Skip to main content

Posts

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Chuki....

Ni sehemu ya Ubinaadamu si eti! Kama unaweza kupenda basi ujue unaweza kuchukia pia....zote ni hisia! Mie bana ukiniudhi kwa kiwango cha kutosha na ukijaribu kuingilia Maisha yangu binafsi nakuchukia wewe, Familia yako, Ukoo wako, Jamii yako, Kabila lako na Nchi yako kwa Ujumla. Yaani watu wanaotoka huko unakotoka wewe wote wanakuwa Maadui, yaani siwaPENDIIIIII mf ni Wanajeria.....Mungu anisamehe ila daa! Nawachukia balaa.....wengine ni wale Majirani zetu waliozima ka' umeme wa Tanesco (what does it mean) ambao hatutaniani na Kiswahili kwao ni sawa na kuwa Malaya the Nigerian of East Africa....BOY I HATE THEM. Alafu kuna Wazimb hihihihihihi nikupe stori? Ni washenzi.....hapa hapatoshi kwa stori, maana ninazo nyingi. Huyo mimi, halafu kuna wewe (sio wewe bali yule)....ambae unamchukia tu mtu wakati wala humjui, hujawahi kukutana nae na wala hajawahi kujihusisha na lolote linalokuhusu! Unaanza Vita!.....aah! Kuna jamaa namkumbuka alikuwa namuandama mwenzie kwa chuki ya wazi kabisa ha

Nipo mtaani kwako, upo home?...

Sipendi hii tabia kwa Moyo Mkunjufu kabisa!!! Nilikuwa namkimbia rafiki yangu Mghana kwa tabia hii....niambie basi siku moja kabla hujaja kuwa unapanga kuja kwangu....sio unafika Mtaani kwangu au pengine Mlangoni halafu ndio unaniambia kwa Simu! Sio peke yake, hata ndugu (wa mbali) na jamaa wanatabia hiyo....kuna siku (nikiwa bado Nyumbani) nilimrudisha mtu kwao on next flight....the next Bus bana, hela ya next flight mie ninayo?!!....nikaambiwa nina Roho Mbaya. Katoka huko Mwanza sijui wapi eti kaja kutafuta Kazi, asa kwanini usituambie mapema tujiandae na Bajeti!....anyway achana na hilo. Mie huwa sifanyi jambo ambalo najua sipendi kufanyiwa, tatizo linakuja pale Mwenza wako sasa anatabia hiyo....hehehehe Baba Babuu Asali wa Moyo wangu bana anaudhi kweli!!! Mnaweza mkawa safarini mara akakumbuka fulani anakaa karibu na hapo mnapopumzika labda....ananyanyua simu "eh bwana fulani! Upo nyumbani?....tupo hapa karibu kama vipi tuje kuwasa

Make up artists....

Ukiingia kwenye Department stores au Boots (Duka la Dawa na Vipodozi) kubwa kwa sie wa Ulaya hii hapa....unakutana na MUA kwenye "viOSK" vyao wenyewe wamejiremba wamependeza....er kwa mbali! Asa sinilikuambia tangu nigonge miaka 30....sasa ni 30na nimeanza "kuipenda" ngozi yangu ya usoni! "Mambo ya mwanamke reception".....sasa kama mtu hukujaaliwa "reception" nzuri au kurembeka(mimi) basi angalau Ngozi iwe nzuri na yenye afya kuwapotezea watu "focus". Mwanamke nimejaribu bidhaa kibawoo za kufanya Uso wangu uwe laini na wenye rangi moja....maana...mmh! Sijawahi kutumia Mkorogo (na sina mpango huo), sina tatizo na Chunusi (mpaka nile Chocolate), yaani ngozi yangu inakaribia ukawaida tu japo inatoa mafuta ya kutosha kukaangia Vitumbua....anyway! Nimejaribu skin care nilizokuwa nikitumia miaka ya nyuma in my late 20s, sasa zinadunda, kitu cha uso ama kimekomaa au kimekuwa Sungu (Kisayansi ngozi hupoteza n

Kabla hujafa, hujaumbika!

Ni kawaida ya watu (wengi) kucheka matatizo ya wenzao au kuyazungumzia katika mtindo wa "kichekesho". Mimi napenda sana kucheka na kuchekesha (japo kuwa sichekeshi....yaani nikitoa kichekesho watu hawacheki mpaka nielezee kwanini nilichosema kinachekesha)....hihihihi achana na hili! Matatizo nayogusia hapa ni yale ambayo mtu hana uwezo wa kuyazuia, sio matatizo ya kujitakia(kuchagua) kama vile Utumiaji wa Madawa (japokuwa hata hawa mie huwa siwacheki). Kama huna utu na huna mpango wa kumsaidia mwenye matatizo kwanini uzungumzie matatizo yake kwa watu wengine katika hali ya "kumcheka"? Wengine wanapoleta habari za mtu za kusikitisha kutokana na matatizo yake yaliyobadilisha Mwili au Akili (Ulemavu) yake hawacheki kwa kukenua Meno, lakini jinsi wanavyoelezea unagundua kabisa wanamcheka mhusika. Mf; "Eh bwana unamkumbuka Elia? Daah jamaa yaani kaisha halafu sasa anatembelea Mgongo. Yule jamaa alikuwa anajifanya mjanja sana"....umeona? Hakenui meno laki

Kuvaa Wig!

Nimekugaya eti?!! Well kwani tulisaini mkataba wa mimi kuwepo hapa kila siku? Hihihihi usiache kusoma bana, hebu baki hapa upate stori ya Wig. Ujue kuna siku akili inachoka alafu kunakuwa kama "empty" hivi kichwani kwa ndani, yaani hata yasiyo na maana nayo huondoka basi inakuwa ngumu kidogo kuandika ili ueleweke. Ikifikia mahali unaandika (huku unasoma bila shaka) lakini unahisi hakileti maana....basi tambua kuwa unahitaji Mapumziko kiakili! Anyway.... Wanangu na Baba yao wamelala....Joto limewachosha, maana leo ka' tupo Kisarawe.....achana na hilo. Nimekaa hapa nikakumbuka Wig langu la kujinyonga wenyewe mnaita Curl sijui Karikiti. Kwa kawaida mie sio mvaaji wa hayo mavitu, ila baada ya "issue" ya nywele nkasema ngoja nami niwekeze kwenye "Afro Wig". Siku (2.5yrs ago) nkalivaa, baada ya kutoka Kazini nkaenda Chekechea kumchukua Babuu ....hee! Mtoto wacha alie alafu anaangalia juu (lilipo Wig) hehehehe....nikazuga bana mbele ya Wazungu as walijua nim

Mama yangu alikuwa Kimada!

Uishie hapo hapo!! Najua umekuja mbio hasa kama wewe ni Kimada aka Mwizi au mtoto wa Kimada. Mama yangu alikua Mke wa haki na sote tumezaliwa Ndoani.....alikuwa* kwasababu Baba ni Marehemu, huko Ahera sijui kaoa tena? Roho itaniuma sana nikijua kaoa tena. Anyway. Kuna wale watoto wa Vimada ambao huja na mijisababu kibao ili kutetea Mama zao Vimada au Baba zao Malaya....wengine wanakuja na "Wake wanajibana wakati Vimada wanajiachia miili yao"....wengine wanajifanya wamefanya "Utafiti" na kugundua kuwa Vimada wanajua Mapenzi kuliko wake n.k. Hakuna ku-justfy hapa, kama wewe ni mtoto wa Kimada utabaki kuwa hivyo!! Tena ngoja nikolezee Mama yako ni kamwizi na baba yako ni kamalaya....tuliache hilo kwanza. Hivi unajisikiaje kwa mfano Umeolewa/Umeoa mtoto wa Kimada, yaani Mama mkwe wako ni "mwizi" wa mume wa mtu na huyo Mume(Baba mkwe) ni Malaya.....hihihihihi mie nisingekuwa comfortable yaani ningekuwa nawakwepa m

Kupotea Suna!

Mara ya kwanza kumiliki "SmartPhone" ndio ikawa mwisho wa Mimi kupotea(in my head)....leo 2014 na Tech yote ya Ramani na Gadgets zote zilizopo za "Directions" bado napotea.....Hapo ndio Suna inakuja sasa(sina sababu nyingine). Kwa kawaida nikipotea huwa sioni aibu kumuuliza mtu au kuomba anielekeze....tofauti yangu na wewe ni hivi; huwa sisimamisha mtu yeyote tu, nategea wale ambao sio attractive (at least machoni mwangu). Kwanini nachagua unattractive watu(Wake kwa Waume)? Hata sijui....ila nahisi kama wao ndio wanatoa maelezo vizuri kuliko wale "attractive"....wanakuelekeza utadhani unawatongoza(mie mwanamke, mke na mama nikutongozee nini wee fala...). Naweza nikaenda mwendo mrefu kutoka sehemu niliyopotea mpaka nikutane na unattractive person ndio nimuombe "directions". Nishakuwa stereotyped sana, hivyo wala siogopi kustiriotaipu watu.....ndio maisha...heri umejua kuliko ningekudanganya. Si eti?

Macho yane...

Jana si nilikuambia "nalikizoka" sehemu- sehemu ya Ulaya?....nkaenda kwenye Shopping Centre yao kubwa na wanangu wawili! (Siku zote huwa napita kwa nje tu). Simlituambia wa Ulaya hatuwezi "kulikizoka" Tanzania, sababu tukija huko sio Likizo tena bali tumerudi nyumbani, ni ukweli kabisa (sijui hili limekujaje hapa, tuliache)! Basi humo ndani (shopping centre) Macho yangu yamesifiwa na watu kibawoooo....hee! Mwanamke nikashanga....(Najua nina tumajicho tuzuri ila sio kiviiiiile)! Mkaka mmoja akashindwa kujizua akaniuliza "where are you from"? Nkamwambia "England" hihihihiihi nkaona NOMA! nkasema Tanzania, East Afrika, I have 2 kids and a husband....akasema "are all grown women look like you?....Fit, Nice skin and beautiful eyes?" Nkasema Yes! (Nimeitangaza Tanzania hapo) England hawayaonagi Macho yangu au dharau tu washenzi kabisa wale, mmmh! Ila inawezekana ni u-busy wa Maisha. Watu hawana habari, akili yote ina-focus kwenye £ ili kulipa

Siri...

Unawajua wale akina "nilificha/nilifanya SIRI kwasababu nilikuwa nalinda hisia zako"....."Kwasababu sikutaka kukuumiza" mifano ya watu the shenzi kind of people? Halafu sasa umejua! maumivu ni zaidi kuliko ungejua siku aliyoifanya hiyo siri....well in my case, reaction yangu ni ileile ufiche siri kwa miaka 10 au uniambie masaa machache yaliyopita....AM GONE!! Siri uliyofichwa kwa Miezi/Miaka huuma zaidi kuliko kuambiwa moja kwa moja! The thing is kuendelea kuishi na mtu huyo ni sawa na kuishi maisha ya "Uongo". Usikute hapa nafichwa mambo kibao alafu kimbelembele na-blog hihihihihi, siku nikijua hata kama nimefikisha miaka 50, sisamehi aisee...hii ni karne ya 21 sio Enzi za Yesu!! Aah. Kuna mambo ya kifamilia hupaswi kumueleza mwenza wako unless unajua kabisa yatamu-affect yeye na watoto. Vinginevyo yaache huko huko "familiani". Sasa hizo sio Siri ninazozungumzia hapa, maana hazikuhusu! Si

Karibu, jisikie upo Nyumbani....

Utawekewa "Maeneji" mabaya nyumbani kwako na maukarimu yako yaliyopitiliza yasioyojua mipaka, shauri yako! Unawajua wale wageni wanakuja kwako alafu wanaaza Ziara rasmi ya Chumba hadi Chumba, Droo hadi Droo, wanajipulizia Manukato yako na kujaribishia Viatu na Nguo zako.....WANANIUDHI sana. Wazungu wao huona sifa au sijui ni Kacha yao! Hata sielewi, kama ni mara ya kwanza kufika kwake atakupa Ziara ya nyumba yote mpaka Stoo kwa hiari yao....(Tuwaache). Ujue hapa Duniani bana kila mtu anamikosi yake, shida, raha na tabu zake. Hujui kapita wapi kutegemeana na "Imani" yake ili kujaribu kuiondoa Mikosi (kila mtu na siri yake bana). Siku unamkabidhi Nyumba yako unaanza kuona mambo hayawi mambo. ....usikute "eneji" yangu nzuri kwangu mimi na familia yangu, sasa ukinikabidhi nyumba yako nijisikie ka' kwangu alafu "eneji" yako mbaya ikai-triger "eneji" yangu nzuri na kuzalisha "sumu" yakawa mambo sio mambo usilalamike....Mfano tu

Uelewa na kumbukumbu ya Mtoto.

Nilipotobolewa Masikio nilikuwa na Miezi Sita (kwa Mujibu wa Mama), alienitoboa ni Mama wa Kimasai na aliekuwa kanibeba/shika ni Bibi yake Mama. Sikumbuki maumivu, lakini nakumbuka nililia sana nilipomuona Mama wa Kimasai na Shanga zake na Masikio yakiwa marefu "kwenda chini". Siku niliyomsimulia Mama kuhusu hiyo siku ya tukio (nilikuwa teen na bado naikumbuka)...alinishangaa na kusema kuwa lazima nilisikia akisimulia watu, mtoto wa miezi Sita hawezi kukumbuka. Nilipokuwa na miaka 3 au zaidi, tulikuwa Mjini Mbeya....Mama, Mimi, Mjomba na watu wengine tulikuwa tunapita pembezoni mwa Mto. Mjomba wangu alinibeba na kutishia kunirusha kwenye Maji(Mto)....Nadhani ndio maana naogopa Maji....Safari zangu ni za Anga, Reli na Barabara, mie Meli sijui Boti sipandi....Mtumbwi? Bora uniue. The point is, Mtoto anauwezo wa kutunza kumbukumbu kuanzia umri mdogo sana kuliko tunavyoaminishwa na "Mzungu" the Shenzi. Sio unafanya mambo u

Kaja for a reason....

Wacha kujipa Moyo.....hakuna mtu anajiijia tu maishani mwako isipokuwa wewe unaruhusu awe/aingie Maishani mwako. Ukisema umefanya maamuzi mabaya ya kuruhusu huyo particular mtu maishani mwako nitakuelewa. Kumbuka wewe ndio responsible kwa kila kinachotokea maishani mwako iwe ni maamuzi mazuri au mabaya.....beba mzigo na ujipange upya, sio kujipa-jipa moyo...eti sababu Mzungu anakuaminisha kuwa "people come in your life for a reason". Kuna watu wanaishi ili kuharibu maisha ya watu, ndio furaha yao. Wengine walikosa mapenzi na malezi bora kutoka kwa Wazazi/Walezi matokeo yake wanayatafuta waliyoyakosa kwa kuharibu maisha ya wenzao.....nakadhalika. Sasa ni juu yako kumsoma yeyote anaekuja maishani mwako na kumruhusu aingine kama Rafiki, Mpenzi, Jamaa ( wale mliooa/olewa Ukoo Mmoja), ukigundua tu kuwa umekosea basi haraka muepuke kabla hajaharibu zaidi. Nikupe mfano?....I looooooooooove mifano hihihihihi(watu tunauelewa tofauti, bila mifano wengine tunatoka kapa). Unaishi maisha

Mali ya Familia...

Kuna baadhi yetu tunatabia/kasumba ya kuita Mali za watu kuwa zetu na pengine kuanzisha fujo na kupelekea Vita kubwa ili kila mmoja apate "mgao" wake. Kwasababu tu Mali ni za Baba/Mama yako au Kaka/Dada yako haikupi haki ya wewe kupata Mgao....wacha papara za kutaka kunijibu, nitakupa mfano ili unielewe vema. Baba na Mama wameachana wakiwa hawana kitu, Baba kaanzisha uhusiano mwingine na kupata familia "mpya"....mambo yakaenda vema wakawa na Mali za kutosha....wewe uliezaliwa na Mama wa kwanza unadhani una unahaki na Mgao sawa kama watoto waliomo kwenye "familia Mpya"? Upatikanaji wa Mali za Baba yako na familia yake Mpya unamchango Mkubwa wa Mama yao (familia Mpya) na sio Mama yako (alieachana na Baba yako akiwa hana kitu)....sehemu ya mali utakayoipata ni ndogo sana, tena kama Mke atakubali upatiwe. Mf; wa kwanza. Mf wa Pili: Dada/Kaka kajipinda na kujituma yeye na Mume/Mkewe na sasa wanamiliki Mali nzito, inakuaje wakubwa/wadogo watu mhesabu kuwa hizo

Weusi mzuri...

If you have to tell us then it isn't....Mambo vipi? Weusi wa Afrika tuna issues zetu ambazo zinasababishwa na Watawala wetu(Siasa)....ila Weusi wa Wamarekani wana issues vichwani mwao kuhusu Weusi wao, yaani wapo ka' Mikorosho vile. Ujue kunatofauti ya kujivunia ulivyo na kulazimisha watu wajue kuwa unajivunia ulivyo. Mf: Kuna ulazima gani wa kusema "mimi ni mweusi na ninajivunia" wakati tunakuona wewe ni mweusi, unajipenda, unapendeza na unafanya mambo yako kama watu wengine. Kwanini utulazimishe kutambua kuwa "unajivunia"? Mf wa pili; Kitu gani kinakufanya uweke "kichwa cha habari" cha video/picha na kusema "beautiful black baby"....kwani ukiandika "baby" au "beautiful baby" haileti maana au hakuna watoto weusi na wazuri isipokuwa huyo wako? Unatulazimisha kutambua kuwa unajivunia Weusi wako alright, lakini picha/video "unazipausha" ili zionekane na karan

Kumbukumbu...

Nimekaa hapa nakumbuka watu wote niliosoma nao Msingi na Sekondari kwa Majina yao yote Mawili(la mwanzo na la Mwisho).....nimeambulia kusisinzia. Darasa Moja tulikuwa. Wanafunzi 200na! Tuligawanywa katika Mikondo 5 yaani A-B-C-D-E-F....shule kubwa ka' Kijiji....hiyo Msingi. Sekondari hatukuwa wengi sana Mikondo ilikuwa Minne. Sasa mwanamke nkasema ngoja nipime uwezo wa akili yangu sehemu ya kutunza kumbukumbu....nimefeli yaani nimepoteza kumbukumbu hata Miaka 40 sijafika!. Nikajipa Moyo; labda niagize picha za enzi za shule ili nikiona sura zao niwakumbuke vema, lakini hata hivyo sikupiga picha na kila mtu niliesoma nae kwahiyo haitosaidia. Yaani ndio basi tena. Nimejisikia vibaya sana....yaani kupoteza kumbukumbu ya sehemu ya Maisha yako ndio inauma hivi?!!! Kama ulisoma na mimi na unanikumbuka eeh! Drop me a line. Babai... Mapendo tele kwako...

Msingi/Malezi bora...

Habari gani? Kuna watu walikosa Malezi(Msingi) bora utotoni, malezi bora sio kula vizuri, kuvaa vizuri na kusoma shule nzuri bali kulelewa katika Mazingira ya Heshima na Adabu (kwako na kwa watu wengine), Staa/Stara, Uvumilivu, Kuridhika, Kutokata tamaa, Utu na Haiba. Hivi majuzi nimekutana na mtu akaanza nipa stori za mambo na vitu Ghali anayomfanyia Ex wake....nadhani alitaka kufikisha ujumbe kuwa yeye ni mtu wa kujali sana na kutumia Mahela kwakwe sio tatizo. Kwa bahati mbaya alikuwa hajui kuwa mimi ni Mwanamke (a bit tofauti) sibabaiki na Mahela ya watu kwani naamini ninauwezo wa kutafuta na kupata zangu.....pamoja na kusema hivyo zawadi napokea hihihihihi! Stori zikaendelea huku nami (kama kawaida) nikiuliza maswali...."Kwanini unamhudumia Ex wakati una mwanamke mpya?"...."Kuna kitu unataka au unapata kutoka kwa Ex"..."Je, Ex ana siri zako nzito unaogopa atazitoa"? n.m(na mengineyo). Kabla hatujaagana chi

Phd...

Naitaka sana yaani, sitaki kuzeeka bila kuipata....shughuli inakuja ni lini hasa nitarudi "shule"? Baada ya kupiga mahisabati nadhani by the time nagonga Miaka 50 Mwenye enzi Mungu akibariki mwanangu wa Pili (mwisho) atakuwa kwenye Teen kati hivi na huo ndio utakuwa muda mzuri. Nia sio kupanda Cheo au kugombea Uwaziri(Ubunge) la hasha! Ni kutimiza Malengo niliyojiwekea kuwa kabla sijazeeka niwe na kaelimu katika levo ya "Udaktari" Dk Dinah blablabla. Sasa angalau mie nilisomaga (si ndio nkachelewa kuzaa!Nilitaka kula life kabla ya Majukumu).....Mambo ya kutoka Binti wa_____ to Mke na Mama wa_____ in my early 20s haikunivutia....Ningeishi Mimi kama mimi lini sasa eti?!!! Anyway, kwa wale "baadhi" walioamua kuanza na Mke na Mama wa_____ hu kurudi "shule" baada ya watoto kukua which ni kitu kizuri ila unakuwa "hujayafaidi" maisha ya Usichanani....ule uhuru wa kutokuwa na Majukumu au kufikiria watoto na Mum

Pale Mwenza aongea kwa Code na rafiki zake....

Alafu mkifika nyumbani anaku-de-code-a yote....hapo sasa ama utadanganywa kabisa au utapewa robo ya ukweli(utadanganywa kwa robo tatu). Unajua upokwenda kutembelea watu mnaofahamiana au unapokuwa kwenye shughuli kwa kawaida inayojumuisha watu mbalimbali baadhi yetu tunaofahamiana/juana sana huongea kwa "Code" au unavutwa pembeni kisha unaambiwa jambo au kuombwa Msaada. Nia na madhumuni ni ili watu wengine wasielewe, wanasahau kuwa watu tunaupeo tofauti, baadhi "tunadikodi" hapo hapo......wengine ndio mpaka wasubiri "wadikodiwe" na Wenza wao watakapofika nyumbani. Natumai unaendelea vema, mimi leo bana sijielewi-elewi, yaani ka' nimepigwa au nimefanya kazi ngumu sana ningekuwa kwetu(KissWay) ningesema "nililimishwa" Usiku wa kuamkia leo. Heri ya Wiki Mpya! Babai. Mapendo tele kwako...

Ugumu wa Masomo...

Hisabati....Hisabati....Hisabati! Sikufanya Mtihani wa Mwisho kwasababu nilijua nitapata LieFu.....sikulitaka Li-F kwenye Cheti changu. Nikapiga Mahesabu ya namna ya kuepuka F kwenye Cheti changu cha Fom Foo....nikapata jibu deshi-deshi, ila mie nilitaka Deshi moja tu so siku ya Mtihani sikutokea.....nikajipatia Mathematics-!! Nilifurahiiiiiii. Nazipenda Hesabu (kuhesabu hela na Pea za viatu tu) ila kama somo hapana, sio kwamba nilikuwa siziwezi la hasha! Nilikumbuka Kanuni zote, nilifuata na kupatia njia ili kupata jibu. Tatizo lilikuja Muda napoteza muda mwingi kuhakiki jawabu matokeo yake najikuta nimefanya Maswali 5 out of 25=Efu...SIPENDI Somo la Hisabati sababu speed ya akili yangu ni a bit slow. Hakuna kitu kinachoniudhi kama kuishiwa Muda wakati wa Mtihani......Baba (Merehemu) alikuwa ananiambia "ukitaka akili yako iwe "sharp" na kuongeza uwezo wa ku-focus kwenye hesabu, fanya Mzoezi ya Hesabu mahali ambapo kuna k

Michezo ya Utotoni 90s

Jambo! Msita (Mdako), Dama, Marede, "Amina sasa naomba, turudiane...hayo yamekwisha kipenzi changu" yaani kuruka Kamba....don't you miss them au wewe ulikuwa wa Kishua unashinda kubebelea ma VHS ya akina Comando Kipensi....?? Usiseme ulikuwa unacheza Game, enzi hizo Bongo hakukuwa na Games za Tv achilia mbali PCs....Tv zenyewe zimechanganya 1994. Nilikuwa mzuri sana kwenye Marede na Mdako(Msita kwa wale wa pande za Shinyanga na Mwanza). Nikikamata Jiwe kwenye Mdako sikosei....kwenye Marede kila Timu ilinitaka mimi (niligombaniwa). Marede ya kujaza Chupa kwa mchanga niliipenda lakini sikuruhusiwa kuicheza kwasababu ya vumbi(Nilikuwa na Pumu). Ila nilikuwa naibia....kisha narudi ndani nimebanwa....kupumua siwezi....jicho limetoka ka' Ndula(unazijua Ndula weyeeeee)....hehehe. Naishia kuonewa huruma na kupewa na kupewa ile Inhaler, kisha nakuwa nimerudishiwa Uhai.....Nashukuru Imeisha (sijabanwa Tangu nilipofikisha miaka 21).

Heshima kwa Maiti...

Imepotelea wapi? Au ndio kwenda na Wakati? Juzi kati nimekutana na Picha ya Maiti ya Mpendwa wangu....pamoja na familia kufanya kazi ya ziada kuzuia upigaji Picha wa shughuli nzima ya Mazishi achilia mbali Mwili wa Marehemu wa mpendwa wetu zaidi ya alieajiriwa kwa ajili ya kazi hiyo....bado kuna jitu likapiga picha na ku-share online. Kwasababu hana Uhai tena haina maana kapoteza Haki zake kama Mwanadamu mpaka atakapozikwa(Fukiwa). Maiti ingeweza ingejisitiri na kupozi ili apendeza au kutokea vizuri zaidi....pia angechagua ni Picha gani itumike kutangaza Tukio lilipolekea Mauti kumfika. Unapata faida gani ku-publish au ku-share picha ya Maiti?.....kwanini unataka tumkumbuke Marehemu kama Maiti na sio alivyokuwa Hai na mwenye furaha?!! Unaweza kusema naegemea kwa Waingislishi kwa vile naishi huku na wao hawana utaratibu wa kuonyesha Maiti au kuiaga zaidi ya Jeneza na Picha ya Marehemu alipokuwa hai....nia ni kubaki na kumbukumbu ya yeye

Radio za Dini

Hiyaaaaa! Umewahi kuzungumzia Sheria za Dini ya Kiislam dhidi ya Wanawake kwa Binti wa "kisasa" wa Kiislamu ukasikia anavyojitetea!....Hadi huruma. Kuna siku mmoja aliniambia Uislamu hauna budi kubadilika baadhi ya Sheria na kwenda na wakati.....sizungumzii wale Waislamu wa Mwezi wa Ramadhani to Ramadhani....la hasha! Nazungumzia wale Mabinti ambao wanaipenda na kuifuata Imani yako kwa Dhati lakini wanahisi kuna mambo kwenye Sheria ya Dini yao zinawakandamiza. Nimekuwa nasikiliza sana Radio za "Kiislam" (za Kikristo miyeyusho,kazi kuomba Michango tu).....napendezwa sana na Mafundisho yao ya Maisha, kitu pekee kinachonikwaza ni pale wanapozungumzia Wanawake....Mwanamke kwenye Imani ya Kiislam bana....daaah!(Naachia hapa). Radio za Kikristo nazo zimejaa Ushuhuda wa kipuuzi tu yaani....alafu wanaomba Michango kuliko kufundisha wasikilizake wake namna ya kuishi Kikristo.....Maombi ya Michango ya pesa 90%....Shuhuda 7% na 3

Kuchapia...

Ni Sunna....Relax! Enyi Wakaguzi wa Lugha Fasihi sijui Fasaha Mtandaoni mnahitaji kwenda kunywa dawa zenu....(Lazima mna some sort of Mental Disorder). Ailimradi unaelewa kinachozungumziwa au kilichokusudiwa unapaswa kurekebisha kichwani mwako kisha endelea na mambo mengine... Wengine tunachapa/ongea haraka na muda wa kuanza kuhariri hatuna....Mimi binafsi ni Bingwa wa kuchapia....mara nyingi nikisoma (kesho yake) nagundua kuwa nimechapia lakini bado naeleweka. Huwa nachapia hata nikiongea na watu japo sio sana, labda maneno mawili kwa siku....aiiii hebu ngoja kwanza....sasa nina watoto which means naongea zaidi....usikute nachapia zaidi ya maneno 10 kwa siku! Haulipii kusoma na alieandika halipii Kodi kuandika....tulia na furahia uwepo wako Online. Kumcheka mtu kwa vile nimekosea/chapia is bullying/Trolling.....hihihihihi! Happy new Week! Babai... Mapendo tele kwako...

Dave na Jamaly

Hawa walikuwa "my best friends" wangu yaani walifanya lolote kwa ajili yangu....baadhi ya watu walidhani jamaa walikuwa wapenzi wangu. Naelewana vema na Wanaume kuliko Wanawake, naturally, wanawake hawanipendi (I think like man most of the time) hihihihihi natania, I just don't click kirahisi na watu wa jinsia yangu. Jamaly nilisoma nae Msingi na wote tukafaulu yeye akaenda Tambaza na mie nikaenda shule moja hivi pale Mjini kati.....Bado urafiki wetu uliendelea Mpaka Chuo. Tulikuwa tunakaa Dawati Moja (yeah nilikuwa nakaa na Wavulana), tulikuwa tunapishana nafasi ya kuongoza darasa. Tulikuwa tukisoma pamoja lakini hatukuwa tukikaa pamoja kwenye Mitihani sio wajua ile kupangwa kwa herufi.....still tulikuwa tukibishana ni maswali gani yatatoka kwenye Mtihani usika. Urafiki na Dave ulianza Kidato cha Pili, na ukaendelea Mpaka naondoka Tanzania karibu miaka 17 iliyopita. Tulikuwa tukisoma pamoja kila tunapotarajia Mitihani japoku

Addicted to Dini....

Jiadhari, inaua! Wataalamu wanaamini kuwa kila Mwanadamu anaumwa Akili(anaugonjwa fulani wa Akili) na huwa triggered na aina ya Maisha anayoishi mhusika. Sasa kuna wale watu wako so dedicated na Imani zao mpaka unahisi akili zao hazipo sawa....hizo mtu zipo Addicted (Dini imetriga Gonjwa la Akili). Kama zilivyo addictions nyingine Imani ya Dini inaharibu Mahusiano, Inasababisha Mfarakano kati ya familia na familia na hatimae kupoteza Maisha au kumfanya Muathirika kuishi Maisha yale yale wakati Mkuu wa Dini (Zungu) anafurahia the High life + attention ya Jamii. Nakumbuka enzi, Mtu (kwenye familia yangu) alikuwa yupo radhi kupeleke "fungu la Kumi" kanisani kila Mwezi kuliko kuwanunua watoto wake mahitaji muhimu. Ilifikia mahali anasomesha watoto wa Waumini wengine wakati Elimu ya watoto wake haieleweki. Addiction ilinoga akaamua kuacha kazi ili "afanye kazi ya Bwana"....akawa anaamka asubuhi kwenda Kanisani na kurud

Nafurahia kuwa Mama...

Lazima umeisikia hii kwa Wanawake wengi wa kileo....Mimi sifurahii kuwa Mama (way too hard) ila najivunia kuwa Mama kwa wanangu. Kuna wale wanawake ambao wakikua tu wanatamani kuwa Mama (kuzaa) yaani kuwa mama ni muhimu kwenye "list" ya mambo wayatakayo Maishani. Mimi sikuwa hivyo, yaani kuzaa haikuwemo kabisa akilini mwangu....nilijua siku moja nitazaa, lakini sikuwa na haraka au niseme urge/desire ya kuwa na Mtoto. Hata nilipojifungua Wanangu sikupata ile hisia wanazopata wanawake wote(wengi waongo hehehehe) "falling in love like never before" au "falling in love all over again"....nilijipa "hi5" in my head nikafurahi na kuwa-proud huku nikujiuliza "kapitapitaje pale"? Haina maana siwapendi Wanangu la hasha! Nawapenda sana na siwezi kuishi bila uwepo wao....hata kwa masaa machache yaani SIWEZI. Ila Mapenzi kwa wanangu hayakuhitaji mimi ku-fall in love na Mapenzi kwa Mtu baki ndio huita

Nafurahia kuwa Mama...

Lazima umeisikia hii kwa Wanawake wengi wa kileo....Mimi sifurahii kuwa Mama (way too hard) ila najivunia kuwa Mama kwa wanangu. Kuna wale wanawake ambao wakikua tu wanatamani kuwa Mama (kuzaa) yaani kuwa mama ni muhimu kwenye "list" ya mambo wayatakayo Maishani. Mimi sikuwa hivyo, yaani kuzaa haikuwemo kabisa akilini mwangu....nilijua siku moja nitazaa, lakini sikuwa na haraka au niseme urge/desire ya kuwa na Mtoto. Hata nilipojifungua Wanagu sikupata ile hisia wanazopata wanawake wote(wengi waogo hehehehe) "falling in love like never before" au "falling in love all over again"....nilijipa "hi5" in my head nikafurahi na kuwa-proud huku nikujiuliza "kapitapitaje pale"? Haina maana siwapendi Wanangu la hasha! Nawapenda sana na siwezi kuishi bila uwepo wao....hata kwa masaa machache yaani SIWEZI. Ila Mapenzi kwa wanangu hayakuhitaji mimi ku-fall in love na Mapenzi kwa Mtu baki ndio huitaji

Rafiki wa kweli...

Haitaji kuku-support kwenye kila jambo hata kama ni baya! Kama ukikosea atakuambia ukweli hata kama unauma....akiku-support kwenye kila kitu ujue ni MNAFIKI. Ndio maana Mimi sina Rafiki bali nafahamiana na watu....oh wait! Actually ninarafiki Mfamasia nilikuwa nae Chuo in olden days....labda kwavile ni Mghana so tofauti ya Kacha imefanya Urafiki Udumu. Sijui wenzangu mlilelewa vipi lakini kukosolewa ni muhimu kama kusifiwa. Ilikuwa unakosolewa kwa kinachokosoleka (ujinga/upuuzi ulioufanya) mbele ya wenzio so that usirudie tena upuuzi wako. Usiogope kuitwa "double standard" akienda ovyo mpe cheupe ajirekebishe. Babai... Mapendo tele kwako...

Kujiremba....

Kipajiiii....heri ya Alhamisi! Nilipokuwa Msichana 10-17 sikuwa najali mambo ya kujiremba....Mama hakuturuhusu kupaka Rangi ya Kucha Ijumaa kisha tuondoe J'pili jioni. Eti tulikuwa tunaharibu Rangi zake... Basi tukawa tunapaka Wino mwekundu(Pen nyekundu) au ukitaka Rangi "clear" au kucha zing'ae basi unachukua Marumaru au Vipande vya China (sahani, vikombe n.k vilivyovunjika) unasugua kwenye Sakafu ya Sementi kisha ile vumbi yake unaisugua kuchani. Nilipofikia Miaka 18 nikaanza kupaka Wanja na Lip gloss. Nimeanza kujipangusa Poda usoni, kutinda Nyusi na kupaka Mascara nilipokuwa na miaka 28....anyways! Baada ya kuwa addicted na Beauty Vlogger nikaamua kujitutumua kwenye kujiremba bana....basi siku ambayo najua sitoki nje mwenyewe napanga nitakavyo vyaa the next day na Vipodozi gani vya kujipaka....(Ninavyo kibao kwani kila Birthday napewa zawadi ya Vipodozi....watu wachokozi)! Naamka mapema, nafanya shughuli zangu za ndan

Mti/Ua Shamba....

Yenye viwango na Uchunguzi wake umefanywa kisasa.....(Wataalam wa Sayansi) sio wale wa "Maono"....The wezi. Oh! Heri ya Juma Nne....Hongera na ahsante kwa kuichagua Blog hii. Ile Nywele issue (bado ninayo) bana inanifanya nijifunze mengi kuhusiana na vitu asilia ambavyo vinamanufaa mazuri kwa mwili wa Binadamu ikiwa ni pamoja na nywele. Kunywa maji ni muhimu kwa ajili ya ngozi, nywele na kupunguza Mafuta Mwilini kwani inakuzuia kula chakula kingi/kupita kiasi.....ila ukiwa ulibeba mtu mbili Tumboni eh bwana lazima uwe mwangalifu na maji unywayo. Unakunywa "Fundo" ndogo mbili na sio kumimina robo/nusu Lita kwa wakati mmoja....unaeza pata Mimba atifisho a.k.a Kitambi....(Hata sijui kwanini nakuambia hili)! Oooh! Back to Miti shamba, ninayotaka kuizungumzia hapa ni Chai.....huyoo ulidhani mizizi na Magome? Hehehehe....Chai ya Kijani na ile ya Maua aina ya Chamomile. Come to think of it, Mizizi na Magome hutumiwa kama

Mabadiliko ya Ngozi

Naamini au niseme kuwa nadhani nina ngozi nzuri, kwamba si nyeusi na si nyeupe. Ila tatizo linakuja kwenye mabadiliko yake kutokana na Hali ya hewa inavyobadilika. Awali wakati naishi Tanzania ngozi yangu ilikuwa inachukia Mafuta Mazito, hivyo nikawa napaka mafuta ya "maji" ya asilia ambayo ni ya Nazi. Baadae nikagundua aina fulani ya "Lotion" nikawa nachanganya Mafuta ya Nazi na kupaka mwilini (usoni incl). Kipindi chote hicho sikuwa naona mabadiliko ya Rangi ya Ngozi yangu kama ninavyoiona huku Ulayani. Yaani wakati wa Baridi na kipupwe Ngozi yangu inakuwa Nyeupe (napauka)....alafu wakati wa Kiangazi naiva (Rangi inakolea).... Nikadhani labda macho yangu yanaumizwa kutokana na Mwanga wa jua wakati wa Kiangazi ndio maana najiona "nimeiva). Siku nikaenda kwa Daktari kumueleza tatizo langu hehehehehe I know(am so stupid....not really mie muoga wa Magonjwa bana)....nilidhani labda ni dalili ya Ugonjwa wa Michael Jac

1st time Mothers....

Za mida hii....? Enzi zile za Usichana(shuleni) kulikuwa na kipindi cha watoto "chuchuchu" kilikuwa kikiendeshwa na Marehemu Amina Chifupa(Pumzika kwa Amani). Alipojifungua basi kila wakati ilikuwa "nani huu hivi, nanihu vile" yaani ali-share excitement ya kuwa mama kwa mara ya kwanza. Mimi na wanafunzi wengine, tulikuwa tunakereka kweli na hiyo "mwanangu hivi, vile".....tukawa tunasema "Amina nae ka' yeye ndio wa kwanza kujifungua, Ulimbukeni tu!! Kumbe bana tulikuwa wadogo, hatukujua hisia anazozipata mwanamke baada ya kujifungua kwa mara ya kwanza. Niulize mimi nilipojifungua mara ya kwanza hehehehehe nilikera watu kwa picha na vijimaandishi vya kuwakilisha vitendo au pose yake kwenye Picha. Hakika niliwakera watu sana tu. Namkumbuka Marco Mwenda (nae ni marehemu alifariki kwa ajari ya Gari mwaka Jana, apumzike kwa Amani)....aliwahi kuniambia " Da' Dinah nawe unachosha, utadhani wewe ndio mama wa kwanza hapa Duniani"...

Kesi za Kubaka za Miaka ya 70s-80s....

Bari gani? Hizi Kesi na Hukumu zinazotolewa huku dhidi ya "vibabu" waliobaka au ku-abuse wasichana wadogo miaka 40 iliyopita zinaudhi eti! Unaeza sema "masikini vibabu vya watu vinafungwa bure kwa makosa ya miaka ile".....au ukajiuliza "hao wanawake walikuwa wapi tangu enzi zile kupeleka Mashtaka yao". Well! Huwezi kuelewa mpaka uwe umepitia huko au wewe ni mwanamke na unakuwa targeted kwasababu tu una Matiti na Uke. Sipendi kulinganisha lakini linapokuja suala la ku-abuse wanawake kingono hasa sehemu za kazi Tz, mimi ni mmoja kati ya wengi ambao tulitishiwa kufukuzwa (kunyimwa ajira ya Kudumu) kama tutakataa kujitoa kimwili. Wenzangu sijui, lakini mie na misimamo yangu nikamwambia "unikome ka' ziwa la mama yako na sina shida na Kazi yako".....nikatoka, mefika nyumbani nikaenda kumshitaki kwa Mama na Baba (hihihihi hapo nilikuwa Binti wa miaka 25). Sijui sheria ya Unyanyaswaji wa Kijinsia na Ubaka

Comments kwenye Gazeti la "kushika"

Jambo jambo? Sijasoma Gazeti la kushika kitambo kweli, asa nipo Trenini nasoma Gazeti la asubuhi, baada ya kusoma sinkawa natafuta "comments" ili nisome maoni ya watu....ikabidi nijicheke! Wiki ijayo kuna Uchaguzi wa Wawakilishi wa Ulaya, Hakuna chama kinachonifurahisha mpaka sasa. Nikieka majina ya Vyama hapa nitaanza kufuatiliwa kwa karibu na siku nikitereza tu narudishwa Kisarawe, so wacha wabaki "kapuni". Sijui umuhimu wa Umoja wa Ulaya kwangu binafsi zaidi ya kushikilia Bango Haki za Binadamu, hivyo nitapiga kura ili tubaki kwenye umoja huo kwa maana hiyo sitochagua yeyote anaetaka tutoke kwenye Umoja wa Ulaya. Siasa inagusa Maisha yangu, napenda Siasa ila nimeacha kufuatilia zile za Nyumbani kwani hunipa hasira alafu hazinifaidishi. Za huku zinaeza kukupa hasira (kama umekatiwa msaada wa senti hihihihi) lakini angalau unapewa nafasi ya kumtumia Mbunge wako kwa issues ambazo labda hazikutiliwa maanani na wajinga

Kila Kidume(secretly) hupenda kidume Maishani....

Hapana sio "Mikorosho" bali kupata/zalishiwa mtoto wa Kiume......Heri ya Wiki Mpya kwako! Umewahi kutana na wanaume ambao watoto wao wa kwanza ni wa Kike, na ukasikia wanavyotetea Binti zao na kuponda watoto wa kiume au hata kujifanya "hawajali" mtoto gani anazaliwa. Wengi hudai "Bora Binti Malaya kuliko Kidume Shoga"....ukielewa Sentesi hiyo kwa undani utagundua kuwa Msemaji hapendi watoto wa kike na kesha Muita Malaya kabla hata hajakua masikini. Hawana mtoto wa Kiume hivyo "ushoga" hausiki (hauna nguvu) hapo lakini tayari wamuita Binti Malaya....haa! Kisiri-siri wanatamani sana na pengine waliombea kupata mtoto wa kiume lakini haikuwa hivyo..... Wengine husema "Mheshimu Mkeo kwani kakuzalia kidume muendeleza jina la Ukoo" Mimi binafsi SIKUTAKA kabisa kuzaa mtoto wa Kike kama 1st born kitambo kabla hata sijajua kama ipo siku nitazaa. Nadhali ilitokana na hali ya kujisikia "safe" na kuheshimiwa (ogopwa) kwa vile nilikuwa na m

Marehemu....

Mungu aendelee kuwapa Mwanga wa Milele, Amina......hebu ngoja kwanza!! Wameenda wakiwa "wamelala" sasa mwanga wanini wakati wamelala? Ile kasumba ambayo mimi naona ni ubinafsi au kutafuta/taka kuonewa "huruma".....yaani marehebu baba blablabla....Marehemu sijui nani blablabla. Marehemu Baba wa Taifa anatuangalia na kugalauka Kaburini......yaani aache kufanya yaliyomuhimu huko aliko abaki kutuangalia sisi huku na kugalauka kutokana na ujinga au makosa na shida zetu! Sidhani kama hao marehemu huwa hata wanatuombe tulio hai tuendelee kupata "kiza" cha milele ili tusiamke na kukabiliana na shida za Dunia. Mtu akienda, ameenda na huna budi kukubali kuwa kaenda na anaendelea na maisha mengine bila wewe....dizaini ukifa unasahau all bout Dunia na watu wake.....Mambo ya new start...new life. Si wanasema unakuwa "declared dead only" kama Ubonko (Ubongo) haufanyi kazi, sasa kama Ubonko haufanyi kazi kumbukumbu za ya Duniani watazitoa wapi? (In my

Fashenista....

Za jioni? Kabinti kanakua basi sijui ni homono au au kitu gani?!! Khaaaaaaa! Hakajui kuongea basi kila kitu ni "this...this" huku kanasonta (nyooshea kidole) anachokitaka. Unamvalisha Viatu, anaenda kubeba Viatu vingine anataka umvishe juu ya vile ulivyomvisha mwanzo.....Uanamke shughuli, tena kumbe shughuli huanza mapema hivi! Aiiiii.... Ujue...kunatofauti kati ya Kupenda Fashion na Kujua Fashion. Mimi napenda sana tena sana ila sifuati sheria zake(well sizijui na sina muda), navaa ninavyotaka au kujisikia. Sasa kwavile tu napenda Fashion hainipi ruhusa au Mamlaka ya kukuambia uvae nini na wakati gani wakati vaa yangu tu inaashiria nahitaji kuambiwa ninayowaambia wengine. Tangu nimegundua Vlog ayeee nimekuwa addicted, sadly wengi wao ni 20s, which is annoying. Few days ago....oh kiswanhehee....siku chache zilizopita nikakutana na Vloggers ambao wapo 30s aiii nkajiSubie (subscribe). Sasa najifunza kuwa stylist.....natania, una

Kilugha kinakera!

Morning/Noon! Lugha za Tanzania zinaingiliana hivyo hazikeri alafu lazima utaambulia maana kwa mbali hasa kama unatetwa. Kuna Mtangazaji "Tiger beibiiii" wa Ebony ya Iringa huwa ananikosha sana akitumbukizia/nogesha kwa kilugha chake, sio Watangazaji wa Dar wamejaa "you know what I mean" "waraaaap" nyiingi....hiyo sio nukta, nimegusia tu. Lugha za Nchi hii bana ayee! Kichina, Kinigeria, Kipolishi, Kizairwaa, Kisomali, Kirusi na nyingine nyingi....zinakera sana (kwasababu sing'amui kitu). Asa ombea umepanda Basi Moja na Mnaija, Mkongo na Mchina, alafu wapigiwe simu kwa wakati mmoja....Utadhani wamekodisha basi kwa ajili yao tu. Sikuhizi nawaelewa sana Wainglishi wanapoonyesha kukerwa unapoongea Kilugha chako....(Sehemu ni wivu as hawajui lugha nyingine hihihihihi). Huwa siongei Kiswahili ninapokuwa kwenye kadamnasi ya watu ambao najua hawaelewi na kama mazungumzo ni nyeti (lazima kilugha ili wengine was

Daktari na Dawa wanazotupa....

Jambo weye? Umewahi kwenda kwa Daktari ili kuongezewa Dawa unazotumia (repeat prescription) Daktari akakubadilishia Dawa akikuambia "hii ni bora zaidi" kuliko hiyo?!!! Unahofia "side effects" lakini Daktari anakuhakikishia kuwa hakuna baya litakalotokea (niligundua kuwa dawa mpya ni Ghali zaidi kuliko ile ya awali). Jana natazama Documentary (yeah am that boring) nkajifunza kuwa hawa Madaktari tunaowaamini wakati mwingine wanatupa Dawa kama majaribio bila sisi kujua. Na wakati mwingine wanakula Deals na Makapuni ya kutengeneza Dawa ili kufanya Dawa husika kuwa popular au kama sehemu ya Uchunguzi. Ile "kama utapata tatizo lolote tafadhali nipigie simu haraka" hiyo ni report muhimu sana kutoka kwako kuhusu dawa husika. Ushindani wa kuuza Dawa kwenye Makampuni hayo ni mkubwa sana, imefikia mahali Madaktari wana-creat "Disorders" na kula Deals na Wafamasia ili kutengeneza Dawa "kutibu/tuliza Disorders&

Wanyumbani na Wanje....

Heri ya Wiki Mpya! Siku hizi wa Nyumbani na wa Nje zimekuwa "jamii" mbili tofauti wakati zamani tulikuwa kitu kimoja ailimradi tu sote tunatoka Nchi mmoja iitwayo Tanzania. Kuna kama kaushindani au kaubaguzi ka chini kwa chini hivi....well, nilishakuambia kuja Nje siku hizi sio deal labda ndio maana wa nje tunadharauliwa hihihihihi. Alafu tunajifanya tunajua sana utatuzi wa matatizo yanayojiri nyumbani wakati wengine hatujagusa huko mwaka wa Tano huu....kazi kufananisha tu "Kwa mfano huku blablabla" sort of people. Pia kuna wale ambao wapo Nyumbani kazi yao kulinganisha pia....wale akina "when I was in London" kind of people...."Hata wenzetu wa Ulaya blablabla" wakati hujawahi kuishi huko au ulikaa si zaidi ya tumiaka 3. Wote hamna tofauti linapokuja suala la kujifanya mnajua utatuzi wa matatizo yanayojiri Tanzania (hasa kijamii, kisiasa na kiuchumi). Sie wenye watoto wadogo haturudi moja kwa moja

Hoarders....

Hello! Mambo! Wadogo zangu wa Kike enzi zile walikuwa wakiniita....wacha ni seme tu bana....najulikana kwetu kama "mchafu" sio kwamba siogi, sishafishi nyumba au kutandika kitanda la hasha! Nilikuwa nafanya hayo yote in my own time....sio ukiamka tu unakimbilia kuosha vyombo(which I hate) au kupiga deki na kupangusa vumbi incase wageni watakuja.... So nilikuwa na-swap kazi hizo na yeyote mwenye zamu ya Kufua au kunyoosha....nazipenda kwavile zinafanywa baadae....pia napenda kusafisha choo/bafu (huwa nasafisha usiku)....hihihihi. Asa siku moja mume wa mimi na mimi tulikuwa tunaangalia kipindi kuhusu Hoarders....hee, mkibaba akaniambia wee mwenyewe ni "hoarder" aiiii niliumiaaaa mpaka nikakaribia kulia! Wacha nianze kubisha(vere mbishi nikiwa na uhakika, tabisha mpaka kesho yake) na kuthibitisha maana ya Hoarders....nikisisitiza kuwa ni Ugonjwa wa Akili. Kesho yake nikaenda "store" nikakutana na Masanduku na M

Lete Ushahidi wa unachoongelea...

Hello DHB/DHW member....year 2003 lazima umezaaka hihihihi maana mie tu niliekua katoto mekuwa kibibi(no, not princess, ni kibibi as in Mzee).....drop me a line please!! Enzi hizo bana, kulikuwa na malimbukeni wa Elimu ya juu kibawoo au niseme Wasongo....ukisema kitu online lazima wakuambie uwape/utoe vielelezo au statistics. Yaani walitufanya sie wa Elimu ya Chini going on to Elimu ya Juu(enzi hizo) tujione "hamna kitu" kabisa, tulinyimwa haki ya Msingi ya kusema tulichojisikia au tulichotaka au kukijua . Ukiongelea kitu bila kuwapa "ushahidi" wanakuambia unaongelea mambo ambayo "unadhani" unayajua, lazima mtu uwe na ushahidi wa kuthibitika kuwa unachozungumzia "umesomea" au unakisoma. Siku hizi aiii unapewa kielelezo cha picha inayotembea na sauti kabisa tena bila kuomba....shukurani kwa Teknolojia na urahisi wa ku-share yale tutakayo/ujisikiayo. Kwaheri kwa sasa. Mapendo tele kwako...

Celebs

Hii jamii ina power ya ku-normalize kila kitu, hata vile ambavyo ni normal lakini jamii nyingine hawavifanyi, wao hu-normalize. Mfano ni "attachment parenting" ambapo mama analala na mtoto wake na kumnyonyesha for as long as possible. Hiyo "attachment parenting" si ni kitu cha kawaida kwenye jamii ya Kitanzania(na Afrika kwa ujulma)....nimezaa mwanangu wa kwanza nikapigwa marufuku kulala nae ili kuepusha cot death. Nikakumbuka Mama alipozaa wadogo zangu 3 wa mwisho, wote alikuwa analala nao kitanda kimoja na hakuna aliepoteza maisha.... Aii....nikawa na lala na mwanangu ka' ifuatavyo na amenyonya mpaka mwaka na miezi 3. Siku hizi analala chumbani kwake lakini akiota ndoto mbaya anakimbilia kwetu so tunalala wote wanne. Huyu wa pili bado analala na sisi na bado ananyonya (mwaka na miezi 3) tena huyu ni king'ang'anizi kuliko kaka yake ambae hakujali kulala peke yake au kulala na sisi.. Kingine ni Kuzaa kwa kupasu

Uswahili Mzigo...

Halo, haloooo....Halo ya Mbuzi meeeeee! Kuna tofauti kati ya Uswahili way of life which ni kitu cha kujivunia, ni kama "culture"....alafu kuna Uswahili "ile hali ya kutokuwa Mstaarabu" na Uswahili simply kwavile wewe ni mwafrika(Muafirika). Wenzetu wa Kishua hawapendi Uswahili kabisa yaani! Wao wanaishi Kizungu zaidi....usiniulize kwanini wengi wao wakifika Uzunguni (Ulaya, Marekani, Down Under etc) wanakuwa Waswahili kupita wale Waswahili wa Mtaani kwetu pale KissWay(Kisarawe). "Unaedha" dhani kuwa wamebadilika, hapana hawajabadilika bali kuishi "Kizungu" Ulaya inabidi uwe Posh....U-posh waenda sambamba na Pochi(mahela).....sasa inawezekana kabisa tuhela twako + rangi yako, Elimu na ulikotoka inakuwa ngumu kidogo kuishi "kizungu" kwa Wazungu.....sijui umenielewa?!!! Sasa unaishia kuishi na Waswahili wenzako "wa Kizungu" ambao awali hukujua tofauti yao kati ya Middle class, Working class, Chav n.k Kama tunavyojitenga Tanzania

Baba zetu nao...

Wiki Mpya oyee! Nimeacha kujivunia Tanzania kama Taifa(Kisiasa) miaka kadhaa iliyopita, najivunia Tanzania kama Nchi na baadhi ya Tamaduni zake, kama vile kuvaa Vibwaya (vile vifupi, kuachia tumbo na kufunika Matiti), Ngoma na nyingine nzuri nzuri. Kuna unataratibu wa baadhi ya wanaume kudai kuwa mwanamke yeyote atakaelala nae ni Mama yako na mtoto yeyote atakaezaliwa na mwanamke ambae sio Mama yako ni Ndugu yako. Sina uhakika kama ni Utamaduni,Tabia au pure______! Mama yako ni yule aliekuzaa au "kisasa" aliekulea tangu ukiwa na umri wa masaa au siku chache.....sio random women aliolala nao Baba yako. Pia ndugu yako ni yule mliotoka tumbo Moja, wengine ni Jamaa (tena ukiamua kuendeleza ujamaa huo kwani sio lazima). Tabia ya Baba kulazimisha watoto wao kuwaita wanawake wengine Mama au watoto waliozaliwa huko (kabla au baada ya Ndoa) wadogo/kubwa zao sio haki na sio sahihi kwa mtoto/watoto husika. Huyo ni Mkeo na hao ni watoto wako w

Mkorogo...

Habari... Mkorogo ni kutumia bidhaa "illegal" au "home made skin lightening" na "kujiton" ni kutumia bidhaa zilizothibitishwa na Jamaa wa Ubora wa Viwango eti?.....wote nia yao Moja. Waafrika kwa Waafrika kwa ubaguzi wa rangi zetu hatujambo....tofauti ya Ubaguzi wetu sisi Watanzania ni kuwa hatutengani au kuuana kwa sababu baadhi yetu ni weusi sana au weupe sana. Well, isipokuwa kama wewe ni Mweusi tii alafu huna nywele laini na unaishi Somalia au Sudani Kaskazini.....oh au Chotara ndani ya South Africa. Ila Machotara ndio huwa wabaguzi zaidi kwa Weusi kuliko sisi wenyewe kwa wenyewe....Usiombe ukutane na Chotara wa Kizungu aliekubaliwa kwenye jamii ya Kizungu ayeee!! Anyway, nukta hapa ni kuwa tofauti ya weusi wetu wa ngozi ndio hutufanya tuwatanie wenzetu na kuwaita majina....Mf: Cheusi dawa, Mpingo,Cha usiku n.k Huu utani huwafanya baadhi(hasa wanawake) wajisikie wanyonge, hawavutii....inafikia mahali wa

Usinijaji....

....relax is a human nature! Tangu u-single mother umekuwa "fashion" vijana karibu wote wa late 20s na early 30s walishazaa huko nyuma, hivyo ni ngumu kweli kukutana na mtu ambae ni "m-clean" ka' wewe (hana mtoto/watoto). Shughuli inakuja kwa sie tuliozaa(Oa/Olewa) na Wanawake/Wanaume ambao washalizaaga "ujanani" huwa tunajajiwa sana yaani. Unaonekana "Mwizi" kwenye jamii na familia, hata mtoto aliezaliwa kabla wewe hujakutana na Baba/Mama yake uhisi kuwa wewe ndio sababu ya Baba/Mama yake kula Buti la pua ( I know how it feels cause I was a kid once). Unaenda mahali na Mumeo/Mkeo na tutoto twenu (bila yule wa kabla) watu wanawasonta-sonta (Shinganya Oyee!! Kusonta ni kukunyooshea kidole kama ulikuwa hujui)....anyway! Wengine bila haya wanaanza kuuliza "nanilihu na Mama/Baba yake hawajambo" mbele yako just to piss you off....Mindugu mingine Mikosi kweli!!? Inafikia mahali unajistuki

Kufananishwa/Linganishwa....

Jambo! "Baba yangu alikuwa bla bla bla kwanini wewe usi bla bla bla kama yeye" kaolewe na Baba'ko sasa (this apply to wakibaba pia, kaoe Mama yako sasa eti).... Kama tulivyozaliwa Nyakati, Siku na Dakika tofauti ndivyo ambavyo tunapaswa kuishi tofauti(na wazazi wetu). Utaishije maisha waliyoishi wazazi wako wakati wewe ni mtu tofauti na unaishi kwenye Nyakati tofauti na wao? Kuna zile "manners" nzuri ambazo ni muhimu maishani na kila familia inapaswa kuwafunza watoto, mfano Kusalimia, Kuomba, Ukarimu, Heshima, Kushukuru, Msamaha.... Kama utafananisha hizo hakunaga mashida, mengine yaliyobaki yaache yabaki huko huko yanako stahili. Ungependa kuwa au kuishi na mtu kama Baba/Mama yako? You need to go out a bit more rafiki.....by out I mean OUT OF YOUR COUNTRY!!! Kwaheri kwa sasa. Mapendo tele kwako...

Kujipendekeza Kipaji....

Helloooooo! Napenda kuandika mambo ambayo watu huogopa kuyasema lakini yanawakera...kwanini? Sababu sinywi Pombe hehehehe...! ....Kwa kawaida Ndugu wa mume hupaswa kuwa karibu na wewe (hata kwa ku-pretend) ili ujisikie umekaribishwa kwenye Ukoo eti...kwa Kacha yetu ya Kitanzania. Mwenyewe unajitahidi kuweka mawasiliano ya karibu....wao walaa(mpaka uwatafute)! Unajipa moyo labda wanashughuli nyingi na muda hawana, unasubiri siku mbili-miezi mitatu still Jiiiii....hee unaanza kujistukia, unataka kumuambia Mumeo lakini unaona noma. Maana wengine hawachelewi kukuambia "unataka kutugombanisha, we mwanamke tu....wale ndugu zangu"....so unaugulia Moyoni. Kujipendekeza mwisho mara 3(in my head), unajaribu kwa Mwaka mzima wao hawajitumi kukutafuta hata XMas to Xmas! Sina marafiki kwa ajili hiyo(sijui kujipendekeza, najaribu....usipoweka effort nafunga Ukurasa na songa mbele..... Unajiuliza nani atanizika "nikikufa