa kwa makundi kwasababu wanajuana kwa kutoka shule moja ya msingi ama shule zao zilikuwa jirani. Kulikuwa na Wanafunzi kibao kutoka Mlimani Shule ya Msingi, Olympio na Upanga(wajuajiii, mabishoo, Kiingereza kingii). Ikabidi nitafute namna ya kujiunga nao, maana kati yao watakuwa na mimi Darasa moja.....nikaanza kutumia Tiketi ya Kuiba (naongea Kiingereza kwa Nyimbo hihihihihi). Nilikuwa najua nyimbo nyingi ahsante  "Double Compact something Cassete Music system".....unaweka Compact yako halafu unasimamisha ili kuandika mstari wa Wimbo husika. Nilikuwa na "book" full of nyimbo za RnB. Baba(Mungu amrehemu) alikuwa anatununulia hizo eti tujifunze Kiinger

Wale wasema "Watanzania" Wavivu/Wazembe/Waoga...

Binafsi naamini kuwa sio sahihi kumuita mtu majina ambayo unauhakika ukiitwa wewe hutofurahia iwe ni kweli upo hivyo au la! Mfano unapomuita Mwenzio Malaya unapaswa kuwa na Uhakika kuwa  Baba ni Baba yako kweli (una DNA bila rushwa). Utamponda huyu hajitumi au Utaiponda Ofisi yake? Sasa kwa sababu tu wewe umezaliwa au kubahatika kuwa na shughuli ya kufanya huna haki ya kuwalaumu na kuwaita majina mabaya kama vile Tegemezi, wanapenda kuomba-omba Wavivu, Wazembe, Waoga, Masikini wa Fikra n.k. Pia wewe wa Ughaibuni, kwavile tu wewe unaishi huko ulipo na kuona Maisha ya baadhi ya "wenye Nchi" mazuri na ukapendezwa na labda utaratibu wa Serikali na kudhani Utaratibu huo umewekwa na "wananchi" hao kwa sababu sio Wavivu/Wazembe au majina yeyote machafu unayowaita Watanzania wenzako basi tambua kuwa unakosea. Kabla ya kuanza kumlaumu na kumshutumu Mtanzania  mwenzio kuwa matizo yake yanasababishwa na yeye kuwa mvivu au kutopenda kujituma au kufanya kazi k

Wale akina Wanangu Come First....

Hakika! wao kwanza kabla ya watu wengine baba yao included(hello Asali wa Moyo hihihihi). Hata mie nimewahi kusema/kuwaambia watu kuwa Wanangu kwanza halafu wengine na mengine ndio yanafuta. Nakumbuka nilikuwa na mwambia Mama, "nikija kuwa na mtoto, sitoruhusu mtu amshike....hata baba yake" hapo nilikuwa sijui Uchungu wa Mtoto wala Emotional connection na Bond kati ya Mimba/Mtoto na Mama. Nilihisi kuwa mtoto yupo Salama zaidi akiwa na Mama(nadhani ni Nature tu). Baada ya kuwa Mama hakika Wanangu waka wa kwanza kabla ya lolote kubwa au dogo. Maisha yangu yakazunguukwa na Wanangu na kila kitu kinachowahusu. Ikafikia mahali nikaanza kuhisi sifurahii hii "biashara" sijui "kazi" ya kuwa Mama. Ikawa too much mpaka nikasahau mimi ni nani. Nikasoma mahali (ukinipa mtihani wa Mimba, Kuzaa na kukabiliana na shida/mabadiliko ya kuwa  Mama early days baaya ya kuzaa nafaulu zaidi ya Kufaulu), maana sijawahi kusoma in my life kama nilivyosoma/ninavyoso

Eating Clean: Kifungua Kinywa kwa busy mums

Kama wewe ni busy Mum wa watoto wawili chini ya Miaka Mitano bila Msaidizi kama mimi,  hakika utakuwa unatafuta Kifungua kinywa kitakachokaa tumboni muda mrefu.  Chakula kitakachokuchukua kuanzia saa Moja asubuhi mpaka saa Kumi na Moja Jioni(au muda wako unaokula Chakula cha jioni/usiku). Hapo katikati unaweza kutafuna chochote na kunywa maji (ya kutosha) ili kujiongezea nguvu na kukata Kiu ila hutopata hisia ya kutaka kula chakila kizito. Baada ya kujifungua mtoto wa pili nilikuwa nakula Lunch asubuhi na nilifanikiwa kupunguza Mwili wa "Mimba".....then nikagundua Mayai na Kale (mboga jamii ya Kabeji). Nadhani ni kama Spinach(sio Mchicha kama Wanavyoita wa UK na US), unazijua zile Spinachi tulikuwa tunapanda kwenye Bustani za Shuleni(kama ulisoma Shule za Msondo aka non Academy? Radha yake na Muonekano wake ni tofauti lakini nahisi kuwa ni Jamii hiyo. Kwa kawaida nakula Mayai 3(kiafya unajitaji 2 kwa siku)....huwa nachanganya na Kale  kisha na

Kipindi cha Baridi ndio unahisi kuwa Stylish....

Jambo! Nimeamua kuipenda Autum/Winter sasa, sio tu kuwa Kipindi hiki ndio najihisi kuwa stailishi bali pia napata nafasi ya kutumia(vaa) kila aina ya nguo niliyonayo kwa Kujiamini zaidi kwasababu hakuna  ile "presha" ya Kunyoa Kwapa wala Miguu na Mikono.....(well naficha chini ya Tights, Jaketi au Koti). Halafu Majira haya ni Marefu kuliko hizo siku 3 za Kiangazi. September Mpaka June ni total Baridi. mekosa Pic ya Mweusi ambae ana-stayle kama yangu (ubaguzi kando) Halafu pia Wivu wa hali ya hewa unakuwa hauumi sana kwa walio  Nchi za joto, unajua kuna muda unaangalia Fashinblogs za Tz halafu unapata Wivu wa hali ya hewa.....wanavalia nguo nyepesi na wanafurahia Kiangazi kwa Muda mrefu zaidi yako. Kipindi cha Kiangazi huku kinadumu kwa Mwezi mmoja, tena sio Mwezi Mzima mnapata Jua la maana bali mara mbili au tatu kwa Wiki ndani ya Miezi 3! Sasa kuna ulazima gani ya kuipenda Summer(Kiangazi)? Halafu huku tulikohamia Mwaka huu Kiangazi kilijitokeza kwa Si

Dawa za Kuzuia Mimba.....Ukweli uliofichwa!

Haiyaaa! Kitambo eti? Leo tuzungumzie Dawa za Kuzuia Mimba, pengine unajua Mengi kuhusu hili zaidi yangu kwa sababu mie sijawahi kuyatumiaga haya Makorokocho bana. Sababu kuu haikuwa kwamba niliogopa Saratani (zote zinaongeza Uwezekano wa kupata Cancer), au Kunenepa(inategemea na Mlo wako) au kukonda bali sikutaka kuwa "mchafu"......Napenda Ngono sana tu ila sina Mpango wa Kuolewa na Wewe wala kuzaa na Wewe sasa kwanini unikojolee(achie uchafu wako, wakati wangu unauosha in sekunde). Mara nyingi huwa nakuwa Mkali ikiwa Binti(well mdogo wangu) ananijia na kuniomba ushauri wa kutumia Dawa za kuzuia Mimba wakati hana mpango wa kuolewa na huyo Bf wake.....nkauliza utakojolewa na wangapi in your life wajameni??!! Pia huwa naudhika ninaposikia Wanaume wanasema kuwa ni kazi ngumu sana kumalizia Nje na Condom inapunguza "utamu" na hivyo kuwasukuma/Lazimisha Wanawake kwenda na kutumia Vidonge/Sindano au kufanyiwa "upasuaji mdogo" ili kuwekewa ile "Y

Maharage Mabichi kutoka Tz yauzwa ASDA-UK

Unajua ile furaha unayipata unapokula kitu kutoka kwenu ambacho hujawahi kukila ulipokuwa kwenu? Kwamba unakula kwasababu tu unahisi unampa sapoti Mkulima wa kwenu. Hii ni mara ya tatu nanunua bidhaa hii  kutoka Asda kwasababu kuu mbili. Moja ni ya kijani(sababu za kiafya na kutunza mwili) na pili ni kwasababu yanatoka Bongo. Jinsi ninavyotengeneza: (kama upo interested)... Kula na/kwa Wali kama mboga: Nayachemsha kwa sekunde kiasi kisha namimina Tui la nazi (well unga wa nazi uliochanganywa na maji ya moto). Ongezea utamu kwa mlo wako kwa kuweka Embe mbivu au Ndizi mbivu. Kula na Samaki bila Wanga: Nayachemsha  pamoja ya "maua ya coli" na "brocoli" kisha  nanyunyizia pilipili Manga na Chumvi kisha namwagia "Fish sauce" kama uonavyo picha na tuvipande twa  Samaki. Kama ni mpenzi wa Rost pia zinakwenda vema hakikisha una Gravy. Unaweza kuchanganya hizo na Kisamvu (kuungwa na Karang

Siri ya Mtoto wa Kwanza, Kati na Mwisho....

Inawezekana Ndugu zako wanaokufuata au uliowakuta(inategemea umezaliwa wa ngapi) sio Damu  moja kwamba  baba na mama yenu ni mmoja. Umewahi kujiuliza kwanini mtu anaendelea kuzaa na mume/mke ambae anamtenda(tereza nje)? au Utakuta Ndoa inamatatizo lakini wanazaa tu kila mwaka....haikuhusu lakini kama Binaadam kiasilia hatuishi Kudadisi na Kujaji. Kiasili Watoto tunadhania kuwa Mama zetu ni "Malaika" lakini bwana mwanamke akiamua kushenzika anakuwa Mshenzi zaidi ya Shetwani, tofauti ni kwamba Wanawake ni wazuri kwenye kuficha siri zao. Akitaka usijue Baba yako ni nani basi hutokaa umjue......akikuaminisha kuwa fulani ni Baba yako basi itakuwa hivyo(ukidai DNA unapewa Radhi hihihihihi). Mtoto wa Kwanza: Binti yupo na anaempenda lakini Wazazi hawamtaki Jamaa aoe.....wanataka aolewe na mtu wao. Binti anaolewa na mimba yake bila muoaji kujua. Pia Binti anaweza kuwa anaendelea na ampendae ili azae nae batoto atakaowapenda kama baba yao, kuliko kuzaa na limtu

Tulionyimwa Komwe....Faida/Hasara zake!

Tufunge na kuomba kuwa na Komwe isijekuwa Fashion kama vile kuwa na Makalio Makubwa. Tutajificha wapi? wewe utakuwa unanyoa manywele yako Usoni ili uwe na Komwe?.....well mie huwa nanyoa katikati ya Nyusi (huwa zinatishia kukutana japo sio nyingi mnaita "fuzz") pia ili kutenganisha Nyusi  na "Mstari wa Nywele" huwa na Nyoa kati kati yake! Pengine hujawahi kugundua kuwa "Hairline" yangu ipo chini hasa sehemu ya pembezoni(zoom time, usiote tu hihihihi). Umbali kutoka Nyusi kwenda kwenye Nywele ni Inchi Moja na Umbali kutoka kwenye Komwe(ambalo halipo) kwenda kwenye Nywele ni Inchi Mbili na Nusu. Kuwa na "low hairline" kuna tofautiana kama ilivyo kwenye Makomwe, tofauti hizo zinafanya baadhi kutaka kuwa na Sura ndefu na hivyo kuondoa Nywele kwa kutumia Njia mbali mbali ili nywele zisirudi(tazama Picha). Mie binafsi tayari ni ba Mdogo(sura ya kiume), sasa nikiachia Nyusi kuungana wajameni si nitasababisha mkanganyo even more(usiche

Wazungu wanajua Kupenda au wanaogopa kuonwa Wabaguzi?

Kama ulikuwa na Uzoefu mbaya na Wanaume/Wanawake wa Rangi yako hili ni Tatizo lako, na uzoefu wako mbaya haufanyi wanaume/wanawake wote wa jamii hiyo kutokujua Mapenzi/kupenda. Linapokuja suala la kupenda kila "individual" anapenda kivyake kulingana na labda Ubora/viwango atakavyo/alivyojiwekea kutoka kwa mtu anaetaka kumpenda(well huwezi kutaka kupenda, penzi linaibukaga tu popote) na pengine ni kutaka kujaribu ili kuona wa rangi hii wapoje kama sio "attraction"(sio kila mtu anavutiwa na yeyote, wengine wanavutiwa na watu wa jamii/rangi fulani tu). Ukiachilia mbali hayo hapo juu, pia Imani au "life situations" zinaweza kukufanya Ufunge ndoa na Mtu wa Taifa/Rangi nyingine (mostly Wazungu) ili kuboresha maisha Kiuchumi au kuapta Makazi ya Nchi fulani ambayo kutokana na Imani yako ni kuwa Utaishi maisha Bora zaidi.....au Status kama sio (hii haikuhusu wewe) kukimbia "Kacha" Maana wanawake Weusi wa Kijamaica au USA/Latino kwa DIRAMA a

Mama wa Nyumbani kujipenda/pendeza.....Nani anakupa Ari?

Kwa sie Wafanyakazi huwa ni kawaida kushindia khanga/Pjs mwisho wa Wiki kwasababu tunatilia kila siku tuendapo kazini. Lakini je ikitokea umeamua kuwa Mama wa nyumbani kwa Muda(mie) utakuwa upo hivyo siku zote Saba za Wiki kwa Muda wote Mpaka mtoto aanze Shule?. Ni rahisi sana kujisahau na kupoteza "utambulisho" pale unapokuwa una-deal na watoto muda wote. Unafubaa, na ikiwa Nguo zako nyingi zilikuwa Office like ndio kabisaa(nani anavaa kiofisi wakati yupo nyumbani?). Skinny Jeans nazo ni shughuli....! Hapo ndio kutafuta Ari kunajitokeza....ni vema kuwa/kupata/kupewa Ari(kuwa Ispired that is) kwa uHasi ama uChanya.....zote ni hisia na ukizipata pengine unaweza kuzitumia kufikisha ujumbe kwa watu wengine au ukaepuka na labda kujifunza kama sio kupata nafuu kuwa "aah am  not the only one then". Mfano: Kuna Binti mmoja Maarufu ambae Kijamii anaonekana kuwa na Mwenendo mchafu na ni Mfano mbaya kwa Mabinti wengine ambao wanakuwa "ispayadi

Namna ya Kuondoa Mdoa(Tetekuwanga) Usoni.....

....haraka! Najua kuwa unajua napenda ku-share kile ambacho nimejifunza na kwa sehemu kubwa ni kutokana na Uzoefu. Kwabahati mbaya niliugua Tetekuwanga(ililetwa na Schooler boy wangu). Kwasababu yeye ni Mtoto haikuwa mbaya kama mie Mtu mzima. Hii ndio nikawa naitumia Asubuhi na Usiku kama mbadala ya hiyo hapo chini Lancome Genifique ndio Serum yangu Kitambo. Mbaya zaidi Mapele yakajitokeza kwa Wingi Usoni( sijui kwanini hayakwenda Mapajani au Tumboni au Miguuni)....unapopata tatizo la Ngozi mahali ambapo sio rahisi kuficha inakupotezea Amani kabisa yaani. Hakuna Dawa ya kuondoa Mdoa hayo kwa haraka(inachukua Miezi 2 mpaka Miaka kadhaa inategemea madoa yapo deep kiasi gani Ngozini). Dactor niliandikiwa dawa ya kuondoa Madoa(mie naita Mkorogo) lakini baada ya siku chache nikahisi inaharibu ngozi yangu kwa namna nyingine, kwamba inaondoa Mdoa Meusi Usoni lakini "pores" zinapanuka/zinakuwa kubwa(sijawahi kuziona pores zangu) nikaamua kuachana nayo.

Penzi la Kwanza halikufi(halifi)....

Well Penzi lolote la Kweli halifi/halifagi na penzi hili huwa halitokei kila mara, ikitokea limetokea(hilo Penzi la kweli) basi mtu unakuwa umefika.....kama ni Safari ya Reli ya Kati basi Umemaliza...upo Kibondo Kigomaaa. Pamoja na kufika kwako Kibondo( Kimapenzi) bado huwezi kusahau yule uliempenda Kweli(au kwa mara ya kwanza....sio Ngono kwa mara ya kwanza, wacha haraka). Sasa hii ni mchanganyiko wa penzi hilo "kutokufa" au wewe kukumbuka hisia ulizozipata baada ya kuwa na huyo Mwanamke/Mwanaume ambae hana uhusiano na wewe Kidamu (sio Mama/Baba).....sote tunajua namna ya kupenda na kupendwa Wazazi wetu sio? Mwanaume wa kwanza kumpenda ni Baba yako(ikiwa wewe ni Mkimama) na Mwanamke wa kwanza kumpenda ni Mama yako(ikiwa wewe ni Mkibaba). Hisia za kumpenda mtu baki ni nzuri na wakati mwingine zinachanganya(kuujua Ujinsia wako).....unaeza kujikuta unashindwa kutambua ni yupi hasa unampenda kiukweli(hisia hizi ni Mpya na ni tofauti na za kumpenda Babako).....ukako

Marafiki(best) ni Milele, Wapenzi waja na kuondoka....

....kweli kabisa (kama upo chini ya miaka 29). Unapofikia umri mkubwa mambo mengi yanabadilika na unajikuta kuwa huitaji Marafiki ili kuwa na furaha(kufurahia Maisha yako). Sio hivyo tu pia unakua/badilika(nao pia) na hivyo mnakuwa hamuendani tena kama ilivyokuwa enzi zile, Matokeo yake unakuwa unafahamiana na watu na sio kurafikiana nao(best friends eeh Siwezi!). Marafiki wanakusaidia kujifunza kuhusu Maisha (kihisia), wanakusaidia kujua namna ya kukabiliana na Drama za "maisha", wanakusaidia kujua  nini cha kudharau/kushikilia Bango, wanakusaidia kujua kuwa wewe upo tofauti nao, wanakusaidia kujuana nini cha kuchangia/kutokuchangia, wanakusaidia kujua ni wakati gani unatakiwa kuachana na jambo na kusonga mbele, wanakusaidia kuelewa jambo/somo Darasani (tunauelewa tofauti) n.k. Hivyo ni Muhimu sana tena sana kwa Mtoto kutengeneza Marafiki ili aweze kujifunza hayo niliyoyataja hapo juu. Sio kila kitu Mtoto anajifunza kutoka kwa Wazazi, mengine anajifunza akiwa S

Kujiamini kwa Mtoto kunaanza lini?

....Watoto wa "Ulaya" wanajiamini sana, je kuna namna ya kulea mtoto ili akikua ajiamini kama wa Ulaya? Mkaka mmoja aliniuliza. Nadhani wengi wetu tumeaminishwa Mengi ya Ughaibuni ni Mazuri/Mema....lakini katika hali halisi sivyo. Kuna soko zuri sana la Vitabu/Vipindi vya TV vinavyofunza Wazazi namna ya kulea watoto wenye Kujiamini. Ni tatizo la Wazazi husika ambao walilelewa "Kimaendeleo" na hivyo kuhofia kuwa watoto wao watakuwa kama wao. Hofu hiyo inawafanya wazazi kuwa-overprotect watoto. Nahisi tu sina uhakika. Kujiamini kunategemea zaidi na Malezi(nakubali) lakini sehemu kuwa ya Mtu/Mtoto kujiamini inatokana na yeye mwenyewe alivyoumbwa. Niliwahi kugusia Bloguni hapa kuwa kuna baadhi tumezaliwa hivyo(tunajiamini) lakini pia wapo ambao hawajiamini mpaka wafunzwe/himizwa/pewa Moyo/saidiwa kujiamini. Naamini Watoto wa Afrika(well Tanzania wa kizazi kileeee) tunajiamini kwasababu tulitumia muda mwingi kujifunza kimwili na sio kihisia kama watoto

Wanawake hatupendani....usimbee awe Jaji sasa!

Sina hakika kama hii ni Imani tu au ni kweli, Naturally Wanawake hawanipendi mie binafsi(imagine ningekuwa mzuri sasa!) ila Wanaume wanananipenda(napatana zaidi na Wakibaba kuliko Wakimama). Kuna siku Mfanyakazi mwenzangu akanijia kwenye Dawati langu akanambia "dinah unajua nakuchukia".....mie nkacheka halafu nikamwambia "sio peke yako, nimezoea kuchukiwa na wanawake"....wewe ungesema is because i am Black! Sasa, hii "wanawake hawapendani" ipo kila Nchi Duniani.....kila mtu anaibuka na sababu yake kwanini hasa hatupendani. Baadhi wanadai ni Wivu wa kike(umbile/kupendeza/mafanikio/kuwa na easylife) na wengine wanasema ni mambo ya Homono tu. Mie sio kwamba nachukia wanawake bali sipendenzwi na tabia ya baadhi ya wanawake wanaofanya maamuzi ya Kipumbavu, kama vile kutojikinga dhidi ya Mimba, au kujitegeshea kushika Mimba ili tu waolewe au wapate sehemu ya Kipato ya Mwanaume husika. Sipendi mwanamke ajishushe ili kuonewa kirahisi. Vilevile

Usenge + Ubunifu wa Mavazi=Skinny Models

Unaamini katika Chunguzi za Kisayansi? Mie naamini zile za Kitibabu(ambazo ni Sayansi pia.....kabla hujanijaji, tambua kuwa kuna Sayansi za aina nyingi....Viumbe,Mimea,Siasa,Kemikali n.k). Natumaini wewe ni mzima kabisa. Kama ujuavyo suala la Waonyesha mavazi/Wanamitindo kuwa Size Sufuri ni pana na mpaka likaingizwa kwenye Siasa(likafeli). Lakini bado hawa wafanya biashara watumiao Miili yao kuonyesha mavazi(Models/Wanamitindo) wanaandamwa kutokana na wembamba wao. Baadhi ya watu "mtaani" wanadai kuwa Wabunifu wanachagua "unreal women" kwasababu wao(most of them) ni Mikorosho/Wasenge na hivyo nguo wanazobuni ni za kutosha Wavulana na sio Wanawake......Unabisha?, endelea kusoma sasa. Kiasilia Mwanaume anaevutiwa na kupendeza kwa mwanamke atazingatia Umbile la Mwanamke, kwamba juu Mdogo halafu chini mkubwa/pana(Peasi)  au Juu mkubwa , kati mdogo halafu chini mkubwa pia(namba nane)....tuliobaki ni WAVULANA hihihihihi. Sasa kwa Msenge ambae ni Mbu

Kuoga Usiku Vs Asubuhi/Mchana!

Haiyaaa! Kiangazi Kimeisha na Mvua ime-cotton fire, hii sio sababu ya wewe kuacha kuoga. Usafi wa Mwili ni muhimu kama vilivyo vitu vingine Maishani. Lakini je wewe unaoga mara ngapi kwa Siku? na je kuna ulazima wa kuoga zaidi ya mara moja kwa Siku? Wanawake tunapewa/peana PRESHA kuoga-oga  mara nyingi na tunaambiwa tusipooga tunatoa harufu kwa sababu ya Maumbile yetu, lakini wanasahau kuwa kunakosababisha harufu sio mwili as in Ngozi, bali kwapa na kunako(Nyeti) ambazo hata wanaume wanazo na zinatema harufu pia ikiwa hazitaoshwa. Sasa nikianzia mwisho, hakika kuna ulazima wa kuoga zaidi ya mara Moja kwa siku, Inategemea unafanya kazi gani na wapi, unatumia Usafiri gani(kubanana  kwenye daladala/train hakika unabeba wadudu) na bila kusahau hali ya hewa. Ikiwa unafanya kazi Hospitali(una deal na maambukizo), unaishi mahali penye joto sana au kazi yako inakufanya utoke jasho sana mpaka unanata basi wewe oga mara zote unazohitaji. Kitibabu tunapaswa kuoga angalau

Kwa Mliojipiga/Lipua/Fuata Sheria Ughaibuni....

....yote Maisha na kila mtu anayatafuta kwa namna yake sio(usidhani nakukebehi, naelewa sana). Sasa kama ilivyokawaida ya Mie, ninapohisi kuwa nimejifunza huwa sio mchoyo ku-share. Hujambo lakini? Unafurahia simu yakoo Mpya(smartphone) ambayo ipo loaded na ma-Apps mwengine wala hujui kazi yake(unadhani yanafanya Simu yako kufanya kazi vema) kumbe katika hali halisi sivyo. Baadhi ya Apps(zile zinazowekwa kila unapo Update Software) huwa zinawekwa na Mitandao husika ili kufuatilia Nyendo zako. Tangu zamani wamekuwa wakifuatilia ili kuboresha Huduma za Mawasiliano, lakini kutokana na uwingi wa Uovu hasa kutoka kwa wenzetu wale Wauaji kwa jina la Dini yao takatifu, hali imekuwa mbaya linapokuja suala la "privacy". Sio Kampuni za Simu tu ndio zinatabia(banwa Kishria) bali pia Facebook, Google na Whassap wanatabia ya kutunza yote unayo-post kwa ajili ya "kuboresha" Huduma zao (wanamaanisha kutunza Data uwekazo kama Ushahidi pale  mambo yamebuna na Serikal

Pale unapokuwa Mke mwema....

....halafu unaonekana sio mwanamke "kamili", kwanini? kwasababu hulalamini-lalamiki pale mumeo anapoacha bafu chafu baada ya kuoga au pengine anachelewa kuamka na kuacha kitanda kipo shagala bagala....(hizi sio kazi za mwanamke ni usafi), huombi-ombi pesa ya manunuzi, Vipodozi wala Salon. Inawezekana upo hivyo kutokana na Malezi/mafunzo uliyopitia au huenda umejifunza kupitia Blogs, maana Siku hizi kuna kila aina ya maelezo yanayotuelekeza namna ya kuwa  Wake(na waume) wema, mengine ni mazuri na mengine yanapotosha.....Akili kumkichwa unapoamua kuchukua na  kujaribu ulichokisoma! Ulalamishi na kutaka jambo/kitu kifanyike pale tunapotaka  ndio  inatufanya wanawake kuwa wanawake (ni sehemu ya uanamke), sasa hayo yakikosekana inakuwa kama vile Mumeo ameoa  mwanaume mwenzie ahahahaha. I mean sawa kujitegemea kiuchumi na kuepuka ulalamishi.....lakini pia tukumbuke kuwa baadhi ya Wanaume hupenda Changamoto Ndoani (sio za kugombana na muumizana mioyo/hisia)! Nat

Urijali/Uanaume Kamili/wa Kweli!

.....hapa lazma nivabe! Lakini kwasababu napenda kuchangia "knowledge" sio mbaya nikikuelezea nilichojifunza. Inawezekana kabisa hukubaliani na ninachotaka kuandika, basi angalau nipe nafasi na unisikilize(soma na share....ahsante). Unajua pale unaanzisha Topic halafu watu wanaivamia na kuaanza Malumbano (ya busara) halafu wewe upo pembeni unafurahia huku  unachukua "Material", basi ndivyo ilivyokuwa. Wengi tunaamini(mie mmoja wao mpaka Wiki Majuzi) kuwa Mwanume Rijal/Kamilii ni yule mwenye Uwezo wa Kusimamisha Uume kwa muda Mrefu au mwenye uwezo wa Kusimama na kufanya mapenzi na kufanikiwa kummimba mwanamke. Baadhi hudhani kuwa Wasenge sio Marijali kwasababu hawapendi wanawake aka hawawezi kuingia ukeni sababu hawawezi kuinuka(Hanithi).....kama Kusimamisha kwa muda mrefu ni Urijali basi hawa  majamaa ni MARIJALI haswa!! Achana na hili. Sehemu ndogo wanaamini kuwa kama Mwanaume  ni Rijali mwanamke mmoja hamtoshi....daah! Ujinga Mzigo. Hawa wan

Knowledge vs Ego....

Kwa maCeleb Ego hujionyesha wazi kwenye mahojiano ya moja kwa moja. Baadhi wanadhani kuwa ni wao tu ndio wanazo hizo Ego, nitakupa mfano na pengine kukusaidia(kama hujui) kuitambua kutoka kwa Mwenza wako. Kwa mimi na wewe Ego zetu hujitokeza zaidi pale tunapogombana. Ndoani/Mahusiano huwa tunagombana sana eti? Wakati mwingine ugomvi unakuwa hauna hata maana. Ujue kuna ile kugombana kwasababu mmoja wenu kafanya kosa kubwa kama vile umegundua kuwa amekuwa akipeleka Pesa mahali ambapo hupajui! Kwa mfano. Sio kwanini hakupokea simu?!! Na ikiwa mnawatoto basi mnaweza kugombana kwasababu mmoja wenu anahisi kuwa anaingiliwa kwenye kona yake ya malezi(wanaume) au mwingine(sisi wakimama) kuhisi kuwa watoto wanaonewa au mwenzio hatoi muda kuwaelewa watoto na badala yake anatanguliza kufoka (hasira) kwa watoto. Katika hali halisi kama mmoja wenu anawakilisha linalomkwaza kwa namna ya kawaida(kukereka bila hasira/kufoka) na mwingine kusikiliza hakutokuwa na ugomvi. Inaitwa MAWASILIANO/K

Ngono ya Usiku mmoja M'ke vs M'me....

...nani Malaya? Hello there. Kwenye harakati za Mpito za Ujana ni wazi unajifunza kwa kufanya mambo mengi kwa kupatia au kukosea. Sio mara zote unakosea ili kujifunza(usifanye makosa makusudi kwa kisingizo cha kujifunza), wakati mwingine unakosea kwa Uzembe(kutokujali). Kama ilivyo kwenye kila kipindi cha  " Mpito" mambo huwa magumu.....wakati mwingine mtu unajikuta unakata tamaa na kuamua kuwa LIWALO NA LIWE na hapo ndio maamuzi ya kizembe yanapojitokeza. Inaweza kuwa Pombe au Utumiaji wa madawa na Ngono Holela au vyote. Inawezekana kabisa kufanya hayo ni katika hali ya kutafuta "amani" au kuondoa "msongamano wa mawazo" na pengine ku-fit in na jamii inayokuzunguuka wakati huo wa Ujana wako. Kwaharaka haraka unaweza kudhani umepata "tiba" lakini katika hali halisi unajiongezea shida/majukumu kabla ya Muda wako. Sasa, kutokana na hali ilivyo siku hizi (Mambo ya Haki sawa sijui Usawa) inafanya mambo mengi ambayo awali yalifanyw

Weusi wa Ngozi sio Uchafu....

....ila usipokuwa muangalifu kwenye kuchagua Rangi za Mavazi/Nywele hakika utaonekana Mchafu(huvutii), hii  haina kujiamini.....nadhani ni muhimu kuchagua Rangi zinazoendana na Rangi ya Ngozi  yako. Mambo?!! Kuna siku nipo na mishughuliko yangu ya ndani wakati Asali wa Moyo anatazama Mashindano ya Tenesi ya Wibledoni. Anapendezwa sana na wale Williams Dadaz....mmoja wao alikuwa anacheza. Mwenyewe anafurahia uchezaji wake (au kuona Tako  kila kisketi chake kinapoinuka hihihihi maana mdada mMashallah). Sina hili wala lile nasikia mwenznagu anawasifia wadada Williams kwa kutokuwa kama Celebs wengine.....mie nkasema hao sio ma-Celeb ni Sports Stars (kwa Kiswahili ndio tunasemaje vile?) ila Media inalazimisha kuwaweka kwenye Kundi la M-aceleb kitu ambacho sio haki kwasababu wapo walipo kutokana na kazi/kujituma kwaoo na sio kuonekana kwenye Tv au kuuza Haidthi kwenye magazeti au....oh well kwa Umalaya. Katika kufunga maelezo yangu nikamalizia na....kiukweli mie siwaelewi

Je Unaogopa Kujaji watu(wenzio)?

Habari yako? Nilikuwa Likizo ya Kiangazi.....katika hali halisi  nilipaswa kukujulisha lakini nikahisi kama vile nitakuwa najionyesha au napitiliza ku-share so nikapiga kimya. Anyway habari kwa ufup,  kama bado unajali ni kwamba Madoa ya Tetekuwanga(Chickenpox) yamepungua Weusi. Ujisedhani hali ya Hewa ya UK inafanya Ngozi kutakata haraka ndugu, nilipewa Mkorogo(andikiwa dawa ya kuondoa Weusi) nitumie kwa Muda wa Wiki 8. Baada ya kugusa Wiki ya Pili nikaona Vijitundu vya ngozi(pores) vinapanuka! Aiiii nikautupilia mbali Mkorogo. Duania ya leo inamengi na kila kukicha tunaongezewa sheria za namna ya Kuishi vizuri au kuishi na watu kwenye jamii. Tunaambiwa tusiwajaji wenzetu kitu ambacho sio rahisi kwa sababu kujaji ni asili ya  mwanadamu, pia bila kujaji hakika utakuwa unafanya maamuzi mambovu na hivyo kuishi ukilalama "kwanini mimi". Nimekwishawahi kukuambia hapa(kwenye blog hii) kuwa mie huwa najaji watu/mtu kama wewe ila tofauti yangu mimi na wewe